Kumbe kitunguu saumu kinalipa hivi

Kumbe kitunguu saumu kinalipa hivi

Jamani watanzania ifike mahali tuache maneno mengi tufanye kazi....mimi kwasasa niko shambani niko nalima japo kwasasa nimejikita kwenye kilimo cha hoho ila mwaka huu nalima tangawizi pia....rai yangu kwa yeyote anayetaka kujifunza aje hapa IGAWA - MBEYA atajifunza mengi sana kuhusu kilimo cha umwagiliaji....hapa watu wanalima sana vitunguu(maji)...japo sijaona mkulima mzuri wa vitunguu swaumu....lakini pia hapa maji yapo mwaka mzima.

karibuni sana tulime kisasa....kilimo kinalipa sana...atakaye taka kuja igawa kujifunza nitampa ushirikiano wa hali ya juu with maximum care and security
Kaka interest yangu ni tangawizi. Nipo Makambako ipo siku nitakuja hapo Igawa. Napenda kilimo sana. Mashamba yangu yapo Mambi Igurusi
 
[h=3]KILIMO CHA VITUNGUU TWAUMU - garlic[/h]




UDONGO
Vitunguu twaumu vinahimili aina nyingi za udongo, ila vinastawi zaidi katika udongo usiotuamisha maji kabisa na wenye mbolea asili, kama mbolea si ya kutosha kwenye udongo, tumia samadi iliyokwisha oza vizuri usitoe samadi bandani na kuipeleka shambani moja kwa moja kwenye shamba la vitunguu thwaumu, labda kama utaliacha shamba bila kulimwa kwa zaidi ya miezi 6, pia unaweza kutumia mbolea za viwandani kama ammonium nitrate, ammonium sulphate, urea n.k wakati wa kupanda na kila baada ya wiki 4 – 6 mara mbili zaidi

UPANDAJI
Kipindi kizuri kwa upandaji ni kipindi ambacho hakuna joto hasa miezi ya May mpaka August kwa Tanzania, Unachukua kitunguu twaumu na kutenganisha vitunguu kimoja kimoja (bulbs) na kuchagua vile vikubwa maana hivi ndivyo vitakavyo kupa mazao mengi na bora, nafasi kati ya kitunguu na kitunguu ni sentimeta 10 na kati ya mistari ni sentimeta 30. Baada ya kupanda pandishia udongo na uukandamize kuhakikisha kwamba kimekaa vizuri na hakiwezi kuathiriwa na mvua au maji wakati wa kumwagilia ili kisikae upande au kungolewa kabisa. Uotaji mzuri hutegemea pia namna vitunguu thwaumu vilivyo hifadhiwa kabla ya kupandwa, kama vilihifadhiwa sehemu zenye joto na hewa finyu uotaji wake utakuwa duni na dhaifu.


UMWAGILIAJI

Kama kuna upungufu wa mvua au ni kipindi cha kiangazi basi ni vizuri ukamwagilia shamba lako, wakati mzuri wa kumwagilia vitunguu twaumu ni asubuhi na sio jioni au mchana, hii inasaidia vitunguu twaumu kujijengea uwezo wa kupambana na magonjwa, baada ya mizi miwili unaweza kupunguza umwagiliajai huku ukiangalia kwa kuchimba kidogo kama vitunguu twaumu vimezaliana vya kutosha na kuanza kukomaa, ukiona vimekomaa acha kabisa kumwagilia ili visioze

UANGALIZI
Aina nyingi za vitunguu twaumu vitakuwa kama vinatoa mbegu kwenye mmea (angalia picha chini), ingawa kuna nadharia nyingi lakini inashauriwa kukata hizi mbegu chini kabisa kwa kisu kikali na kisafi, usikate mapema mara baada ya kutokeza bali subiri mpaka mmea unapoanza kama kujikunja ndipo ukate, kwa wale wanaoacha mbegu hizi ukiamua kuzipanda kwa msimu wa kwanza zitazaa kitunguu kimoja tu cha duara lakini chenyewe ukikipanda tena kwenye mzunguko wa pili kitazaa vitunguu vingi kama kawaida



Ungoleaji wa magugu na majani ni muhimu muda wote ili kuondoa kugombea rutuba, hewa na maji shambani, kwa wenye mashamba makubwa wanaweza kutumia dawa za kemikali kama ROUNDUP na nyinginezo ili kudhibiti magugu, ingawa mimi sishauri hivyo.

MAGONJWA
Magonjwa kama botrytis (kuoza shingo) blue mould na fusarium (kuoza kwa vitunguu) husababisha hasara kubwa kama hayatadhibitiwa kwa kutumia viuatilifu mara unapoona dalili, pia magonjwa kama white rot huchukua zaidi ya miaka 20 kuondoka kama yatavamia shamba lako, inashauriwa kufanya mabadiliko ya zao kila baada ya miaka mitano kwa kupanda mazao mengine yasiyo jamii moja kama vitunguu maji, unaweza kupanda maharage, mahindi, karoti na kabichi katika mzunguko huo. Pia magonjwa kama kutu ya majani husababisha na unyevu mwingi hasa kama mimea itakuwa kwenye udongo unaotuamisha maji au mimea kumwagiliwa jioni au usiku, kumbuka kumwagilia asubuhi tu Ili kudhibiti ugonjwa huu wa kutu mimea ingolewe na ichomwe au utumie viuatilifu vya kuulia fangasi wa mimea.
Pl hujaongelea gharama zake mku
Plus estimation za mavuno kwa ekari na bei yake
 
Hz gharama zake zikoje?
tuseme bei ya 300,000 hadi 500,000 kwa gunia na kupanda gunia 16 hadi 28 kwa ekari unaapata gharama za mbegu 4.8m hadi 14m. madawa, vibarua na mbolea sina uzoefu washambani. ngoja tuwasubiri watu wa babati.
 
