Kumbe lile daraja pale Kindondoni linaitwa Selander Bridge?

Limeandikwa kwenye kibao cha shaba SELANDER BRIDGE,uwe unadoma soma,mambo ya kusikia sikia ndiyo yaliyozaa maneno kama"KOLOBOI"badala ya "Call boy"ikimlenga jamaa wa zamu anaekaa na taa usiku kwenye makutano ya barabara na reli,ambapo hata kwa mchana anakuwa na kibendera ambapo hakuna taa rasmi za kuashiria.
 
Daraja lilijengwa kwa mara ya kwanza na wakoloni, likaitwa Slander Bridge.

Nyerere alipohamia Msasani, likawa ni dogo na lina kero nyingi ndipo akaamua kulijenga upya na kulipanua bila kubadili jina. Kuna majina mengi sana yaliyoachwa na wakoloni bado tumeendelea kuyatumia kwa muda mrefu sana; mfano Ocean Road ilibadilishwa majuzi tu kuwa Barack Obama, na Oyster Bay bado mpaka leo tunaiita hivyo hatujaibadili.

Nyerere hakuomba kitu ila alishtukizwa zawadi ya kujengewa kitu, yeye akaamua kujengewa daraja. Detail za ujenzi zilifuatia baadaye. tena afadhali yeye aliomba daraja tunalotumia wengi, miaka ya hivi karibuni kuna watu wangeomba wajengewe ghorofa Tokyo hapo hapo.
 
Niongezee hapo, mkabala na Kanisa la St. Peters hapo kuna Shule ya Mbuyuni. Wakati wanajenga pale Selander, Vifusi vya kokoto vilitokea hapo bondeni pembezoni mwa Shule ambayo ilibarikiwa kuwa na Walimu wa watu al-maarufu Tanzania mmoja wapo akiwa Mama Janet M.
Kwaavile ulikuwa uwanja wa shule, baada ya kumaliza kutifutifua hapo, walilazimika kama sio kulazimishwa kuusawazisha na hata kuongezea udongo pamoja na mchanga.
Hapo uwanjani kuna mpaka nondo za zamani za daraja lililofumuliwa
Uwanja ule ukaitwa Uwanja wa Kajima na hapo ikatokea timu moja inaitwa Kajima Sports kama sikosei.

Karibu Dism
 
Wabongo wanaita Ostabei
Oyster bay
Oyster= Chaza
Bay= eneo la bahari lililoingia nchi kavu
 
Wengi wenu mnazungumzia NEW SELANDER BRIGE ambalo limejengwa mwaka 1982 kwa msaada wa Japan. Lakini pale pembeni pana daraja la mwanzo OLD SELANDER BRIGE ambalo lilijengwa mwaka 1929 na wakoloni wa Kiingereza na kupewa jina la huyo afisa JOHN SELANDER aliyefariki mwaka 1927.
Wazo la ujenzi wa daraja jil mwaka 1929 ni baada waingereza kuanza kutawala Tanganyika, hawakutaka kuishi maeneo ya upanga ambayo wajerumani waliishi hivyo wakatafuta eneo la Oysterbay na kuanzisha makazi. changamoto ikawa kuvuka huo mkondo wa bahari kwenda Oysterbay, ndipo wazo la kujenga daraja hilo likaanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…