Kumbukumbu ya kifo cha Munga Tehenan

Kumbe Munga Tehnan alikuwa na dini?? Nakumbuka alinifundisha kuwa hakuna Mungu mwingine mbinguni na duniani isipokuwa mimi mwenyewe
 
niliwahi kuanzisha uzi humu kuulizia kama kuna yeyote mwenye habari njema za gazeti la JITAMBUE atujuze kama litarudi tena mtaani. Yaani sijawahi kuona gazeti zuri kama lile jamaa aliondoka nalo kabisa.
 
Mkuu habari za siku....................
Naomba tuwasiliane kuna habari njema kuhusu gazeti hilo la JITAMBUE..............................

mkuu ni habari njema kwe2 sote,wakt unataftana na huyo mpendwa hapo juu na wadau wengne naomba utukumbuke.
 
niliwahi kuanzisha uzi humu kuulizia kama kuna yeyote mwenye habari njema za gazeti la JITAMBUE atujuze kama litarudi tena mtaani. Yaani sijawahi kuona gazeti zuri kama lile jamaa aliondoka nalo kabisa.
Naweza kushangaa leo nikisikia maneno kama yako................. Labda kwa wale wasiojua, ukweli ni kwamba mimi ni mmoja wa waliokuwa waandishi wa gazeti lile na kusema kweli katika jambo ambalo lilimsumbua kichwa sana Hayati Munga mpaka anaenda kaburini ni kitendo cha gazeti lile kukosa soko la kuridhisha. Ingawa wengi leo wanalisifu sana hapa, lakini lile gazeti lilikuwa haliuzi ukilinganisha na magazeti ya udaku. Ilifikia mahali hata lilikuwa halirudishi hela iliyotumika kulichapa....! Kama mnakumbuka TK Media ilikuwa na magazeti mawili, Mshauri Wako ambalo lilikuwa likiandika habari za wanawake zaidi na hilo la Jitambue ambalo lilikuwa linaandika habari mbalimbali za kisaikolojia na utambuzi kwa ujumla. Ilibidi tuyaunganishe yote mawili ili kampuni imudu kujiendesha maana ilifikia mahali magazeti hayo yanaendeshwa kwa fedha za mifukoni. Leo hii nikisikia watu wanadai Gazeti la Jitambue lirudi.............inanishangaza kwa kweli.

Kuna ushahidi hapa hapa JF. Nimekuwa nikirejea baadhi ya makala za Jitambue hapa, lakini watu wanadai ni ndefu na hawawezi kusoma...............Awali nilitaka kuacha, lakini hao baadhi wanaosoma wamekuwa wakinipa moyo.
Mhusika anayeshikilia Gazeti hilo anataka kuliuza lakini kila mtu anaogopa kulinunua kwa sababu falsafa ya gazeti hilo haiuzi, nani angependa kuhatarisha mtaji wake? Inahitaji utambuzi wa hali ya juu kuliendesha gazeti la Jitambue la sivyo hakuna atakaye weza.

Hayati Munga aliwahi kuniambia kwamba anashindwa kuelewa kwa nini Gazeti la Jitambue haliuzi ingawa lina maarifa mazuri yanayoelimisha. Aliwahi kuandika katika mojawapo ya tahariri zake katika gazeti hilo kwamba Watanzania ni wavivu wa kusoma na hasa vitabu au magazeti yaliyosheheni maarifa na elimu. Wengi tunapenda kusoma habari za udaku, kitu ambacho yeye haikuwa ni falsafa yake. Ilibidi tuanzishe mradi wa Vitabu ili kama vikiuza basi vichangie kuliendesha gazeti hilo, lakini pia hilo lilishindikana.............Vitabu navyo havikuuza kama ilivyotarajiwa.

Kuna watu wenye ujuzi wa aina nyingi humu na wana uwezo mkubwa wa kuelimisha wengine, lakini wadau wengi humu hawako tayari kupokea maarifa hayo, sana sana utawasikia .... oooh ni ndefu sana... au Chapa Gazeti..........na maneno mengi ya kukatisha tamaa. kama mtu huna muda wa kusoma basi kaa kimya au print ukasome nyumbani.

Siamini kama Gazeti hilo litauza hata akipatikana mtu wa kuliendesha...................................
 

Watu kama wewe mlta mada ndio mnatufanya Watanzania kuonekana kweli ni taifa la "omba omba".

Huu upuuzi wa kumkumbuka nyinyi marehemu halafu mchangishe pesa za sadaka ni ujinga wa hali ya juu. Sadaka uitoe wewe, uje kuichangisha kwangu?

