Kulikoni mitandao ya Twitter na YouTube kutokuwa hewani?

Kulikoni mitandao ya Twitter na YouTube kutokuwa hewani?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kuelekea saa kumi na mbili leo, mitandao ya Twitter na YouTube imekumbwa na kwikwi.

Haya mambo ya kuchaguliana kipi tusikilize au kipi tusione hali tumenunua bando na kulipia tozo zenu zote yanatoka wapi?

Ama kwa hakika tunastahili maelezo kwa kuingilia starehe zetu.
 
1640966865697.png
 
Hao ni TCR CCM ambao hawapendi Tundu Lissu aongee na watanzania
Kwani yule mtaalam wa kuifunga si alidedi akifanya mazoezi afu maiti yake ikagoma kupelekwa kwao kuzikwa? Au wameshaajiri mwingine?
 
Kwani yule mtaalam wa kuifunga si alidedi akifanya mazoezi afu maiti yake ikagoma kupelekwa kwao kuzikwa? Au wameshaajiri mwingine?

Yaonesha kuna mrithi kachukua nafasi
 
Bora kabisa ili tusisikie ushoga
Hivi una akili
Hiyo mitandao inafungwa milele?
Hotuba ipo on
Sekunde ambayo utafungua mitandao watu wataipata hapo hapo hii siyo akili kabisa
Hivi kwa umri mlio nao mmeshindwa kujua kuwa jambo unapolikataza au kuzuia ndiyo linaleta shauku zaidi na watu ambao hawana interest na mambo ya siasa lazima watake kujua kwanini mitandao ilifungwa alikuwa anaongea nini

Huu ujumbe utaenda mbali zaidi ya ambayo ungefika kwa hii akili ndogo

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Nchi iko shimoni kulekule mlioko nyumbani poleni sana mnapswa kuamka

Mjue kipi ni haki kipi ni hisani , kupata habari ni haki ya kila mtanzania na asipangiwe habari ipi ya kuona au kusikia.
 
Kuna siku Mange aliitingisha serikali Hadi jeshilikaingizwa kwenye siasa.
Lissu naye anawatingisha. Wahenga walisema " Ukiona serikali imepiga marufuku kitabu Fulani, kitafute hicho kitabu ukisome"
Vivyo hivyo turudie ule utaratibu wetu wa VPN tumsikilize Lissu.
Bila shaka anajambo jema.
Kumbuka mtu anakohoa akiwa ulaya watu huku hawapati usingizi.
VIPINGO is the way to go
 
Si walisikia yule bwana wa Upande ule aliyeko kulee leo ataawahutibia wananchi wa Nanilia saa12 jion[emoji23][emoji23], sasa hawa wenye nchi wakaamua kumpangia na bimkubwa wao ahutubie leo leo na kufunga kiki zote za yulee bwana wa sa12 jioni[emoji23][emoji23].

Na huo ndio wao wa c+c+m season6 wanaita uhuru wa kuzungumza na uhuru wa vyombo vya habari tokea kwa mwanakuupiga mwingi from zenji-bar [emoji23][emoji23]
20211230_145844.jpg
 
Back
Top Bottom