Elections 2010 Kumkapenia Kikwete kwamgarimu Mwakyembe

Kweli Dr. anajidhalilisha sana,, yeye alikuwa anapiga vita ufisadi iweje leo anasema watu wampe kura Jk.. Dr.. soma nyakati jamaa habebeki hata kwa toroli....

Chadema mwendo mmoja kuelekea ushindi wa kishindo kwa Urais, Wabunge na Madiwani
 

Unamtetea Mwakipesille na kutaka kutuaminisha kwamba ugomvi wao hauna athari yoyote? Then you must be out of mind maana hata mtoto mdogo anajua uhasama uliopo na jinsi unavyoathiri maendeleo ya Kyela.
 

Jaba za nini? Jibu hoja!
 
Wale wale, wameanza tena na mbofumbofu zao, baada ya kushindwa kwenye kura za maoni kwa aibu sasa wanaanzisha mijadala ya Kyela na Dr Mwakyembe kuwalisha watu uongo wao. Hivi hamjifunzi tu, na kama kuna watu wenye kutakiwa kusoma alama za nyakati basi ni hawa wenye kuendesha siasa za majitaka kwenye jombo la Kyela wakiwalazimisha wapigakura kumkataa Dr.

Nimehudhuria baadhi ya mikutano ya Mwakyembe, hakuna hata sehemu moja anayomkashi Dr Slaa au Prof Lipumba. Anawaeleza wazi wasikilizaji wake hao wawili anawaheshimu na ni Watanzania wenye uwezo mkubwa wa kiongoza nchi. Anaitaja tofauti yao na JK kiasi cha yeye kumkampenia JK ni kwa sababu anataka JK amaalizie ahadi zake kwa wana Kyela.

Kwa taarifa yenu, Kyela hawabebwi kwenye malori ni wtu wenye kefuatilia mambo, husafiri kwa baiskeli zao. Jee ina maana walioenda kumshuhudia Ridhiwani kule Ipinda nao walibebwa kwenye malori!!! Tuache chuki, hazina baraka.
 
nasema tena, inahitaji ujasiri wa kifisadi na upofu wa akili kumtetea Kikwete mbele ya watu wenye akili Timamu, mashemeji zangu WanyaKyusa wakimchukia Mtu, wanamuonesha kwa vitendo, kejeli na dharau, hahaaah.
hata wale Jamaa Mbozi , walikataa kusuruhishwa na Ridhwani Kikwete, kwakua hana Hadhi wala uwezo wakuwaweka meza moja.
 
Aliyeongoza zoezi la kumpa Ridhiwani heshima uchief ni Mwenyekiti wa zamani wa CCM Wilaya ya Kyela, Gracewell Mwakalukwa. Huyu hatokani na ukoo wa kitawala huko Kyela, ni kibaraka mkubwa wa Mwakipesile na hii yote ni kujikomba kwa JK. Kwa taarifa Dr Mwakyembe hajawahi shiriki hata mara moja katika matukio hayo kwa sababu watoaji huo uchief hawana sifa hiyo.

Pili Mwakipesile hajaathiri maendeleo ya Kyela tu bali mkoa mzima wa Mbeya. Mfano mmoja ni elimu, Quaresi ameiacha Mbeya ikiongoza katika mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi, leo hii tangu Mwakipesile apewe huo mkoa, Mbeya imeporomoka vibaya, inashika nafasi za kuanzia namba kumi na moja, lakini unamkuta mgombea bila aibu kwenye kura za maoni anawaomba wananchi wamchague kwa sababu anapatana na Mwakipesile!!!!

Kwa ufupi Mwakipesile na kundi lake wanaidhalilisha sana Kyela na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla na wamechangia kurudisha nyuma maendeleo mkoa huo.
 
mimi nasema watawalambalamba wanafamilia ya Kikwetee, ila hatima ya yoote ni waTanzania kuwatosa October 31.
 
mwakyembe nae kutetea chama badala ya watz umeanza kuboa sasa.........................unaweza usipite ubunge kwa style hii kwni nawe unaonekana kuna mambo mengi unayajua kwenye richmond ambayo umewaambia watz kuwa huyasemi wewe na kamati yako kwani itakuwa aibu kwa serikali......sasa tukianza kukung'ang'ania huwezi kutoka hapo...........hebu jichunguze na ujirekebishe tunakuheshimu sana kwa kuongoza kamati ile teule ya richmond kuchumguza kiampuni ile ya akina kikwete,rostamu na lowasa............
 

Nsesi
Fungua mubichwa,maendeleo yanarudishwa nyuma na CCM na wala sio Mwakipesile..Ondoa hiyo CCM,Mbona umengangania humo humo?
 
Kwa ufupi Mwakipesile na kundi lake wanaidhalilisha sana Kyela na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla na wamechangia kurudisha nyuma maendeleo mkoa huo.

Mwakipesile hayupo peke yake katika kuwadhalilisha wana Kyela, kundi la Mwakipesile ndilo hilo hilo kundi la Mwakyembe - wote ni manyang'au. Ni kawaida kwa manyang'au kugombania mzoga na mambo yanapoanza kuwa magumu huweza hata kutafunana wenyewe kwa wenyewe lakini mwisho wa siku hulala pamoja, hawatupani. Yawezekana Mwakipesile na Mwakyembe hawapendani lakini wote ni wana CCM na kwa taarifa zaidi wote wanampigia tafu Kikwete kwa Uongozi bora kwa mtindo wa kubali uliwe kama nawe wataka kula !.
 
Kama usemayo ni kweli basi Tanzania imeamka na Mwaka huu mabadiliko ya kweli yatakuwa makubwa mno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…