Kulipa fadhila kunamkondesha

na hilo la ndoa ndo linalomuwazisha ile mbaya
 
Kwanini huyo dada hakumuambia toka mwanzo huyo kaka kuwa hana feeling nae ili huyo mkaka ahamue kusuka au kunyoa? Wadada wengine bwana! Misaada anataka kumbe moyoni ana yake! Anyway, mkataa pema pabaya panamuita!
zamani kidogo kaupendo kalikuwepo ila sasa doo hali mbaya hajisikii hata
 
awe muwazi tu kwamba kapata tawi jingine la kushika ndo maana anasema hana hisia

wanaume wengine ving'ang'anizi wewe.
Mambo ya hisia haya tuyaache tu.
 
Huyo jamaa mpya naye anampenda huyo binti kama yule wa zamani?? Mwambie huyo kama naye anapendwa si vibaya kumwambia mapema mfadhili wake namna anavyofeel. Lakini awe makini baadae asije kulia maana huenda huyo jamaa mpya anataka kumvua tu nguo...

hahahah anaweza nae akaishiwa hisia ...

haya naona anadharau dafu hajui kama embe ni tunda la msimu
 
Huko anakoenda anapendwa au yeye ndiye anaonyesha upendo zaidi ya mwenzake?? Huyo mwanaume huenda anataka kumtafuna tu na kumuacha!!

hatuwezi kujua katavi. Ila mdada awe makini, asije akaangukia pabovu Maana mapenzi ya mwanzo matamu mnataka mgandane kama luba.
 
hilo ni neno pia unajua feelings zikigoma bwana inakuwa shida
 
hatuwezi kujua katavi. Ila mdada awe makini, asije akaangukia pabovu Maana mapenzi ya mwanzo matamu mnataka mgandane kama luba.

Mimi wasiwasi wangu ni huyo jamaa mpya naye hisia kupotea hapo baadae............
 

mdada umeongea yote. Ahsante.
 
mdada umeongea yote. Ahsante.
Ndio kaongea vizuri sana. Lakini je, ana uhakika gani huko anakong'ang'ania hatatendwa?? Tuangalie pande zote mbili faida na hasara zake.
 
Kama huyo mwanaume ni king'ang'anizi mlipendea nini at first place???
ingekuwa inawezekana watu waanze mahusiano wakifika chuo ingekuwa vizuri zaidi. Imagine wengine wanasomesha mtu tangu form one ila akifika chuo anakuwa hamuhitaji jamaa.
Tatizo nini? Kwanini alaumiwe binti? swala la kupevuka zaidi kiakili na kujua aina ya mwanaume unayemuhitaji huwa ni sababu kuu hapa.
 
Tatizo la dada zetu ni tamaa, mkifika chuo mnazinguliwa na maisha ya town, uzur ni kwamba vibut huwa vianaanza semester ya mwisho ya mwaka wa tatu.
 
Ndio kaongea vizuri sana. Lakini je, ana uhakika gani huko anakong'ang'ania hatatendwa?? Tuangalie pande zote mbili faida na hasara zake.

ukianzisha mahusiano usijenge mawazo ya kutendwa. Ukiwazia hayo mambo utajikuta wewe ndio unaanza usaliti.
 
Ndio kaongea vizuri sana. Lakini je, ana uhakika gani huko anakong'ang'ania hatatendwa?? Tuangalie pande zote mbili faida na hasara zake.
Katavi tatizo la hawa viumbe huwa hawajui wanachotaka usishangae huyu demu akamwaga jamaa akiisha tendwa huko anarudi kwa jamaa kumuomba msamaha tena
 

Halaumiwi binti, ni kuwa watu wanatoa uzoefu wao kwa sababu hii sio ishu ya kwanza kutokea na watu wanatoa uzoefu wao ambao inaonekana mwisho wake mabinti ndio hubaki kulia...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…