Kumekucha: Wachezaji waandamizi wa KMC FC wanalalamika jana Kutokupangwa na badala yake 85% kupangwa wale Wakaa benchi Wazoefu

Pamba inacheza mpira mzuri sana kuliko kmc na wakikutana kmc lazima alale hapa naona coastal union wamepigwa tayari
 
Ligi yetu externally Inakua lakini internally inakufa.

Makocha wa nje wanaokuja kufundisha bongo ndo wanaoweza kuliona hili kirahisi zaidi au ukiwa sio mshabiki wa simba au yanga unaweza kuliona pia.
yanga anaiua kwa kusambaza bahasha alianza kumpa jamaa nyau akamwachia 5-1 kaja jana kaongeza fungu kaachiwa 6-1 tarehe 8 inaweza kuwa 7-1
 
Unafanya Comparison ya vikosi / wachezaji wa KMC walioanza kwenye mchezo wa jana na Yanga bado unashindwa kuwataja kwa Majina.

Ungeweka kikosi cha kwanza cha siku zote cha KMC (best eleven yao)
Then ukaweka cha jana ili tuone kama kuna ukweli ndani yake.

The rest
 
Ligi yetu externally Inakua lakini internally inakufa.

Makocha wa nje wanaokuja kufundisha bongo ndo wanaoweza kuliona hili kirahisi zaidi au ukiwa sio mshabiki wa simba au yanga unaweza kuliona pia.

Exactly mkuu umeongea kitu cha Muhimu sana.
Hizi ndio hoja za maana tunazozitamani kuziona hapa JF.

Ila Taifa letu linazidi kudidimia kila sekta.
 
Utopolo gsm kazinunua team 6

Matokeo ya timu za GSM yana walakin mkubwa sana. Inafikirisha kwamba makocha wa timu zote wana DNA za Utopolo.. Pamba, Coastal, KMC, Dodoma JiJi, Singida, .... Ni kama inapangwa tu nani yuko chini abebwe asishuke daraja. Na ni kama imeshapangwa point zote sita za mechi dhidi ya Uto shurti zichukuliwe na Uto.
 
Wachezaji 9 wa first eleven jana wameanzia benchi, kali yanga alishavuta bahasha yake mapema.

Baada ya kufungwa 6 kwa 1 akamaliziwa hela yake. Wachezaji wa kmc wamelalamika sana kutokana na hujuma dhidi yao.

Ukitoa penati 4 walizopewa yanga mechi ilitakiwa iwe sare.
 
unaongea upumbavu
kwamba siku hizi
1.kenny
2.shemvuni
3.redemtus
4.lanso
5.tangalo
6.okoyo
7.hance masoud
ni chaguo la pili, weka kikosi kilicho cheza na nyau uone walio kosekana kwenye kikosi na wanachi ni wangapi
 
mkuu hapa umedandia treni kwa mbele kwa kukusaidia katazame kikosi kilicho cheza na azam tarehe 06.02.2025 na azam kushinda goli 2-0 ndicho kikosi kilicho chezea 6-1 kwa wananchi

tofauti kikosi cha azam alicheza saliboko kikosi cha yanga alicheza okoyo

hata mleta bandiko nikimwambia alete kikosi cha kwanza cha KMC ataona aibu kwa ujinga alio andika

kama ni kuuza mechi tuanze na mechi ya KMC na azam maana kikosi kilicho cheza na yanga ndicho kilicheza na azam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…