Kumbe Wanaohusishwa na Tukio la Bomu Arusha ni Askari Polisi??

Kumbe Wanaohusishwa na Tukio la Bomu Arusha ni Askari Polisi??

sokoinei

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
1,832
Reaction score
566
Maofisa wa Ubalozi wa U.A.E Wanalalamikia polisi kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya Kimataifa vya habari na Wananchi wa Tanzania kupitia Waziri wa mambo ya ndani Dk Emmanuel Nchimbi kuwa raia wao wanahusika na tukio la Uhalifu lililotokea Arusha.

Kimsingi wametoa muda kwa Serikali ya Tanzania kuwaachia raia hao kwani nchi hiyo inaamini kuwa hawahusiki kwa namna yeyote na tukio la Arusha na kwamba kukamatwa kwao ni kinyume cha taratibu za sheria za Kimataifa.

Taarifa zinadai kuwa watuhumiwa wawili kati ya hao ni "ASKARI POLISI"wa nchi hiyo ya Falme za Kiarabu na Mwenzao mmoja ni Ofisa wa Ushuru wa Forodha wakati raia wa Saud anayeishi U.A.E ni mtaalamu wa maswala ya Moto.

Taarifa zinaonyesha kuwa vijana hao ambao wote ni watumishi wa Serikali waliwasili Jumatano iliyopita kwa likizo fupi ya kutembelea nchi za Afrika Mashariki na walitarajiwa kurejea U.A.E alhamisi wiki hii.

Taarifa zaidi zinabainisha kuwa baada ya kuwasili Tanzania na kutembelea jijini Dar es salaam kwa siku mbili vijana hao waliwasili Arusha Jumamosi wakitumia gari dogo la rafiki yao ambae ni Mtanzania mwenye asili ya kiarabu na kufikia hoteli ya Aquiline iliyopo jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi Jijini Arusha.

Usiku huo jumamosi taarifa zinaonyesha kuwa vijana hao walikwenda kustarehe katika Vilabu mbalimbali vya starehe wakihama kutoka Kilabu vitatu tofauti.ilipotimia saa 9 alfajiri walirejea ktk Hoteli waliyoifikia.

Asubuhi ya Jumapili ambayo kanisa ililipuliwa kwa Bomu vijana hao waluanza Maandalizi ya kwenda Nairobi nchini Kenya kumalizia ratiba yao ya Starehe ilioanzia Tanzania lakini kabla ya kuondoka ndipo walipo kamatwa.

TAARIFA ZAIDI: Soma gazeti la Raia mwema.

Soma After Arusha Bombing Is NOT Time for TZ to Adopt CCTV Culture?
 
Kwani Victor Ambroce ambaye ni mshakiwa Nam a moja ni raia wa wapi?

Leo tupo kwenye mazishi jamani punguzeni munkari
 
duuh hii sinema ya kuhuzunisha sana hata haileweki.
inasikitisha sana serikali inavyotangaza majina ya watu kama haya bila kuwa na ushahidi yanatuonyesha jinsi gani tusivyokuwa makini, yanaharibu sana image ya taifa letu...

ni lini serikali yetu itakuwa makini jamani....
 
Interejensia Pumbavu kabisa ya polisi haiwezi kusaidia kabisa kujua nani mhusika. Shenzi sana nyinyi
 
umewahi sikia katika utawala huu (MANAKE SIO UONGOZI HUU) KUNA TUKIO LOLOTE LILE LILILOWAHI KUMTIA HATIANI MTUHUMIWA HATA MMOJA. ILI UPATE KULINGANISHA NA UCHUNGUZI WANAOUFANYA NA SIFA WANAZO MWAGIWA POLISI WETU?
 
Kwa mara nyingine JK na Watanzania wote wanaingizwa chaka na watu wa Jeshi la polisi na wanaintelijensia.
 
Hakuna kitu hapa. wana-buy time watu wasahau wafukie kama yalivyofukia mengine. Haingii akilini tukio kama hili anapewa kuchunguza mtu ambaye hana weledi wa kutosha. Hivi ni kweli hakuna askari wenye weledi juu ya kazi hizi? Au ndio kuwabania na kushika kesi ili muonekana mnajua mwishoni kujiiti aibu?
 
Kwa mara nyingine JK na Watanzania wote wanaingizwa chaka na watu wa Jeshi la polisi na wanaintelijensia.
vyombo vyetu vya usalama hasa polisi wanasumbuliwa na tatizo la ilimu.
 
