Kumbe umeme mikoani bado kizungumkuti?

Kumbe umeme mikoani bado kizungumkuti?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Niko ukweni kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa mwaka.

Hali ni mbaya. Umeme hakuna masaa 12 kwa siku. Yaani ni mwendo wa 0700 - 1900 kila siku.

Siku niliyofika nilidhani ilikuwa kutuwezesha nchi nzima japo kumwona Messi akichukua kombe baadaye usiku.

Kumbe hola!

Kumbe haya ndiyo maisha ya kanda ya ziwa wasikojua umuhimu wa kumweka Kipara kwenye vidole gumba kurudisha umeme kama tufanyavyo mjini?

Ninavyoandika hapa kama ada 0700 umeme umeshaliwa kichwa. Hii ni kama ilivyokuwa jana, juzi nk, tokea niingizane pande za huku.

Kulikoni wadau hali ikoje huko mliko nyie wenye kampuni lao wakiendelea kuchepusha maji Ruaha mkuu, kwa raha zao?

"Kwani nani atathubutu kuwagusa wajumbe wa bodi kihasara hasara? Kwani hajipendi yeye?" --in yoga's words.
 
Nchi hii sasa hivi ina mambo ya ajab cha ajab aliyeshika rungu akiambiwa anaupiga mwingi anafikri kauli hiyo inamjenga ! tatizo kubwa aliyepo kule juu hajazoea barabara anaona zina mtesa kazoea mawingu ! hajui shida za wananchi zilivyokuwa kubwa hivi sasa.
 
Niko ukweni kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa mwaka.

Hali ni mbaya. Umeme hakuna masaa 12 kwa siku. Yaani ni mwendo wa 0700 - 1900 kila siku...
Sisi tunajua tupo pamoja kumbe kuna wenzetu mnatuzunguka, mnaenda kula likizo ukweni, kweli wadau hatuna misimimamo.
 
Ni kweliiii

Hapa sahii haupo ‘Njiro- kurudi ni 1830+

Ni kelele za generators mpaka tuchanganyikiwe.
 
Sisi tunajua tupo pamoja kumbe kuna wenzetu mnatuzunguka, mnaenda kula likizo ukweni, kweli wadau hatuna misimimamo.

Kwani ninyi ni wadau wa wapi au wa nini mkuu?

Kama ni kwenye yale mambo yenu ya mbususu, ma single mother na ya namna hiyo, wengine sisi siyo wa huko!

Tafadhali jiridhishe kutambua kuwa hujachanganya madesa.

Hiiiiiiii bagosha!
 
Wanasiasa jana wamesema Bwawa lao ndio wanaanza kulijaza maji,

Kazi tunayo. Kumbe bila kelele hawa wangejimilikisha kila kitu. Ama kweli kazi ya kelele na iendelee. Hawa ndugu hawana dini.
 
Niko ukweni kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa mwaka.

Hali ni mbaya. Umeme hakuna masaa 12 kwa siku. Yaani ni mwendo wa 0700 - 1900 kila sik...

Hapa nilipo umeme umekatik atokea asubuhi
 
Sakina huku wamelala nao mbele. Ni mateso sana.
Umeme ni anasa. Acheni kuendekeza na kupenda anasa. Mababu zetu Mbona waliishi bila umeme na walikuwa na furaha tu na maisha yalienda?
 
Nchi hii sasa hivi ina mambo ya ajab cha ajab aliyeshika rungu akiambiwa anaupiga mwingi anafikri kauli hiyo inamjenga ! tatizo kubwa aliyepo kule juu hajazoea barabara anaona zina mtesa kazoea mawingu ! hajui shida za wananchi zilivyokuwa kubwa hivi sasa.

Kama ilivyotabiriwa 1900 umeme umerejea. Tumsubirie Kipara kesho 0700.
 
Huku mbeya haya maisha walishazoea unataka kunyoa nywele sa moja kusaga sa moja stationery sa moja kuchomelea sa moja ikifika kumi na mbili asubuhi umeme unakatwa
 
Huku mbeya haya maisha walishazoea unataka kunyoa nywele sa moja kusaga sa moja stationery sa moja kuchomelea sa moja ikifika kumi na mbili asubuhi umeme unakatwa
Ujanja ujanja mwiiii..iiingiii.
 
Back
Top Bottom