GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
Angeyasema kiongozi wa dini, angeweza kutuhumiwa kuwa anachanganya dini na Siasa!
Wangeongea CHADEMA, wangeambiwa ni tabia yao kupinga!
Lakini sasa aliyeongea ni kada Luhanga Mpina? Nani atakayemjibu?
Kwa mujibu wa huyo mzalendo, kilichokuwa kikichangia tatizo la umeme kukatika mara kwa mara ni matatizo ya kutengenezwa.
Kulikuwa na ukarabati usioisha, na wakati mwingine, huo ukarabati ulihusisha mpaka maeneo yasiyohitaji ukarabati wowote.
Kama hayo ni kweli, ilikuwaje Rais hakuyabaini? Hakuona kuwa hilo tatizo lilipamba moto baada ya kumwondoa Kalemani kwenye Wizara inayoshughulikia umeme?
Wangeongea CHADEMA, wangeambiwa ni tabia yao kupinga!
Lakini sasa aliyeongea ni kada Luhanga Mpina? Nani atakayemjibu?
Kwa mujibu wa huyo mzalendo, kilichokuwa kikichangia tatizo la umeme kukatika mara kwa mara ni matatizo ya kutengenezwa.
Kulikuwa na ukarabati usioisha, na wakati mwingine, huo ukarabati ulihusisha mpaka maeneo yasiyohitaji ukarabati wowote.
Kama hayo ni kweli, ilikuwaje Rais hakuyabaini? Hakuona kuwa hilo tatizo lilipamba moto baada ya kumwondoa Kalemani kwenye Wizara inayoshughulikia umeme?