kumbukumbu ya siku CHOZI LA DAMU lilipochuruzika

Akili Kichwani

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2010
Posts
1,508
Reaction score
220
Wapendwa, mapema leo nimepata ujumbe huu kutoka kwa rafiki yangu mtanzania tunayesoma naye chuo kimoja. Ujumbe wenyewe unasema hivi :


"Dear AK, Praise the Lord. On this day I thank God for the might works He has done in my life to deliver me from the persecution I suffered under my family. Please glorify the name of the Lord wherever you are"


Ndio nikakumbuka kuwa leo ni tarehe 10 march!

Ni kwamba kwa kifupi, huyu bwana aliwahi kufukuzwa nyumbani kwao akalazimika kuwa mtoto wa mitaani, mengi yalimtokea maishani mwake, mfano amewahi kujaribu kujinyonga mara mbili Mungu anamuokoa hatimaye akaapa kuwa hatajaribu tena kujiua. Kwa miujiza ukafunguka mlango wa shule, akanza shule, shetani akamfuata na huko shule, akapata mateso makuu na wakati mwingine akiangukia mikononi mwa vyombo vya dola lakini Mungu anaingilia kati na kumuokoa na hatari ya kufungwa……….…………………..

Historia yake ni ndefu sana na akikusimulia lazima chozi likudondoke kama una roho ya utu japo kidogo…… lakini kwa sasa yuko huku ng'ambo anachukua PhD! Huwa ana tabia ya kusitisha ratiba yake yote na kutumia siku nzima kama hii ya leo kumshukuru Mungu kwa matendo makuu aliyomfanyia maishani mwake na pia kutembelea watoto wasio na makazi na kuwafariji. I wish ningekuwa naye nimjoin kwenye sala yake ya shukrani, bahati mbaya niko mbali lakini kiroho niko naye ......................

NB:
Niliwahi kuleta habari za mtu huyu hapa jamvini huko nyuma, nimesearch ile thread sijaiona, anayeweza kuiona atapata mengi zaidi huko.

FURAHINI NA SHUKURUNI KWA KILA JAMBO KWANI HAYO NI MAPENZI YA MUNGU
MUNGU AWABARIKI
NDUGU YENU
AK
 
Sijaelewa hapa tunatakiwa kufanya nini kuchangia kitu gani??
 
Sijaelewa hapa tunatakiwa kufanya nini kuchangia kitu gani??

lengo lake ni;
1.kukukumbusha kuwa ata kwenye mateso gan mungu yu pamoja nawe
2.mungu hamtup mja wake
3.shukuru kwa kila jambo cz hujui limekuja kwa nia/lengo gan
4.usife moyo kwa jambo lolote cz mungu ana makusud na anakupenda
5.usisikilize wala usife moyo kwa matendo mabaya bnadamu wanaokutendea cz ubaya wao haushind kudra za mungu

UMEELEWA SASA?
 
Sijaelewa hapa tunatakiwa kufanya nini kuchangia kitu gani??

Unatakiwa kumshukuru MUNGU KWA KILA jambo pia tembelea waliuo na shida na kuwafariji hata kwa maneno tu yatosha " hicho ndicho unatakiwa kuchangia" Pia kumsifu MUNGU anayekupa na kukushindia kila siku
 

Unatakiwa kumshukuru MUNGU KWA KILA jambo pia tembelea waliuo na shida na kuwafariji hata kwa maneno tu yatosha " hicho ndicho unatakiwa kuchangia" Pia kumsifu MUNGU anayekupa na kukushindia kila siku

asanteni wandugu kumfafanulia.............. mi nilipoona swali lake nilibaki nimepigwa na butwaa............

mbarikiwe...............
 

Atakua kaelewa sa ivi, asante kwa ufafanuzi my dear....

Unajua lengo la shetani always huwa ni kukupitisha katika bonde la uvuli wa mauti, kukuua hawezi, anakua anataka uogope, ukate tamaa, ugive up, ndo raha yake ilipo, maana ukishakata tamaa, hata mawazo ya kujinyonga, kujizira na n.k ndo yanatake advantage of you na kukushinda.....

