Kumbukumbu zisizokoma

Kumbukumbu zisizokoma

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Kuna jambo moja la ajabu sana kuhusiana na uhifadhi wao nyaraka ndani ya medulla ya binadamu. Jambo hili lipo hata katika baadhi ya wanyama kama tembo japo kwa mtazamo tofauti kidogo. Hawa wanyama wana uhifadhi wa kumbukumbu wa kutisha mno.

Mfanyie jema au baya, Jambo hilo litakaa kwenye kumbukumbu zake miaka mingi mbeleni. Sasa kwa binadamu kuna baadhi ya kumbukumbu zisizotoka hata iweje na kwa sehemu kubwa huwa ni kumbukumbu za utotoni na sehemu ndogo ujanani.

Sehemu fulani nyumbani kijijini
Watu/mtu fulani nyumbani kijijini
Tukio fulani nyumbani kijijini
Ndoto fulani nyumbani kijijini nknk
Ni kumbukumbu zisizokoma na kila zinapokujia hukuletea hali fulani hivi
Fadhaa
Hamaniko
Furaha
Huzuni
Mshangao nk.

Matukio haya ya hizi kumbukumbu hayaji kama fikra za kawaida bali huuvamia ufahamu wako kwa sekunde kadhaa na kujikuta kama uko huko na kisha hutoweka kwa haraka na kukuachia tafakuri nyingi.

Ni katikati ya muda huu mchache
Tunaangalia lakini hatuoni
Tunaitwa lakini hatusikii
Tunasemeshwa lakini hatujibu.

Ni katikati hali hizi hizi ndio ajali nyingi hutokea na ni ajali ambazo hazina maelezo ya kueleweka. Ni kumbukumbu za ajabu kwenye ufahamu jadidi wa database ya uhifadhi wa nyaraka na matukio mbalimbali kwenye mwili wa binadamu.

Cha kushangaza na kustaajabisha zaidi ni kwamba kuna matukio makubwa yanatutokea maishani mwetu lakini database zetu huyakataa kuyahifadhi.

Kwanini? Mwili wa binadamu ni zaidi ya tuujuavyo!
 
Bongo zetu huchafuliwa sana kuanzia ujanani na kuendelea, ukiwa mdogo ni rahisi zaidi kushika au kuhifadhi vitu kichwani, mfano Mimi kiasili ni observer nakumbuka karibu nusu na robo ya watu wote darasani kwetu kuanzia darasa la pili Hadi la sita na nafasi zao za darasani yaani kwenye madawati lakini Leo hii ukiniambia niliosoma nao Advance ni wachache sana ninaowakumbuka. Yaani haiwezekani Ukumbuke shairi refu sana la kingereza la darasa la pili then definition ndogo tu tena rahisi ya advance uisahau?

Ni wakati Sasa wa kuondoa taratibu takataka zilizopo vichwani
 
Bongo zetu huchafuliwa sana kuanzia ujanani na kuendelea, ukiwa mdogo ni rahisi zaidi kushika au kuhifadhi vitu kichwani, mfano Mimi kiasili ni observer nakumbuka karibu nusu na robo ya watu wote darasani kwetu kuanzia darasa la pili Hadi la sita na nafasi zao za darasani yaani kwenye madawati lakini Leo hii ukiniambia niliosoma nao Advance ni wachache sana ninaowakumbuka. Yaani haiwezekani Ukumbuke shairi refu sana la kingereza la darasa la pili then definition ndogo tu tena rahisi ya advance uisahau?

Ni wakati Sasa wa kuondoa taratibu takataka zilizopo vichwani
Hizi takataka tuaziondoaje mkuu...hebu tupe njia kama unayo
 
Kukumbuka vya primary school na kusahau vya secondary na advance hii huwa inanileteaga maswali sana yani
Ujue vya Advance wakati unajaribu kuviingiza kichwani ulikua na mambo mengi ya pembeni...ie ujana..mahusiano...mawazo ya kifamilia mfano ada..sijui chakula tutakula nini...mara sina uniform..n.k
 
Kwa hio inatubidi tuchukue tahadhari sana maneno na matendo yetu kwa watoto, jwa sababu kila neno na kila tendo hubaki kwenye kumbukumbu zake karibu wakati wote wa maisha yake.
Hata mzee anapo poteza baadhi ya kumbukumbu kwenye ufahamu wake hurejelewa na matukio ya utoto wake ndio maana wakati mwingine wanakuwa kama watoto.
 
Hizi takataka tuaziondoaje mkuu...hebu tupe njia kama unayo
Meditation ama kwa kibantu tahajudi
The use of microchip inserted in our brain is the solution to this
Hicho kifaa kina madhara makubwa maana ni kivamizi (intruder) mwilini kisicho na uasili wao uhai
Kwa hio inatubidi tuchukue tahadhari sana maneno na matendo yetu kwa watoto, jwa sababu kila neno na kila tendo hubaki kwenye kumbukumbu zake karibu wakati wote wa maisha yake.
Hata mzee anapo poteza baadhi ya kumbukumbu kwenye ufahamu wake hurejelewa na matukio ya utoto wake ndio maana wakati mwingine wanakuwa kama watoto.
Sahihi kabisa
 
...
20240827_223650.jpg
Hata hivyo, utafiti unaonyesha kwamba mara nyingi wanadamu hukumbuka matukio mabaya au ya kiwewe juu ya mazuri. Kukumbuka huku kwa kudumu kwa kumbukumbu hasi kunaweza kuwa njia ya utetezi ya mageuzi, lakini kunaweza pia kusababisha vikwazo vya kisaikolojia, kama vile unyogovu au wasiwasi.
 
Back
Top Bottom