Kulikoni Wamachinga walipie vitambulisho mara mbili?

Kulikoni Wamachinga walipie vitambulisho mara mbili?

Sasa mnataka mlipe 20000 kwa mwaka na pesa iende serikali kuu na machinga wapo manisipaa wasilipie manisipaa chochote? Huo usafi na wasimamizi wa mazingira Nani awalipe? Nani awasafishie vyoo? Tuweni na upendo jamani Sasa unataka sisi wenye maduka tughalimike wenyewe na nyinyi mpange mbele ya maduka yetu? Hiyo siyo sawa kabisa Kila mtu anashida jamani.
 
Siku zote nasema kuna watu washashindwa kutekeleza majukumu yao na kulazimisha kila mtu ajiajiri sio kwa lengo la kuinua uchumi wenu ila ni kwa sababu watapata mapato zaidi katika kodi na ushuru ili waendeleze anasa zao.
 
Sasa tatizo ni nini? Walipishwe hata mara nne. Vitambulisho ni muhimu.
 
Habari za majukumu wakuu.

Nilikuwa nangalia Azam TV asubuhi hii. Mtangazaji alikwenda stand ya Segerea kuwahoji watumishi wa stand ile.

Miongoni Mwao ni mfanyabiashara mdogo. Kwa mujibu wa mfanyabiashara yule ni kwamba wao walishalipia VITAMBULISHO VYA WAMACHINGA tsh 20000 kwa mwaka.

Hata hivyo cha kushangaza ni kwamba manispaa unaendelea kuwatoza KODI / USHURU kila uchao. Wakiuliza kulikoni wanaambiwa vitambulisho vya Wamachinga pesa yake ilienda serikali kuu na kwamba haihusiani na manispaa.

Unajiuliza maswali.

Je, mbona raisi wa wanyonge alisema hakuna kuwabughudhi Wamachinga baada ya kulipa ile 20000/ na tena akasema vitambulisho vitatumika hata kwa matibabu?

Tofauti kati ya kodi za manispaa na serikali kuu ni nini na kwanini mtu mmoja tena nyongeza kama anavyoitwa alipe kodi mara mbili?

Uko wapi ule msimamo kwamba Wamachinga akilipa kodi na kupata vitambulisho mpaka mwakani?

Tulidanganywa kwenye kampeni? Kwanini?

Chanzo: Azam TV morning trumpet
Wewe kinakuuma nini? Wahusika wanaona fahari kuichangia serikali yao kwa maendeleo yao, waache.
 
Wewe kinakuuma nini? Wahusika wanaona fahari kuichangia serikali yao kwa maendeleo yao, waache.
Wakalazimishwa. Acha mambo ya taarabu yani mtu aone fahari kuchangia af alallamike? Unatokea Mkoa gani wewe
 
Wakalazimishwa. Acha mambo ya taarabu yani mtu aone fahari kuchangia af alallamike? Unatokea Mkoa gani wewe
Ni watanzania wangapi wakitetewa huwaruka wanaowatetea, mbona ni wengi tu! Wanzfunzi wa vyuo walitetewa kuhusu marejesho ya mikopo, cha ajabu wakakanusha kuwa kuna tatizo, haohao wakaanza tena kulalamika.
 
Kwa kuangalia ukweli na jinsi manispaa zinavyojiendesha hivi vitambulisho vimewaumiza sana manispaa zote nchini.

kwa siku mfano hapo Segerea ushuru wa soko,mama ntilie nk ulikuwa ni kama laki 3 hivi.so kwa mwezi ni 300000x30 ni milion 9.hapo ni stand tu.b Bdo sehem zingine.

vitambulisho vya machinga kwa siku 360 ni tzs 20000. na hii hela inaenda ofisi ya rais. je manispaa inafaidika na nini kwa uwepo wa wa fanya biashara wadogo kwenye maeneo yake ambapo kila baada ya saa 24 manispaa zinatakiwa kuondoa uchafu uliozalishwa na hava wafanya biashara? Kuhakikisha ulinzi(mgambo) wapo wa kutosha nk.

Serikali kwa hili inatakiwa ijitafakari na kuja na suluhisho la kudumu. Pale Kariakooo zaidi ya million tano zinapotea kila siku kuingia kwenye mapato ya wilaya ya ilala,lakini itokee siku Kariakoo apajasafishwa, taka zake zitajaza malori zaidi ya 50 nani analipia huu usafi na kwa hela toka mfuko upi?

Kwa sasa viongozi wengi wana fanya kazi na kutimiza majukumu yao katika mazingira magumu na yenye bajeti kiduchu au zero kabisa.
Kulikuwa kuna haja gani ya kuweka wizara ya TAMISEMI chini ya OFISI YA RAISI????
 
Lipeni kodi tena ikiwezekana mlipe hata mara 3

Ova
 
Habari za majukumu wakuu.

Nilikuwa nangalia Azam TV asubuhi hii. Mtangazaji alikwenda stand ya Segerea kuwahoji watumishi wa stand ile.

Miongoni Mwao ni mfanyabiashara mdogo. Kwa mujibu wa mfanyabiashara yule ni kwamba wao walishalipia VITAMBULISHO VYA WAMACHINGA tsh 20000 kwa mwaka.

Hata hivyo cha kushangaza ni kwamba manispaa unaendelea kuwatoza KODI / USHURU kila uchao. Wakiuliza kulikoni wanaambiwa vitambulisho vya Wamachinga pesa yake ilienda serikali kuu na kwamba haihusiani na manispaa.

Unajiuliza maswali.

Je, mbona raisi wa wanyonge alisema hakuna kuwabughudhi Wamachinga baada ya kulipa ile 20000/ na tena akasema vitambulisho vitatumika hata kwa matibabu?

Tofauti kati ya kodi za manispaa na serikali kuu ni nini na kwanini mtu mmoja tena nyongeza kama anavyoitwa alipe kodi mara mbili?

Uko wapi ule msimamo kwamba Wamachinga akilipa kodi na kupata vitambulisho mpaka mwakani?

Tulidanganywa kwenye kampeni? Kwanini?

Chanzo: Azam TV morning trumpet
[emoji870]tenaaaa
 
Back
Top Bottom