TheForgotten Genious
JF-Expert Member
- Jan 18, 2014
- 2,087
- 3,156
Labda kama kazi ni ya babae ndio hatofanyiwa interview
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ivyo amevifanya chuoni na sio kwenye ajira sasa ni lazima wathibotishe kama anavyo kweliHivyo vyote sijui tabia, client care, humanity na vingine deep sana mpaka psychology ashavisoma na kafanya mitihani huko chuoni ya oral na written tena migumu ilioshiba, it doesn't make sense kwenda kumpima tena upya
Hata sisi wakati tunajiunga na chuo kikuu cha Dar es salaam miaka hiyo pamoja na kupata division one zetu kali kabisa kwenye kidato cha sita, bado tulifanyishwa mtihani wa kukubaliwa kujiunga na chuo uliofahamika kwa jina la matriculation!Just imagine kijana kapata division one ya 7 au 10 form four kaenda high school kupiga PCB. Kapambana sana kachakaa kajitesa kajinyima kapata division one form six ya point tatu au tano.
Kaaply Muhimbili University kapitia mchujo katoboa akaanza masomo ya udaktari.
Kasoma miaka mitano bila kudisco tena kwa mateso makubwa bila kula bata mpaka kamaliza chuo.
Kabla hajaingia intern kafanyishwa mtihani wa MEDICAL COUNCIL OF TANGANYIKA katoboa kaanza interniship.
Kapiga intern kwa mwaka mmoja kisha kamaliza kisha kapigishwa pepa lingine la MCT katoboa.
Kasajiliwa na kutambulika kama MEDICAL DOCTOR na MCT.
Kijana huyu wa kitanzania aliyesoma kwa kujinyima na kujitesa tangu kidato cha kwanza leo hii anafanyishwa interview tena written interview sio prectical interview ili iweje?
Huyu kijana akikosa nafasi mnajua stress atakazopata mtaani na jamii inayomzunguka?
Hiyo michujo yote alopitia akipata ajira mnamlipa milioni moja na laki mbili ukitoa makato anabeba laki tisa bado mnampigisha interview ya nini sasa?
Hamuoni kama mnakatisha tamaa vijana waliopo shuleni na vyuoni?
Wadau
====================
UPDATES
Kwa taarifa nilizozipokea ni kwamba vijana wameitwq huko Galanos sekondali wakafanyiwe interview ya makaratasi
Hii nchi inashangaza sana