Hakuna kitu hapa. wana-buy time watu wasahau wafukie kama yalivyofukia mengine. Haingii akilini tukio kama hili anapewa kuchunguza mtu ambaye hana weledi wa kutosha. Hivi ni kweli hakuna askari wenye weledi juu ya kazi hizi? Au ndio kuwabania na kushika kesi ili muonekana mnajua mwishoni kujiiti aibu?
taasisi zetu za usalama kwa sasa zipo katika kipindi kigumu sana kuliko wakati mwingine wowote, wamezungukwa na pressure toka pande zote ...toka kwa serikali, wananchi nao mbali na kukosa imani kwa vyombo vyetu hivi wana taarifa nyingi na hivyo kutaka kujua kinachoendelea . Ni suala la muda tu kabla ya watu kuanza kuumbuana na kunyoosheana vidole kwa kushindwa kuwajibika kwa wakati .
 
Maofisa wa Ubalozi wa U.A.E Wanalalamikia polisi kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya Kimataifa vya habari na Wananchi wa Tanzania kupitia Waziri wa mambo ya ndani Dk Emmanuel Nchimbi kuwa raia wao wanahusika na tukio la Uhalifu lililotokea Arusha.

Kimsingi wametoa muda kwa Serikali ya Tanzania kuwaachia raia hao kwani nchi hiyo inaamini kuwa hawahusiki kwa namna yeyote na tukio la Arusha na kwamba kukamatwa kwao ni kinyume cha taratibu za sheria za Kimataifa.

Taarifa zinadai kuwa watuhumiwa wawili kati ya hao ni "ASKARI POLISI"wa nchi hiyo ya Falme za Kiarabu na Mwenzao mmoja ni Ofisa wa Ushuru wa Forodha wakati raia wa Saud anayeishi U.A.E ni mtaalamu wa maswala ya Moto.

Taarifa zinaonyesha kuwa vijana hao ambao wote ni watumishi wa Serikali waliwasili Jumatano iliyopita kwa likizo fupi ya kutembelea nchi za Afrika Mashariki na walitarajiwa kurejea U.A.E alhamisi wiki hii.

Taarifa zaidi zinabainisha kuwa baada ya kuwasili Tanzania na kutembelea jijini Dar es salaam kwa siku mbili vijana hao waliwasili Arusha Jumamosi wakitumia gari dogo la rafiki yao ambae ni Mtanzania mwenye asili ya kiarabu na kufikia hoteli ya Aquiline iliyopo jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi Jijini Arusha.

Usiku huo jumamosi taarifa zinaonyesha kuwa vijana hao walikwenda kustarehe katika Vilabu mbalimbali vya starehe wakihama kutoka Kilabu vitatu tofauti.ilipotimia saa 9 alfajiri walirejea ktk Hoteli waliyoifikia.

Asubuhi ya Jumapili ambayo kanisa ililipuliwa kwa Bomu vijana hao waluanza Maandalizi ya kwenda Nairobi nchini Kenya kumalizia ratiba yao ya Starehe ilioanzia Tanzania lakini kabla ya kuondoka ndipo walipo kamatwa.

TAARIFA ZAIDI:Soma gazeti la Raia mwema.

Kwani raia wa U.A.E hapaswi kukamatwa akituhumiwa Bongo, waache ujinga, hao ni watuhumiwa kama wakina Ambrose, hayo maelezezo watayatoa mahakamani! Mambo ya kuchimbana mikwara sjui sku tatu watoke ni kuingilia mambo ya mahakama na kudharau sheria zetu, hao waarabu wasubiri hukumu kama wanavyosubiri wakina Ambrose! Btw,hivi kile kikosi cha kung'oa kucha bila ganzi hakifanyi kazi huko, maana naona kuna watu hawatoi ushirikino wa kutosha!
 
Na bado, hili ni part gazeti tu, tutaona mengi sana!

...Mulogo sianasema wao ni serikali, wana nguvu nyingi sana, tunasubiria kuziona hizo nguvu zao sasa.
 
