Kumbe bajeti ya Tanzania inaweza kuwa Tsh. Trilioni 2 na chenji ikabaki? Inafikirisha!

Kumbe bajeti ya Tanzania inaweza kuwa Tsh. Trilioni 2 na chenji ikabaki? Inafikirisha!

Dong Jin

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2018
Posts
968
Reaction score
2,034
Mwanzoni mwa utawala wa mama Samia, kuna mkopo wa trilioni 1.3 wa masharti nafuu ambao ulikopwa kwa ajili ya kupambana na janga la korona.

Huu mkopo ulipata umaarufu zaidi baada ya aliyekuwa spika wa bunge mh. Job ndungai kuhoji kwanini mkopo huo umeombwa wakati tunaweza kutumia hela zetu za makusanyo ya ndani? Tokea hapo drama za huu mkopo zikaanza.

Kila wizara ilijinadi kupewa kiasi fulani kufanya maendeleo makubwa na mbalimbali katika nchi yetu. Wizara ya afya walipewa zaidi ya bilioni 400, wizara ya elimu bilioni 300+, hivohivo kwa wizara ya maji, wizara ya kilimo, wizara ya ujenzi, tamisemi, na kadhalika!

Sasa kama trilioni 1.3 imeweza kufanya mambo makubwa namna hiyo, je trilioni 2 haiwezi kututosha kwa bajeti ya nchi?

Bajeti ya mh Mwigulu Nchemba imezidi hii ya covid. Sasa ni kwanini miradi mingi inahusiswa na hela za uviko? Au tulidanganywa kiasi sahihi kilichokopwa?

Mapambio ya huu mkopo yamekuwa mengi sana kuliko uhalisia wake. Tungeomba yaendane na uhalisia maana tunadanganywa sana chini ya kivuli cha huu mkopo!

Nawasilisha
 
Bajeti ya nchi ina cover maeneo mengi zaidi hivyo lazima iwe nyingi zaidi ya pesa za huo mkopo, kama bajeti ikiwa ndogo sawa na pesa za huo mkopo basi kuna maeneo pesa hazitatosha.

Ndio maana kwenye bajeti yetu huwa kuna kitu wanaita "nakisi ya bajeti" hii maana yake ni pesa zinazopelekwa kwenye wizara husika zinakuwa hazitoshi mahitaji yaliyoombwa, hivyo wizara hupokea pesa pungufu.

Lakini kwa huo mkopo waliopewa, na kule walipo invest kwenye ujenzi wa madarasa na vituo vya afya naona ulitosha, 1.3 trilion ni pesa nyingi sana kwa kazi hizo mbili pekee, inawezekana kuna wajanja walijipigia.
 
Bajeti ya nchi ina cover maeneo mengi zaidi hivyo lazima iwe nyingi zaidi ya pesa za huo mkopo, kama bajeti ikiwa ndogo sawa na pesa za huo mkopo basi kuna maeneo pesa hazitatosha...
Mishahara na matumizi ya kawaida vinakula sana bajeti
 
Bajeti ya nchi ina cover maeneo mengi zaidi hivyo lazima iwe nyingi zaidi ya pesa za huo mkopo, kama bajeti ikiwa ndogo sawa na pesa za huo mkopo basi kuna maeneo pesa hazitatosha.

Ndio maana kwenye bajeti yetu huwa kuna kitu wanaita "nakisi ya bajeti" hii maana yake ni pesa zinazopelekwa kwenye wizara husika zinakuwa hazitoshi mahitaji yaliyoombwa, hivyo wizara hupokea pesa pungufu.

Lakini kwa huo mkopo waliopewa, na kule walipo invest kwenye ujenzi wa madarasa na vituo vya afya naona ulitosha, 1.3 trilion ni pesa nyingi sana kwa kazi hizo mbili pekee, inawezekana kuna wajanja walijipigia.
Ni kweli lakini hili wimbi la kila wizara kutumia hela ya uviko kwa kila kinachojengwa hapa nchini unaliona lipo sawa? Trilioni 1.3 ni hela ya kiasi gani ambayo unaweza kutoa zaidi ya bilioni 300 kwa kila wizara na isiishe???

Sikatai kuwa bajeti ina cover mambo mengi lakini tusiaminishwe kuwa kila jambo hela ya uviko imehusika! Isingewezekana mkopo ndani ya mwaka mmoja wa mama samia kuwa madarakani uwe Trilioni 10+ lakini kila mradi tunaambiwa ni hela ya uviko...
 
Mishahara na matumizi ya kawaida vinakula sana bajeti
Kabisa mzee na hilo halijawekwa katika uwazi unaotakiwa ndo maana linachukua kiasi kikubwa cha bajeti... Amini nakwambia kuna hela nyingi inapigwa hapa bila hata kujulikana!
 
bajeti ina cover maeneo mengi mpaka madeni ya nyuma yapoo humoo
 
Mishahara na matumizi ya kawaida vinakula sana bajeti
Mapato yetu kama Nchi hayana tofauti na mapato ya familia nyingi za Watanzania wa kipato Cha chini kama mama ntilie au bodaboda.

Mapato ya mama ntilie Kwa mf, yanatosha kununua chakula na MATUMIZI ya siku pekee, kujenga ni Hadi akope au acheze vikoba.

Mapato ya Serikali ya ndani kupitia Kodi yanatosha kulipa mishahara na MATUMIZI ya serikali yasiyo ya kimaendeleo pekee.

Ukiona shughuli ya maendeleo au uwekezaji jua ni MKOPO au Msaada wa masharti magumu mf kuuza raslimali.

Swali: Ni jitihada Gani zifanyike kukuza Uchumi wa ndani tuweze kujitegemea kibajeti ikibidi tuzikopeshe Nchi zingine?

Jibu:

1.Katiba mpya. Tujadili aina ya Uchumi tuutakao na Kutumia raslimali vizuri.

2.Viongozi waache roho mbaya. Mikopo inayokopwa mostly inapelekwa ktk miradi ya wakubwa bt kwenye MALIPO wanalipa maskini.

3. ELIMU ya shule za umma iwe na ubora zaidi ya ELIMU itolewayo ktk shule binafsi.

4. Mawaziri wasitokane na wabunge. Utaratibu huu mbovu umepelekea watu wa uwezo wa chini kupenya Hadi UWAZIRI, mf mwigu na marope.
 
Back
Top Bottom