KULIKONI MALIPO YA WAKANDARASI

KULIKONI MALIPO YA WAKANDARASI

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Mkandarasi anawajibika kutekeleza mradi aliyopewa kwa kiwango kinachokubalika na baadaye hukaguliwa na kama mradi umekidhi kiwango basi anatakiwa kulipwa haki yake. Kwa siku za karibuni mambo siyo rafiki sana kuhusu malipo ya Wakandarasi hasa TARURA.. Mkandarasi unamaliza kazi na hatua zote zimepitiwa mpaka ukaguzi halafu unaambiwa kuwa usubiri malipo. Ikumbukwe kuwa Serikali kwa makusudi mazima iliongeza tozo ili barabara za vijijini ziweze kutengenezwa lakini mbona hali ya malipo siyo kama ilivyoahidiwa?. Naona hapa kasoro hizi siyo za TARURA ila ni za Serikali. Inavyoonekana TARURA Makao makuu hawapewi fedha na Serikali kwa wakati ndiyo maana mambo kama haya yanatokea. Ninashauri mkandarasi anapomaliza kazi yake basi alipwe mara moja.
 
Hapo kabla ya Serikali hii ya Awamu ya Sita hali ya malipo ilikuwaje?
 
Mkandarasi anawajibika kutekeleza mradi aliyopewa kwa kiwango kinachokubalika na baadaye hukaguliwa na kama mradi umekidhi kiwango basi anatakiwa kulipwa haki yake. Kwa siku za karibuni mambo siyo rafiki sana kuhusu malipo ya Wakandarasi hasa TARURA.. Mkandarasi unamaliza kazi na hatua zote zimepitiwa mpaka ukaguzi halafu unaambiwa kuwa usubiri malipo. Ikumbukwe kuwa Serikali kwa makusudi mazima iliongeza tozo ili barabara za vijijini ziweze kutengenezwa lakini mbona hali ya malipo siyo kama ilivyoahidiwa?. Naona hapa kasoro hizi siyo za TARURA ila ni za Serikali. Inavyoonekana TARURA Makao makuu hawapewi fedha na Serikali kwa wakati ndiyo maana mambo kama haya yanatokea. Ninashauri mkandarasi anapomaliza kazi yake basi alipwe mara moja.
Serikali haina pesa

Kufanya kazi na serikali ni useless

Heri utafute product wananchi watakayoipenda maana ni waaminifu na ndio wenye hela na ndio hununua vitu na services na sio serikali

Serikali hua ni problem whenever it touches anything

I really despise government na watu wake
 
Hapo kabla ya Serikali hii ya Awamu ya Sita hali ya malipo ilikuwaje?
Mkuu, unazungumzia malipo ya wakandarasi kabda ya awamu ya sita?!!! Tambua kwamba kazi nyingi za serikali(hadi kufikia 90%) zilikua zinafanywa na ama TBA au SUMA-JKT, au Nyanza au Songoro au Wachina na makampuni mengine ya nje ya nchi. So wazawa walikua hawalalamiki kuhusu malipo sababu kandarasi zenyewe walikua hawazipati
 
Mkuu, unazungumzia malipo ya wakandarasi kabda ya awamu ya sita?!!! Tambua kwamba kazi nyingi za serikali(hadi kufikia 90%) zilikua zinafanywa na ama TBA au SUMA-JKT, au Nyanza au Songoro au Wachina na makampuni mengine ya nje ya nchi. So wazawa walikua hawalalamiki kuhusu malipo sababu kandarasi zenyewe walikua hawazipati
Kumbe Nyanza hakuwa mzawa!
 
Kumbe Nyanza hakuwa mzawa!
Ndio maana nchi nzima inamjua kwa sababu alikua mzawa pekee kwenye game hasa kwenye zile lucrative works. Wakati mwingine hakuonekana kwenye tender processing lakini mwisho wa siku mnaona yeye ndio kawa awarded!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom