Kenya 2022 Kumekucha Kenya: Tume ya uchaguzi yaidhinisha wagombea binafsi 38 wa Urais. Tanzania tuna mpango gani?

Kenya 2022 Kumekucha Kenya: Tume ya uchaguzi yaidhinisha wagombea binafsi 38 wa Urais. Tanzania tuna mpango gani?

Kenya 2022 General Election

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mgombea binafsi ni yule ambaye hatumii tiketi ya chama chochote ili kuweza kugombea nafasi ya kisiasa kama Urais na Ubunge. Kenya Walipitisha sheria hii March mwaka huu na wameidhinishwa wagombea Urais na ugavana bila kupitia chama chochote.

Wagombea 38 wameidhinishwa nafasi ya Rais nchini Kenya huku magavana 74 wakichonga nembo zao binafsi badala ya kutumia nembo za vyama vya siasa. Changamoto inayoonekana ni urefu wa orodha kwenye karatasi ya kupigia kura.

Nakumbuka wakili msomi, Mchungaji Mtikila enzi zake alitamba na hoja hii mpaka akafungua kesi ya kikatiba lakini bahati mbaya wazo lake liligonga mwamba mpaka anaaga dunia mwaka 2015 siku chache kabla ya uchaguzi.

Labda wabunge wetu wasipofungwa na vyama wanaweza kupata mawazo huru bungeni na kuwa na mgombea binafsi kwenye nafasi ya Urais kukabadili upepo hasa kwa wale wanaokatwa lala salama katika michakato ya vyama vyao. Pia inaweza kupunguza kugombania vyama kama kinachotokea NCCR na kule kwingine kambi mbili kuwa na vuguvugu kwenye chama kikongwe linalotarajiwa kuwa dhahiri 2025.

Hivi hili jambo lilikufa na Mtikila?
 
Duuh aisee,kumbe ajira ni tatizo kubwa Africa nzima
Wengine wanaongeza c.v wengine wapo kimkakati kupunguziana kura, wengine ni mamluki tu, wengine wanataka kukuza majina yao, wengine wana nia ya dhati kuupata Urais, wengine...

Sio kila kitu kimelenga ajira
 
Wengine wanaongeza c.v wengine wapo kimkakati kupunguziana kura, wengine ni mamluki tu, wrngine wanataka kukuza majina yao, wengine wana nia ya dhati kuupata uraisi, wengine...

Sio kila kitu kimelenga ajira
Hayo yote unayoyasema bahati nzuri umejipa jibu mwenyewe kuwa wanaongeza sivi......unapoongeza sivi unataka nini kama siyo kutafuta ajira?
 
Wengine wanaongeza c.v wengine wapo kimkakati kupunguziana kura, wengine ni mamluki tu, wrngine wanataka kukuza majina yao, wengine wana nia ya dhati kuupata uraisi, wengine...

Sio kila kitu kimelenga ajira
Kenya wapo mbali sana.
 
Hayo yote unayoyasema bahati nzuri umejipa jibu mwenyewe kuwa wanaongeza sivi......unapoongeza sivi unataka nini kama siyo kutafuta ajira?
Fame
Status
Kutumia umaarufu ulio upata kwa ajili ya gain mbalimbali za kijamii kiuchumi n.k. sio mpaka ukaajiriwe.

Kwa mfano. Kiongozi fulani wa kisiasa anaye aminika anaweza kuanzisha mchango wa kitaifa na kuraise hadi bilioni moja na baadae usisomewe mapato na matumizi ya hizo fedha.
 
CCM wanaogopa mgombea binafsi kwamba eti vyama vya siasa vitakosa nguvu kama wakiruhusu hilo.
CCM bado ina falsaha za kizamani saana.
 
Mgombea binafsi ni yule ambaye hatumii tiketi ya chama chochote ili kuweza kugombea nafasi ya kisiasa kama Urais na Ubunge. Kenya Walipitisha sheria hii March mwaka huu na wameidhinishwa wagombea Urais na ugavana bila kupitia chama chochote....
Tanzania Kazi ni kuwakata Wagombea wote wa Upinzani

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Mgombea binafsi ni yule ambaye hatumii tiketi ya chama chochote ili kuweza kugombea nafasi ya kisiasa kama Urais na Ubunge. Kenya Walipitisha sheria hii March mwaka huu na wameidhinishwa wagombea Urais na ugavana bila kupitia chama chochote.

Wagombea 38 wameidhinishwa nafasi ya Rais nchini Kenya huku magavana 74 wakichonga nembo zao binafsi badala ya kutumia nembo za vyama vya siasa. Changamoto inayoonekana ni urefu wa orodha kwenye karatasi ya kupigia kura.

Nakumbuka wakili msomi, Mchungaji Mtikila enzi zake alitamba na hoja hii mpaka akafungua kesi ya kikatiba lakini bahati mbaya wazo lake liligonga mwamba mpaka anaaga dunia mwaka 2015 siku chache kabla ya uchaguzi.

Labda wabunge wetu wasipofungwa na vyama wanaweza kupata mawazo huru bungeni na kuwa na mgombea binafsi kwenye nafasi ya Urais kukabadili upepo hasa kwa wale wanaokatwa lala salama katika michakato ya vyama vyao. Pia inaweza kupunguza kugombania vyama kama kinachotokea NCCR na kule kwingine kambi mbili kuwa na vuguvugu kwenye chama kikongwe linalotarajiwa kuwa dhahiri 2025.

Hivi hili jambo lilikufa na Mtikila?
Kwa hiyo mgombea Binafsi akishinda uraisi ataunda pia Serikali Binafsi?
 
Raila Odinga ndie next president wa Kenya ishapangwa na wakuu wa dunia baada ya kukubali ajenda zao, uchaguzi uliopita alishinda wakamuibia kura sababu hakukubali ajenda za wakubwa wa dunia.
 
Back
Top Bottom