Kulikoni ya wanawake na mavazi haya? Inasikitisha mnapoteza asili yenu

Tatizo la watu humu ndani saa nyingine wanaweza kudai madai yasiyo na mshiko kabisa, HIVI MTU NA AKILI ZAKE TIMAMU ANAMUULIAZA MTOA MADA KAONA WAPI, KAJUAJE, ILI HALI NA YEYE NI SHAHIDI WA HAYA MAMBO, NI UKWELI USIO NA WASI WALA SHAKA, WANAWAKE (WAKINA MAMA, DADA, SHANGAZI, BIBI) MAVAZI YANAYOVALIWA SIKU HIZI NI KIKWAZO KIKUBWA NA INAWASHUSHIA SANA HESHMA YENU, SIKU HIZI KUONA MAZIWA YA MWANAMKE NA CHUPI, UPAJA, MFEREJI WA T@KO NA VYOTE VISIVYOPASWA KUONWA ADHARANI NI RAISI MNO, UKIENDA BAA, KWENYE DALADALA, KANISANI (BAADHI), KWENYE HARUSI, NA SIO SIRI HII INAWAFANYA WANAWAKE KUONEKANA NI WATU WA KAWAIDA TU NA HATA YALE MATAMANIO YANAKUWA HAKUNA NA KINAONEKANA NI KITU CHA KAWAIDA TU
 
Mkuu kuna watu wanapenda topics fulani fulani na kusifiana pasipo maana sasa inapokuja topic inayogusa tabia na inayoitaji kuumiza kichwa kuchangia basi wanaona umewatukana. Hili ni tatizo hapa kwa baadhi ya watu, mambo yako yanaonekana kabisa lakini watu wamezoea kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa
 


Kweli Kabisa!!!!!!, Wengi huvaa nguo utadhani ni za watoto, zimebana na kutoa kila mfano njeeee!!!!!
 
zimebana na kutoa kila mfano njeeee!!!!!
Haswaaa uku ndio kukaa uchi kwenyewe sasa lakini utasikia mwingine anauliza "umetest wangapi" kuthibitisha? Does it make sense? Hivi ni wangapi wametest ufisadi ndio waweze kuzungumza au kuulaani ufisadi?
 
Hawapendi kuambiwa ukweli wengine humu c ndio mavazi yao pia.
 
JOTO ni moja ya essentials ya breeding bacteria...

kule kwa bibi,kunatakiwa kuwe na air circulation atiii...

usivae chupi...

and if you have to,tafuta ya kitambaa chepesi!!
 
JOTO ni moja ya essentials ya breeding bacteria...

kule kwa bibi,kunatakiwa kuwe na air circulation atiii...

usivae chupi...

and if you have to,tafuta ya kitambaa chepesi!!
utawajua tu kwa comment zao......................
 
Ni kweli Mokoyo naona sasa mambo yanaenda yakibadilika kwa kasi ya ajabu..heshima kwa baadhi ya wanawake imepungua..sijui kama ndio imekuwa soko huria kujitangaza ...
Wakati mwingine hata sisi huwa tunasikia aibu pale tunapokutana na kina dada wenzetu wamevaa mavazi yasiyo na adabu mchana kweupe..unajihisi kama umevuliwa nguo..
Labda ndio mambo ya utandawazi yenyewe...
 
Wanawake siku hizi wanaacha maziwa nje, mistari ya makalio nje, mapaja nje, wengine hawavai chupi, sidiria, wala skin tite. Si ajabu sasa kuuona uchi wa mwanamke mkiwa ndani ya daladala, ofisini, barabarani wakitembea, sehemu za starehe n.k

Tujifunze kutokana na historia. mabadiliko ya mitindo ya mavazi ni "cultural evolution" na huwezi kuyazuia. Nakumbuka katikati ya miaka ya 80 nikiwa primari kuna mwanafunzi alifukuzwa shule kwa kuva kaptula iliyokuwa na marinda!. Marinda na pindo la chini la suruali ilionekana kuwa ni uhuni mkubwa na sana sana kule vijijini walikwa wanavaa wacheza sarakasi waliokuwa wanatoka mjini. Leo hali ikoje?

Siku ya kwanza mimi kumuona mwanamke amevaa suruali hadharani (1988) kule kijijini ilikuwa ni gumzo, watoto zaidi ya hamsini walitoroka paredi na kumfuata kwa nyuma yul dada aliyekuwa ametokea Nairobi na baada ya hapo alikatazwa na uongozi wa asirudie tena. Leo hali ikoje? Tukubali tu kuwa mavazi tunayoyaona sasa hivi ni mabadiliko ya kawaida ya kimitindo na naamini sisi tunaoyakemea leo, ndio tutakaowanunulia watoto wetu na wake zetu mavazi hayo hayo miaka kadhaa ijayo...
 



nakuunga mkono mdau!
 
Kama ni great thinker kweli, huwezi kumjibu mwezako namna hii Mkulu...
Mkuu nina uhakika hujasoma swali lake lilivyokuwa limekaa. Nway turudi kwenye mada imekaaje, sijaona mchango wako Mhe.
 
nakuunga mkono mdau!
Mhe. Mayenga, watanzania tunaogopa na kuchukia ukweli, tukiambiwa ukweli ndio tunaanza kusema tumetukanwa, tumedhalilishwa pasipo kujirekebisha au kujitetea kama ni uonevu kweli
 
Tukubali tu kuwa mavazi tunayoyaona sasa hivi ni mabadiliko ya kawaida ya kimitindo na naamini sisi tunaoyakemea leo, ndio tutakaowanunulia watoto wetu na wake zetu mavazi hayo hayo miaka kadhaa ijayo...
Una uhakika Mkuu Ramos na maneno yako hapo kwenye blue?
 
afadhali umeeleza charity, watu wanasahau kwamba hizi nguo tumeiga kwa wazungu na si jadi yetu!
jadi yetu ni kuembea na nguo sa magome ya miti na ngozi za wanyama.
ila je tukirudi huko unadhani kutakuwa na usalama wa nafsi tena?
 
Go akina mama Goooo tembeeni uchi tu huu ndio utamaduni wa mwafrika matiti wazi no kuvaa ch****pi unafunika tu na nguo kwa juu, huu utamaduni wa kuvaaa nguo tumedandia tu toka kwa waarabu na wazungu harafu tunasema wakina mama wanavunja maadili yetu maadili yetu yapi hayo? tunajivika maadili ya ukristo na uislam na kusema ni yetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…