Kumbe wayao ni wenyeji wa mkoani Mtwara? Leo nimejifunza kitu jipya kupitia hapa JF.

Mi ni Myao pia wa Masasi,acheni kukariri
Uko sahihi.
kinachoongolewa hapa ni wapi mliko wengi..ukiacha uasilia wa Msumbiji Wayao wa Masasi wanaondugu/Koo zaa Tunduru.
Masasi Wayao wanapatikana kwa wingi maeneo machache kama vile eneo la Mtandi(Masasi Mjini),Mpindimbi,Chiwata na Nagaga.
 
Uko sahihi.
kinachoongolewa hapa ni wapi mliko wengi..ukiacha uasilia wa Msumbiji Wayao wa Masasi wanaondugu/Koo zaa Tunduru.
Masasi Wayao wanapatikana kwa wingi maeneo machache kama vile eneo la Mtandi(Masasi Mjini),Mpindimbi,Chiwata na Nagaga.
Wamakonde asili yao ndio Msumbiji,Wayao ni Malawi mkuu,hata hao wa huko Tunduru na kwingineko wayback walitokea Malawi.Hivyo Myao hana asili ya Tunduru
 
Wewe ni muongo asili ya wayao sio msumbiji
 
Wewe ni muongo asili ya wayao Yasio msumbiji
Soma nilichokiandika na kukielewa
...Large Yao Kingdoms came into being as the Yao Chiefs took control of the Niassa Province in Mozambique in the 19th Century.
During that time Yao began to move from their traditional home to today's Malawi and Tanzania which resulted in the Yao population(appr..2m Malawi, 4k Mzq, 6k tza) in the present today. LIKUD
 
Wamakonde asili yao ndio Msumbiji,Wayao ni Malawi mkuu,hata hao wa huko Tunduru na kwingineko wayback walitokea Malawi.Hivyo Myao hana asili ya Tunduru
Nakubaliana na wewe,Wayao wengi kwa sasa wako Malawi ila asili yao ni Msumbiji(soma hata maandiko), walikwenda Malawi na kuja Tanzania kwa sababu mbalimbali ikiwemo migogoro na jirani zako Wamakua na masuala ya kutafuta fursa(biashara) LIKUD
 
Asante kwa somo la historia.
 
GENTAMYCINE Habahatishi.

LIKUD hana Historia unaweza ukamwambia kuna wajaluo Tanzania atapinga aseme ni wakenya.

Huyo ndo hajaelewa Mkuu, amekurupuka.. Siku hizi hadi wasukuma wa Lindi na Kisarawe, Zanzibar wapo wengi tu.

Popoma alitaka kumaanisha " mmakua" kutoka Mtwara kwa sababu Siku zote ndio anaandikaga hivyo. Ila hapo juu alijisahau akaandika " Yao" kwa sababu hana unakuwa wowote isipokuwa huwaga anaandika kujivika umakua ili aonekane katoka kabila moja na Mzee Mkapa. Ndio maana anasemaga " Genius kwa kizanaki, kimakua na Kitutsi"

Ila kwa sababu ni muongo huwaga anaandika kubabaisha basi kwenye hiyo post amechanganya Madesa...

Wayao asili yao ni Malawi sio Msumbiji and they have nothing to do with wamakua. Ni vitu viwili tofauti.
 
wayao na wamakuwa ni watu wawili tofauti. Wayao kwao Tunduru, wamakua kwao Masasi.

Wamakua wana asili ya Msumbiji na Wayao wana asili ya Malawi.

At least hata wayao na wamwera wa Nachingwea na Lindi kiasi wana historia ya pamoja na ni watani.

In addition to that, Popoma siku zote anajitapaga kwamba yeye ni mzanaki, mtutsi na mmakuwa( kabila la mkapa)

Ila kwa kuwa watu wengi ambao sio wenyeji wa kusini huwaga wanayachanganya hayo makabila mawili ( wamakuwa na wayao) basi na yeye kajichanganya kwa sababu yeye hana uhusiano wowote na makabila hayo.

Kajisahau kwamba anasemaga yeye moja kati ya wazazi wake ni mmakuwa
 
Sawa lakini kwa Tanzania tunajua ni Tunduru ni kama Wangoni ambao inasemekana asili yao ni Afrika Kusini lakini kwa Tanzania ni Songea.
Na wazaramo pia wapo Dar na Pwani na huwezi kumlazimisha wa Dar umwambie yeye asili yake ni Pwani wakati hana hata ndugu yake anayemjua anayetokea Pwani
 
Na wazaramo pia wapo Dar na Pwani na huwezi kumlazimisha wa Dar umwambie yeye asili yake ni Pwani wakati hana hata ndugu yake anayemjua anayetokea Pwani
Kwanza Pwani na Dar ni kitu kimoja hata mipaka yake yote inajionesha wazi,Dar yote imezungukwa na mkoa wa Pwani na Wazaramo wote unaowajua wewe na usiowajua hata waishi wapi lakini asili yao ni Pwani,kama siyo Kisarawe itakuwa Mkuranga, Kibaha au Bagamoyo.
Mfano ni ile familia ya Tambaza ambayo ilimiliki Upanga yote,Kivukoni yote na eneo la Kigamboni asili yao ni Bagamoyo.
 
Mipaka ya huko kwingine wayback ilikuwa ni mimoja pia mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…