Kumkosoa sana ni dalili kuwa huyo sio wako bali unamlazimisha afanane na umtakaye

Kumkosoa sana ni dalili kuwa huyo sio wako bali unamlazimisha afanane na umtakaye

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
KUMKOSOA SANA NI DALILI KUWA HUYO SIO WAKO BALI UNAMLAZIMISHA AFANANE NA UMTAKAYE.

Karibu kila mtu ana taswira ya nani anamtafuta kama mwenzi/rafiki hivyo siku ukikutana naye utamtambua kuwa ndiye kutokana na kuendana na sifa utakazo.

Kosa kubwa tufanyalo ni kumlazimisha ambaye siye ili awe ndiye na hapo ndipo wengi tunageuka washauri wa mahusiano yetu wenyewe kwa muda mwingi kwa lengo la kutaka awe yule ambaye unamtaka.


Ukiona kwa asilimia kubwa unamkosoa sana ili abadilike jua tayari upo kwa mtu ambaye siye sasa unafanya zoezi la kumbadilisha awe ndiye.

Kitu kigumu kuhusu binadamu kadri unavyoongeza juhudi za kumbadilisha naye anaongeza juhudi za kubaki vile alivyo kwa sababu ki asili binadamu hapendi kubadilishwa.

Kuna kanuni moja nzuri na ngumu hapa isemayo ikiwa huwezi kumpenda alivyo basi mwacha alivyo tofauti na hapo utageuka mshauri na mkosoaji wake kila siku

#Mwanasayansi Saul kalivubha.
#Mitandaoni fikia ndoto zako
 
Hakuna perfect, ila hakikisha unachagua yule ambaye changamoto zake ni zile unazoweza ku deal nazo au kuzimudu, ukihisi ni kubwa achana naye.
Mambo ya kusema atabadilika/au nitambadilisha tayari umekuwa mtumwa na mtunzi wa nyimbo za malalamiko na masikitiko
 
Wanasema upendo unafunika madhaifu ivyo ukiona unaona mapungufu yake mengi kuliko mazuri yake ujue ujampenda kwa upendo wa agape
 
Hakuna perfect, ila hakikisha unachagua yule ambaye changamoto zake ni zile unazoweza ku deal nazo au kuzimudu, ukihisi ni kubwa achana naye.
Mambo ya kusema atabadilika/au nitambadilisha tayari umekuwa mtumwa na mtunzi wa nyimbo za malalamiko na masikitiko
Kweli kabisa
 
Hakika wewe nimwanasayansi nguli,umepita mulemule mkuu.uzidi KUBARIKIWA
 
Mi ndo mana wanaume wa hivyo nlikua naachana nao haraka sana najua sio wangu na atanisumbua badae mtu kakukuta upo simple anakulazimisha uwe slay queen mara weka kucha vaa wigi vaa hivi khaa
 
Back
Top Bottom