Wacheni utapeli na ujinga wa kuwa ombaomba na kutumia majina ya hawa marehemu kwa kujipatia ulaji.
 
Kusema kweli sikujua kama huyu ndugu alishatutoka. Ilikuwa lini? Imeniuma sana. Alikuwa kichwa. Kichwa kwelikweli. Pole nyingi kwa mjane na ndugu wengine. Nimeshituka!
 

Deeply sorry to hear this. Nakumbuka gazeti lilikuwa linafika Kigoma baada ya siku mbili Kufuatana na ratiba ya train, i never missed a copy of it.Though kuna wakati likaanza kuwa la kubahatisha mara lipo mara halipo( nadhani ni kutokana na soko kama ulivyoeleza). Limechangia pakubwa kunijengea confidence na kutokukata tamaa, i really miss it. I also read somewhere ulikuwa mmoja wa wahusika wa ile makala ya masahibu ya aibu (sometimes za kujitakia) yaliyokuwa yakiwafika watu (iliitwa siku niliyofedheheka kama sikukosea),hivi vile vilikuwa ni visa vya kweli au fiction?
 

Baadhi vilikuwa visa vya kweli vinavyotumwa na wasomaji na baadhi tulikuwa tunatunga kulingana na ujumbe tunaotaka kutoa kama elimu ya utambuzi.
Ilikuwa ni sehemu ya kuwafanya watu wajitambue..................... kwamba hata kama umetupwa kwenye pipa la taka kwa fedheha, lakini bado wewe ni binadamu kamili............. unaweza kusimama na kusonga mbele.
 

mkuu mtambuzi naomba kama inawezekana tuwasiliane na Invisible tuanzishe special thread au subforum kwa ajili ya makala za huyu jamaa mimi nakumbuka enzi hizo nilikuwa mwanza ukuchelewa siku mbili unakuta gazeti limekwisha kabisa mpaka wiki nyingine labda kuna watu walikuwa wanalihujumu mkuu.
 
Mimi ningeomba wadau wwnye nakala za huyu bwana ama kiwanda alichokuwa anachapa magazeti tuzikusanye tufanye gharama ya kuzichapisha hapa jf kama special thread.amini nawaambia makala zile zitawasaidia wengi

Mods tupe Sticky ya thread hii tafadhari.
 
Jamani hivi gazeti la Jitambue lilikufa na Munga!?
Mwanzoni pale mara tu baada ya Munga kufariki wauzaji wakaanza kusema litaanza kutoka muda si mrefu........tumesubiri weeeeee!!!! wapi!
Nasasa kuna kitu hiki kinaitwa FAJI nasikiasikia tu ndiyo nini? gazeti au?
 

Kama niko nalisoma vile......."unaweza kusimama na kusonga mbele" Haya makonfidensi niliyonayo yamechangiwa kwa kiasi kikubwa sana na Jitambue. Lakini Mtambuzi naomba kutofautiana na wewe. Wako majamaa wengi humu wanaolizimia gazeti hilo na mambo yake. Ni kiasi tu cha kuboresha mwonekano wake na labda likatoka kwa mwezi mara moja na tunaweza tunaolifahamu kununua hata kwa Tsh 3000/=.
 

FAJI ni kifupi cha FAMILIA YA JITAMBUE........... Ni mkusanyiko wa wanafunzi wa Utambuzi ambao walikuwa wanahudhuria madarasa hayo ya Utambuzi mtoa mada akiwa ni Hayati Munga Tehenan pale maeneo ya Kimara Rombo....Kwa sasa madarasa hayo yapo pale Tabata Kimanga kwa Dk. John.
 
Nakubaliana na wewe...........Lakini inahitaji kujipanga kidogo................. Ngoja nitaanzisha thread niwaombe MODS wai-sticky ili kukusanya maoni ya wadau namna ya kulifufua na kuliendesha..............
 
Nitakuwa najibu maswali hapa ya wale wenye kutaka kujua zaidi juu ya Gazeti hilo na hiyo shughuli ya kuadhimisha miaka mitano tangu kifo cha mwasisi wa Gazeti hilo Hayati Munga Tehenan..........................
 
Nakubaliana na wewe...........Lakini inahitaji kujipanga kidogo................. Ngoja nitaanzisha thread niwaombe MODS wai-sticky ili kukusanya maoni ya wadau namna ya kulifufua na kuliendesha..............

Usisahau wazo la kuwa na blogs au hata website ikibidi..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…