DOKEZO Kulikoni mbona Bohari ya Dawa (MSD) mmefunga Duka la Dawa - Mpanda? Tunaomba huduma irejeshwe

DOKEZO Kulikoni mbona Bohari ya Dawa (MSD) mmefunga Duka la Dawa - Mpanda? Tunaomba huduma irejeshwe

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Joined
Sep 23, 2024
Posts
64
Reaction score
43
WhatsApp Image 2025-02-28 at 12.27.03_1f58ef63.jpg
Duka la Dawa la MSD Mpanda Mkoa wa Katavi linalomilikiwa na Bohari ya Dawa (MSD) sasa ni zaidi ya wiki moja limefungwa bila taarifa yoyote kwa Wananchi jambo ambalo imekuwa kero ambayo inasababisha kukosekana kwa dawa ambazo Wananchi tunalazimika kununua kwa bei nafuu.

Kukosekana au kufungwa kwa Duka hiilo lililopo ndani ya Hospitali ya Manispaa ya Mpanda katika makao makuu ya Mkoa ni jambo ambalo halipendezi na limetuacha katika maswali mengi.

Baada ya duka hilo kuwakuwa linafanya kazi, sasa Wagonjwa na Wananchi wengi wenye uhitaji tunalazimika kwenda kwenye maduka ya Watu Binafsi yaliyopo nje ya Hospitali kwenda kununua huko.
WhatsApp Image 2025-02-28 at 12.24.01_1ff576bc.jpg

WhatsApp Image 2025-02-28 at 12.33.55_6b490d26.jpg
Kama tunavyofahamu bei mara zote za maduka binafsi ya dawa za binadamu huuzwa kwa bei ya juu jambo ambalo linasababisha wengi wetu wenye uhitaji kushindwa kumudu gharama za kununulia dawa na hivyo afya zetu kuwa hatarini.

Natoa wito kwa Serikali hasa kwa mamlaka husika na huduma hiyo, warejeshe kwa Duka la MSD kwani ni tegemeo kwetu na msaada mkubwa hususani kwa Wananchi ambao hushindwa kumudu gharama za bei za maduka binafsi ya dawa.
 
Back
Top Bottom