Kumng'oa Mangungu Simba ni vigumu kama kuing'oa CCM madarakani

Mangungu anaweza toka, kama wanachama na mashabiki mkiwa wamoja, machawa ni asilimia chache sana. Tatizo la wanachama wengi mmetawanyika, hakuna watu warahisi kuwatawala kama walio tawanyika
 
Naomba kuuliza mambo mawili mkuu kwako? Majukumu ya Mangungu pale Simba ni yapi na je anayatimiza?
 
Kwani Nkwabi alipojiuzulu lipi la maana lililofanyika?
 
Kwa hiyo 5imba kufanya vibaya msimu huu tatizo sio fedha chafu za GSM tena bali na Ngungus Boy?
 
Mangungu, Try Again na Mo kati yao pamoja na kujifanya ni wana Simba lakini kati yao hakuna mwenye uchungu na Simba. Kwa mtu mwenye uchungu wa kweli na Simba na jinsi matokeo yaliyo mabovu kwani siku ile ile ya zile goli tano hao wangeshajiuzulu bila hata kushinikizwa na mtu. Ila hao jamaa wapo kimaslahi hapo Simba na lazima kuna madudu watakuwa wameyafanya hapo Simba ndio maana pamoja na kufeli kwenye kila kitu bado wanaogopa kuondoka. Ingekuwa enzi zile za JPM saa hizi vyombo vya dola vingekuwa vimeshajipenyeza kimya kimya saa nyingi na kufunua uozo wanaojaribu kuuficha kwa kuendelea kubaki Simba.

Huwa najiuliza huyu Mo ambaye zamani alikuwa hana simile na makocha na wachezaji waliokuwa wanafeli ni Mo huyuhuyu au ni Mo mwingine? Vipi leo amvumilie Try Again aliyemweka mwenyewe pamoja na kupoteza makombe yote toka aachiwe timu miaka mitatu iliyopita?

Na viongozi wa matawi siku hizi wote ni machawa? Nilitegemea mpaka sasa hivi wawe wameshaitisha mkutano wa viongozi wa matawi na kuanza kutafuta saini za wanachama ili kuiomba serikali iwalazimishe viongozi wa Simba waitishe mkutano wa wanachama ili wanachama wamuhoji Mangungu. Wakiridhika na maelezo yake wamwache aendelee ila wakiona hatoshi wamuondoe waweke mwenyekiti mwingine.

Simba wasipowekana sawa sasa hivi basi wategemee mwaka mwingine wa huzuni kuu kwani usajili unaanza hivi karibuni na usajili ndio kila kitu.
 
Wanachama wa Simba wa Dar es Salaam waliomrudisha Mangungu madarakani wametukosea sana sisi wana Simba wote wa Tanzania.
 
Kwa hiyo 5imba kufanya vibaya msimu huu tatizo sio fedha chafu za GSM tena bali na Ngungus Boy?
Fedha chafu zinapenya kirahisi kama uongozi sio madhubuti.
Jiulize kwa nini Inonga aliuza mechi nyingi za Simba na kutuchomesha?Unadhani nani anaweza kufanya michezo michafu kama hiyo?
 
Nafasi ya tatu kwa hisani ya Mangungo! Nafasi ya tatu kolo kapendeza hajapendeza? Kapendeeeeeeza!
Ikiwa wewe ni kolo na hujakereka na huyu jamaa unahitaji kupewa honorary doctorate!! Yaani angekuwa Simba angetuua uto, ila ni wakwetu tunamcheka tu my wetu! Yanga kuna raha jamani mojawapo ni Ally Kamwe, salute!!
 

Attachments

  • sokavibe6_1717060562453222.mp4
    3.3 MB
huwa natamani mikoani zitokee timu zinazojitambua, viondoe ufalme wa hawa washirikina wawili......

hizi timu watu wanazishabikia kwa sababu hawana plan b, timu za mikoani kwetu ni utopolo kupitiliza
 
Kwa nn mangungu asitoke akajiajiri kama wanavyotuambia kila siku halafu manara anamtetea sana mangungu sasa hivi nimeshaanza kupata majibu.
 
Ndugu zangu Wazaramo huwa na neno moia wanaliita Bangusilo, yaani pangusio. Naona hapa Mangungu kaanza kutumika kama Bangusilo.

Kwamba Mangungu ndiye kafanya timu isimalize ligi ikiwa kwenye nafasi mbili za juu. Ndiye kachaguliwa atajwe kuwa chanzo cha kukosa ubingwa.

Yaani mjumbe wa bodi kama alivyo Asha Baraka ndiye awe na nguvu utekelezaji wa majukumu ya kila siku ya timu kuliko CEO na Mwekezaji na Mwenyekiti wa Bodi.

Wanasimba, kikatiba Mangungu hana nguvu yoyote kwenye timu, zaidi ya kuwawakilisha wanachama kwenye kikao cha Bodi ya Simba.

Kama tuna hamu sana ya kumpa Mangungu lawama tukikosa ubingwa, basi kwanza tubadilishe katiba yetu na tumpe hiyo nguvu.

Tulifanya makosa kupitisha katiba ile inayompa nguvu hafifu mwakilishi wa wanchama (Mangungu) kwenye vikao vya maamuzi.

Ikumbukwe kuwa, wanachama ndiyo wenye hisa nyingi kuliko mwekezaji, ila katiba inampa mwekezaji nguvu ya maamuzi, ni upuuzi.

Ova
 
Nimecheka mno! Japo umeandika vingi vyenye msingi ila aya yako ya kwanza imenivunja mbavu.
 
We ukiambiwa kuanzia Leo ondoka hapo kazini kwako na ni kazi uliyopambana kuipata basi unabeba vyako unaondoka sio!?
Pale ni kazini kwake na team mbona Ina mafanikio makubwa
1.Ngao ya hisani
2.Muungano cup
3.nafasi ya 3 kwenye league
Ni nyie tu mashabiki ndio mmeogopa kufanya parade mnaruhusu team yenye kombe Moja itambe mjini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…