Kuna maswali ya msingi sana ambayo hayajapata majibu ya sawa sawa...Tukiassume waarabu wanahusika, Target angekuwa Balozi wa Vatican na Viongozi waandamizi wa Kanisa! Bomu lingekuwa na uwezo wa kufunika eneo lote la kanisa...
Well target wamekuwa waumini, Bomu lililotumika ni ndogo lengo hapa ilikuwa ni vitisho zaidi plus propaganda ya utengano wa udini kuendelezwa...in this case adui anaweza kuwa ndani ya Serikali na vyombo vya dola, anaweza kuwa ni miongoni mwa viongozi wa Kanisa kwani ilishawahi kutokea huko duniani, Inawezekana ikawa ni mpango wa kutugawa Watanzania ili waendelee kufaidi Rasilimali zetu kwani wanajua kuwa tukiungana itakuwa mwisho wao...TAFAKURI PANA INAHITAJIKA HAPA...
 
Awali ilikuwa waliwasili uwanja wa Ndege wa Arusha na sasa ishageuka waliwasili toka Dar es Salaam wakisindikizwa na rafiki yao mwenye asili ya Kiarabu....movie continues
 
Hili sinema limechezwa na jk.mulongo, nchimbi na wengineo..nyie subirini tu kuambiwa lema ndo kawaleta/kawatuma walipue
 
A%20S%20confused.gif

cool-quote-politics-police.jpg
 
Maofisa wa Ubalozi wa U.A.E Wanalalamikia polisi kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya Kimataifa vya habari na Wananchi wa Tanzania kupitia Waziri wa mambo ya ndani Dk Emmanuel Nchimbi kuwa raia wao wanahusika na tukio la Uhalifu lililotokea Arusha.

Kimsingi wametoa muda kwa Serikali ya Tanzania kuwaachia raia hao kwani nchi hiyo inaamini kuwa hawahusiki kwa namna yeyote na tukio la Arusha na kwamba kukamatwa kwao ni kinyume cha taratibu za sheria za Kimataifa.

Taarifa zinadai kuwa watuhumiwa wawili kati ya hao ni "ASKARI POLISI"wa nchi hiyo ya Falme za Kiarabu na Mwenzao mmoja ni Ofisa wa Ushuru wa Forodha wakati raia wa Saud anayeishi U.A.E ni mtaalamu wa maswala ya Moto.

Taarifa zinaonyesha kuwa vijana hao ambao wote ni watumishi wa Serikali waliwasili Jumatano iliyopita kwa likizo fupi ya kutembelea nchi za Afrika Mashariki na walitarajiwa kurejea U.A.E alhamisi wiki hii.

Taarifa zaidi zinabainisha kuwa baada ya kuwasili Tanzania na kutembelea jijini Dar es salaam kwa siku mbili vijana hao waliwasili Arusha Jumamosi wakitumia gari dogo la rafiki yao ambae ni Mtanzania mwenye asili ya kiarabu na kufikia hoteli ya Aquiline iliyopo jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi Jijini Arusha.

Usiku huo jumamosi taarifa zinaonyesha kuwa vijana hao walikwenda kustarehe katika Vilabu mbalimbali vya starehe wakihama kutoka Kilabu vitatu tofauti.ilipotimia saa 9 alfajiri walirejea ktk Hoteli waliyoifikia.

Asubuhi ya Jumapili ambayo kanisa ililipuliwa kwa Bomu vijana hao waluanza Maandalizi ya kwenda Nairobi nchini Kenya kumalizia ratiba yao ya Starehe ilioanzia Tanzania lakini kabla ya kuondoka ndipo walipo kamatwa.

TAARIFA ZAIDI:Soma gazeti la Raia mwema.

Swali la kujiuliza hapa je hawa raia walifuata taratibu zote za sheria kuja tanzania?...
Pia walipotaka kwenda kenya walishakamilisha taratibu zote??..au walitaka kuondoka tu kama vile unatoka tegeta unaenda ubungo??
Receptionist wa zamu katika hoteli hiyo anawaongeleaje wageni hao akihusianisha muda wa tukio katika siku hiyo??
Ikiwa serikali itaonyesha udhaifu katika hili basi tena!......
 
Mmmh hapa pananukia something !! kweli watapona hao? Sasa nchi kama hii mafunzo yote waliyo toa na gharama zote za walipan kodi na misaada yote ya kiUlinzi na usalama, hadi sasa hakuna TIJA !!! Sidhadhani patakuwepo na uadilifu au repoti yenye kuridhisha.... ukikutwa kwenye " WRONG PLACE and WRONG TIME " matokeo ni haya.
 
Back
Top Bottom