Kumbukizi Miaka 25 ya Nyerere; CCM Imetutosa Wastaafu, Kutudanganya na Kutudharau kwa Kauli za Mwigulu Bungeni

Kumbukizi Miaka 25 ya Nyerere; CCM Imetutosa Wastaafu, Kutudanganya na Kutudharau kwa Kauli za Mwigulu Bungeni

Mkongwe Mzoefu

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2018
Posts
861
Reaction score
2,515
Kwako Mwalimu Nyerere;

Wiki hii tunaitumia kukukumbuka wewe na uongozi wako.

Sisi wazee tunakumbuka mbali zaidi hasa zile nyakati za vita Kagera ambavyo wapo wenzetu ambao waliambulia vilema na mpaka leo tunao wakiwa hai na huku wakilipwa Pension ya Laki 1 kwa mwezi na Hazina na hakuna msaada wowote.

Wapo Waalimu, Waganga na wahandisi, makarani na wengine wengi waliokuwa Permanent and Pensionable wote bado wanalipwa hiyo laki mojamoja.

Cha kusikitisha Mwalimu, wale ambao Mungu amewaacha wawe hai kwa serikali hii ya CCM yako uliyoiacha wanaonekana ni chukizo na hasara, kwamba bora fedha zitumike kwa mambo yao ya anasa na sio kuwaongezea sehemu ya pension kama sheria isemavyo.

Waziri wa Fedha na huyu Rais aliyeko madarakani walituambia kupitia Bunge wameunda tume kuangalia jinsi ya kuboresha lakini hakuna lilofanyika.

Ila leo wanajinasibu kuwa eti wanafata falsafa ya mwalimu, jee hii ya kutowajali wazee ilikuwa ndio falsafa yako au wanakusingizia kwa vile uko Kaburini?

Tunaenda kwenye uchaguzi, bora tuwaeleze watoto wetu na wajukuu kuwa ANAYEMDHARAU MZAZI WAKO HASTAHILI KUPEWA HESHIMA YA KURA.

Mwalimu huko uliko tuombee mwisho mwema
 
Kwako Mwalimu Nyerere;

Wiki hii tunaitumia kukukumbuka wewe na uongozi wako.

Sisi wazee tunakumbuka mbali zaidi hasa zile nyakati za vita Kagera ambavyo wapo wenzetu ambao waliambulia vilema na mpaka leo tunao wakiwa hai na huku wakilipwa Pension ya Laki 1 kwa mwezi na Hazina na hakuna msaada wowote.

Wapo Waalimu, Waganga na wahandisi, makarani na wengine wengi waliokuwa Permanent and Pensionable wote bado wanalipwa hiyo laki mojamoja.

Cha kusikitisha Mwalimu, wale ambao Mungu amewaacha wawe hai kwa serikali hii ya CCM yako uliyoiacha wanaonekana ni chukizo na hasara, kwamba bora fedha zitumike kwa mambo yao ya anasa na sio kuwaongezea sehemu ya pension kama sheria isemavyo.

Waziri wa Fedha na huyu Rais aliyeko madarakani walituambia kupitia Bunge wameunda tume kuangalia jinsi ya kuboresha lakini hakuna lilofanyika.

Ila leo wanajinasibu kuwa eti wanafata falsafa ya mwalimu, jee hii ya kutowajali wazee ilikuwa ndio falsafa yako au wanakusingizia kwa vile uko Kaburini?

Tunaenda kwenye uchaguzi, bora tuwaeleze watoto wetu na wajukuu kuwa ANAYEMDHARAU MZAZI WAKO HASTAHILI KUPEWA HESHIMA YA KURA.

Mwalimu huko uliko tuombee mwisho mwema
Baadhi ya mabaya au ubovu wa Mwl. Nyerere:-
1. Kuiga, Kuanzisha na kuendeleza Sera na Itikadi Mbaya kabisa ya Siasa za Ukomunisti/Ujamaa hapa Tanzania.

Huu ndio ulikuwa mwanzo wa Kujenga Msingi mbovu wa Taifa la hovyo kabisa lililopo hivi sasa.
Itikadi na Sera ya Ukomunisti/Ujamaa ikaja kushindwa vibaya Sana huku yeye mwenyewe akishuhudia kwa macho yake kushindwa kwa itikadi yake aliyoileta hapa Tanzania kutoka kwa marafiki zake wa China, Urusi na Cuba.

2. Kutengeneza Taifa la Watu waoga, Wanyonge, dhaifu wa fikra wasiojitambua na Wala wasioweza kuhoji. Taifa la watu 'misukule'.

3. Kutengeneza au kuunda nchi isiyokuwa na Mipango-miji, hususani kupitia kwenye Sera yake mbaya kabisa ya ujamaa/Ukomunisti. Sera au Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti ndio ilikuwa chanzo Cha Kuanzishwa kwa Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, the Worse Operation that completely destroyed the Country and Town Planning process within the Country.
Arusha Declaration and Operation Vijiji also led to the Death of Real Estate Industry and its development.

Kupitia Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti, Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, Watu wengi sana walinyang'anywa Ardhi zao pamoja na majumba yao waliyokuwa wakimiliki. Nyumba nyingi sana za Watu zilitaifishwa, Leo hii nyumba hizo zinamilikiwa na Shirika la Nyumba (NHC).

4. Kutuletea Katiba ya nchi ambayo ni mbaya kabisa, isiyofaa na ambayo imesababisha na inaendelea kusababisha madhara makubwa sana kwa Raia. Katiba mbaya ambayo imewatengeneza Watawala wa nchi hii kuwa 'Miungu Watu.'
 
Back
Top Bottom