So the best way to defeat him is never to give up, to give thanks to God unceasingly, and to let God's love consume you and heal you.
And if the devil reminds you of your past, just remind him of his future!!!!
 
asanteni wandugu kumfafanulia.............. mi nilipoona swali lake nilibaki nimepigwa na butwaa............

mbarikiwe...............
yaan jaman mwenyew nilishangaa
et hajaona cha kuchangia....bt kilichoko kichwan,MOYON ndicho kilichopo machon(ndicho unachoona)na ndicho kilichopo mdomon....
 

thax
umeongea vyema.
 

kweli mpendwa,......... Mungu wetu ni wa kushukuriwa siku zote, kwnani anatupenda sana, anatupenda upeo............. aweza kutupitisha kwenye maji/mito laini kamwe hawezi kutugharikisha....................
 
Nakushukuru Mungu kwa kuniuumba hivi nilivyo!!

Nakushukuru Mungu kwa kuwa umeniokoa na mtego wa mwindaji!!

Nakushukuru Mungu kwa kuwa wale wale walionichimbia mashimo ili nitumbukie, uliwaagizia malaika zako wakawakamata wakawatumbukiza katika mashimo yale yale waliyonichimbia mimi!!

Nakushukuru pia kwa ajili ya kazi yangu, huduma yangu, kanisa langu, rafiki zangu, na familia yangu kwa ujumla

Zaidi ya yote nakushukuru Mungu kwa ajili ya members wote wa JF, asante Bwana kwa ajili ya Dena, asante kwa ajili ya Michelle, asante kwa ajiliya Lizy, na wengine woteeeeeee, kwa maana imeandikwa watujua kwa majina yetu tena umeyachora katika vitanga vya mikono yako!!

Amen!!
 
kweli mpendwa,......... Mungu wetu ni wa kushukuriwa siku zote, kwnani anatupenda sana, anatupenda upeo............. aweza kutupitisha kwenye maji/mito laini kamwe hawezi kutugharikisha....................

Amen!!!!
 

Susy, Amen to that!!!
 
Leney!! inaelekea ww mvivu kuomba, unapenda kuitikia tu!! ha hahaaaaa haya bana!! huna hata kimoja cha kumshukuru Mungu??
 
am real touched by ur testimony! I glorify God for the might work to your friend, and this remind me on the grace of the good God!for wat so ever ups and down God has something huge in store for us,,,,Mungu amuinue zaidi
Thanks for this uplifting sharing,blessings
 
Leney!! inaelekea ww mvivu kuomba, unapenda kuitikia tu!! ha hahaaaaa haya bana!! huna hata kimoja cha kumshukuru Mungu??

Hahahah...yaani nikiwa nasoma shukrani hizo zote na mimi naweka na zangu, then mwisho namalizia na Amen kwenye thread..hahaha...

Ila tuache utani my dear mimi Mungu kanipendelea kupita upeo, yaani sometimes I just cry about it, am soo blessed, it even beats my understanding!!! nikipata misukosuko huwa nakumbuka ule wema wa Mungu halafu naacha kulalamika, maana wema na miujiza ni vingi huwezi kulinganisha na misukosuko ninayoweza kupitia....
Then pia, huwa namshukuru Mungu kwa UPENDO na FARAJA aliyonipa, kikombe changu kinafurika, na kutiririka kama mito ya baraka... yani acha tu mpenzi, ngoja niishie hapa, mwacheni Mungu aitwe Mungu!!!!
 

Amen!!!
mpenzi umeandikia hii post kwenye simu au??? maana hiyo font yake, babu Aspirin hawezi kusoma...LOL
 
yep; Hii ni grim reminder kwetu sote ingawa ningependa kama angefafanua zaidi kisa chake !
 
Leney!!

nimekupata!! nimekusoma my dia!! ni kweli Ayoub alisema

"mjue sana Mungu ili uwe na amani ndivyo mema ya nchi yatakavyokujia"
 
yep; Hii ni grim reminder kwetu sote ingawa ningependa kama angefafanua zaidi kisa chake !

Amesema ni story ndefu sana alishawahi kuipost humu.... hata mimi ningependa kuisoma, tumuombe aendelee kututaftia taratibu mpaka aipate....
 
Leney!!

nimekupata!! nimekusoma my dia!! ni kweli Ayoub alisema

"mjue sana Mungu ili uwe na amani ndivyo mema ya nchi yatakavyokujia"

Amen!!! huo mstari wa Ayubu umenikumbusha wimbo wa Sedekia!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…