Kuna watu hapa jukwaani wao ni kila kukicha ni kuchukua data tuuuu wajawahi kabisa kuingia kwenye field zaidi ya kuuliza ABCD za fursa mbalimbali zinazopambanuliwa hapa jukwaani. Mmoja wao ni huyu bwana Bulldog ni kero tupu aseee mpaka kero, ebu fanya utupie material things hapa jukwaani.... otherwise unaboa mkuu!!
Mkuu kisima nilikua nakuheshim sana but hii comment yako sio ya kiungwana kabisa
Hv ni lazima ulete data humu?we toa msaada the rest ni mtu mwenyewe anajua
Kwanza unajuaje kama mtu hajalima?kwani ni dhambi kuulizia data zingine zaidi ya kilimo unachofanya?huwez kua na plan za baadae?ts a shame mkuu umefanya ujinga wa kiwango cha lami mkuu jifunze kuheshime mawazo hayo hayo unayoona ya kijinga sababu hatuna plan sawa
Hatuwez wote tukashinda kwenye majukwaa ya mapenz au siasa so kwa kila mada inayopostowa humu lazima tuulize maswali na kupata uelewa wa kutosha kama unaona hupend tunavyopata elimu basi acha kuto msaada hulazimishwi
 
Jamani watanzania ifike mahali tuache maneno mengi tufanye kazi....mimi kwasasa niko shambani niko nalima japo kwasasa nimejikita kwenye kilimo cha hoho ila mwaka huu nalima tangawizi pia....rai yangu kwa yeyote anayetaka kujifunza aje hapa IGAWA - MBEYA atajifunza mengi sana kuhusu kilimo cha umwagiliaji....hapa watu wanalima sana vitunguu(maji)...japo sijaona mkulima mzuri wa vitunguu swaumu....lakini pia hapa maji yapo mwaka mzima.

karibuni sana tulime kisasa....kilimo kinalipa sana...atakaye taka kuja igawa kujifunza nitampa ushirikiano wa hali ya juu with maximum care and security
Huku igawa wanakodisha mashamba?na kama wanakodisha kwa gharama gani?
 
  • Thanks
Reactions: 365
Nilishawahi kulima vitunguu hapo Igawa nikala mweleka,nikawa bado kwenye maruweruwe nikanyanyuka hku napepesuka nikalima tena nyanya nikapiga mzinga wa haja hata kumi haikurudi
What happened mkuu
 
What happened mkuu
Mbegu za vitunguu zilikuwa fake sana. Kwa nyanya msimu niliilima bwanae zilimwagika mtaani kama mchanga sijui zilitokea wapi unatafuta wateja wala hupati hata mmoja...watu walitelekeza nyanya mashambani sana pamoja na mimi after two week zikaadimika ndo ikawa imekula kwetu tuliotelekeza.

Nikabadilisha,nikalima mahindi nikavuna msimu wa mwaka juzi kama sikosei daaah,ikawa balaa tena mahindi yalikuwa mengi sana msimu ule bei iliporomoka vibaya mno,yaani kwenye kilimo bado sijawa na bahati nayo sana ila kuna moja hiyo ndo nilipiga mzinga mtakatifu vibaya with no any return.
 
Mbegu za vitunguu zilikuwa fake sana. Kwa nyanya msimu niliilima bwanae zilimwagika mtaani kama mchanga sijui zilitokea wapi unatafuta wateja wala hupati hata mmoja...watu walitelekeza nyanya mashambani sana pamoja na mimi after two week zikaadimika ndo ikawa imekula kwetu tuliotelekeza.

Nikabadilisha,nikalima mahindi nikavuna msimu wa mwaka juzi kama sikosei daaah,ikawa balaa tena mahindi yalikuwa mengi sana msimu ule bei iliporomoka vibaya mno,yaani kwenye kilimo bado sijawa na bahati nayo sana ila kuna moja hiyo ndo nilipiga mzinga mtakatifu vibaya with no any return.
Hammer nadhani hapo ulipata hasara ya pesa ila ulipata faida kubwa ya uzoefu, mimi binafsi nimepata hasara mara mbili kubwa za kipesa ila nikapa faida kubwa za uzoefu, kwa mfano ukilima nyanya usilime shamba zima kwa mpigo kama ni heka tano basi kila heka ipishane na nyingine kwa muda mwezi mzima wakati wa kupanda, ili utapoanza kuvuna heka moja ikikutana na bei mbaya sokoni basi heka inayofuata lazima ikutane na bei nzuri sokoni sababu bei mbaya ya nyanya hua haidumu za zaidi ya wiki tatu.
 
Mbegu za vitunguu zilikuwa fake sana. Kwa nyanya msimu niliilima bwanae zilimwagika mtaani kama mchanga sijui zilitokea wapi unatafuta wateja wala hupati hata mmoja...watu walitelekeza nyanya mashambani sana pamoja na mimi after two week zikaadimika ndo ikawa imekula kwetu tuliotelekeza.

Nikabadilisha,nikalima mahindi nikavuna msimu wa mwaka juzi kama sikosei daaah,ikawa balaa tena mahindi yalikuwa mengi sana msimu ule bei iliporomoka vibaya mno,yaani kwenye kilimo bado sijawa na bahati nayo sana ila kuna moja hiyo ndo nilipiga mzinga mtakatifu vibaya with no any return.
Mkuu naomba usinichoke kwa maswali yangu
Wanna knw ulikosea wp tofauti na unachokisema
Nyanya ulilima miez gani?
 
Back
Top Bottom