Kumlazimisha mtu kutoa sadaka ya shukrani kwa kufiwa na mama yake aliemuuguza miaka 10 kwa cancer na stroke yenye mateso makali sio sawa

Kumlazimisha mtu kutoa sadaka ya shukrani kwa kufiwa na mama yake aliemuuguza miaka 10 kwa cancer na stroke yenye mateso makali sio sawa

FRESHMAN

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2011
Posts
9,137
Reaction score
34,793
Habari wadau

Kuna familia imepata msiba wa mama yao. Mama huyo amefariki kwa mateso makali ya kuugua kwa zaidi ya miaka 10. Mama huyo alikuwa na cancer na Stroke pia.

Familia imeuza mali zao karibu zote katika harakati za kumtibia mama yao na mateso ya kisaikolojia ya kuuguza wamepitia sana kama familia.

Cha kushangaza baada ya mama yao kufariki Jumuiya na kanisa inawalazimisha wakatoe sadaka ya shukrani Kanisani.

Familia inajiuliza kwa nini tukatoe sadaka hiyo? Maana ni sawa sawa na kwenda kumshukuru Mungu kwa kumtesa mama yao kwa magonjwa makali. Yaani mgonjwa ateseke miaka 10 na bado wakatoe sadaka ya kushukuru mateso hayo? Huyo anayetaka sadaka kwa nini hakuzuia mgonjwa asipate maumivu na mateso ili apate sadaka ya kushukuru kweli kwa kumponya mgonjwa?

Kwa upande wangu naona familia ipo sahihi, kwa upande wenu wadau mnaonaje hili ?
 
Mgonjwa angekuwa amepona hapo ndipo sadaka ya shukrani ingeweza kutolewa kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kumponya mgonjwa,lakini kwa sasa hivi watu wamegeuza sadaka kama sehemu ya mapato ndiomaana wanafanya vitu pasipokufikri.
 
Mgonjwa angekuwa amepona hapo ndipo sadaka ya shukrani ingeweza kutolewa kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kumponya mgonjwa,lakini kwa sasa hivi watu wamegeuza sadaka kama sehemu ya mapato ndiomaana wanafanya vitu pasipokufikri.
Sasa hivi mambo ya Siasa yamehamia kwenye dini.
Sasa hivi Ccm wanasifia kila jambo kwamba amefanya au ameleta Samia.
The same kwenye dini tunaambiwa Tutoe sadaka ya Shukrani hata kwa mabaya yaliyo tupata,
Yaani kwa ufupi tushukuru Mungu kwa kila jambo.
WTF
 
Kutoa sadaka ya Shukrani hailazimishwi...wana familia wafanye wanavoona kwao no sawa
 
cha kushangaza baada ya mama yao kufariki Jumuia na kanisa inawalazimisha wakatoe sadaka ya shukrani Kanisani.
Sadaka ya shukrani hutolewa katika misa ya shukrani. Hakuna jumuiya inayoweza kumlazimisha mtu yeyote aombe kufanyiwa misa ya shukrani. Labda yalikuwa matoleo ya kitu kingine. Misa ya shukrani sio lazima, wengine hufanya na wengine hawafanyi, ingawa ni muhimu kufanya. Pili, misa ya shukrani huwa zaidi kwa ajili ya matokeo ya uwekezaji, uwe wa afya yako, elimu, kazi, biashara nk
 
Kama siyo utapeli wangekuwa wanatupa maandiko yanayoonyesha mifano ya watu waliomshukuru Mungu baada ya kufiwa na watu! Tunamshukuru Mungu baada ya kutufanyia jambo jema mf.ametuponya na magonjwa,ajali au mabaya yote aliyokusudia Shetàni juu yetu.
Na mara nyingi tunashukuru kwa kutoa shuhuda Kanisani au po pote ambazo zinaweza kuambatana na Sadaka ya Shukrani ambayo Mtu ataitoa kwa hiari yake.
Siyo kwa ujanja ujanja wa Wachungaji.
 
Back
Top Bottom