king's lawyer
JF-Expert Member
- May 4, 2015
- 408
- 358
Daraja lilijengwa kwa mara ya kwanza na wakoloni, likaitwa Slander Bridge.Story nzuri na inafurahisha ila matukio hayapo clear.
Je, huyo Selander ambaye kwa jina imaonyesha alikuwa na asili ya Uingereza alikuwa mfanyakazi enzi za mkoloni, ina maana alikuwa anafanya kazi kwenye utawala wa Nyerere miaka ya '70? Kama ni hivyo, kulikuwa na haja gani kusema 'alikuwa ni Mkurugenzi enzi za mkoloni' wakati tunaongelea miaka 10 baada ya uhuru?
Na kwa nini Nyerere aliona busara kulipa daraja jina la huyo Selander wakati ufundi na pesa za ujenzi zilitoka kwa Mfalme wa Japan? Mwenye ufahamu wa hayo aendelee kutiririka.
Na kusema Nyerere alivyokuwa na uwezo wa kujielezea alishindwa kujielezea kwa ufasaha Mfalme hadi ikadhaniwa anaongelea daraja la Zanzibar nalo ni ngumu kuamini. Hizi taarifa alikuja kuzitoa nani?
Niongezee hapo, mkabala na Kanisa la St. Peters hapo kuna Shule ya Mbuyuni. Wakati wanajenga pale Selander, Vifusi vya kokoto vilitokea hapo bondeni pembezoni mwa Shule ambayo ilibarikiwa kuwa na Walimu wa watu al-maarufu Tanzania mmoja wapo akiwa Mama Janet M.John Einar Selander alikuwa mkurugenzi wa idara iliyokuwa inajulikanakaa PWD, yaani Public Works Department, wakati wa utawala wa kikoloni. Alisimamia ujenzi wa lile daraja kuelekea Oysterbay ambayo wakati huo ilikuwa inaitwa uzunguni. daraja lile lilikuwa dogo ambalo wakati wa mvua lilikuwa linapitika kwa shida shida. Kwenye miaka ya sabini wakati Nyerere akiwa Japan, alipewa zawadi ya ujenzi na mfalme wa Japan, yeye akaomba ajengewe "daraja" kama yaliyoko japan. Wakati ule mfalme alidhani kuwa Nyerere anaomba ujenzi wa Daraja kuunganisha Dar na Zanzibar akama ambavyo wajapani wameunganisha visiwa vyao kwa madaraja, hivyo akaiagiza serikali ya Japan ilete mkandarasi wa hali ya juu kufanya kazi hiyo kulinda jina na heshima ya mfalme. Serikali ya Japan ikaleta kampuni ya Kajima ambayo ilikuwa kampuni kubwa sana ya ujenzi kuliko zote wakati huo na ilikuwa imeshiriki ujenzi wa madaraja mengi ya kuunganisha visiwa vya Japan. Wahandishi wa Kajima walipofika wakaambiwa ni ujenzi wa Selander Bridge vizuri kati ya Msasani alikokuwa akiishi Nyerere na Ikulu, ni jambo ambalo lilikuwa kama kichekesho kwao. Ila waliona kuwa miundo mbinu Tanzania ilikuwa ni mibovu sana, wakati Japan ikiwa inapanua masoko ya uuzaji wa Magari kwa hiyo wakadhani kuna uwezekano wa kupata kandarasi nyingi za ujenzi huko mbeleni. Wakaweka ofisi yao Tanzania na waliendelea kuwapo kwa muda mrefu kidogo ingawa baadaye miradi ikawa inafanywa na Konoike.
Wabongo wanaita OstabeiKwa miaka mingi, nilikuwa naliita hili daraja la karibu na Kinondoni na Upanga kama SURRENDER BRIDGE na nilidhani pia linaandikwa hivyo maana siku zote nasikia linatamkwa hivyo.
Nimepita juzi nikashangaa mabango mawili tofauti yaliyopo kituo cha polisi pale yameandikwa SELANDER POLICE STATION.
Ningependa kujua Selander ina maana gani? Ni jina la mtu au na mbona sijawahi kusikia mtu akilitamka hivyo?