Kumshitaki Mbunge Lusinde kwa matusi aliyomwaga Arumeru


wapi william malecela? william, hama CCM haraka son, and you know what? the jimbo will be yours to lose!
 
Reactions: FJM
Kwa maneno haya nafikiri CCM wamefanya evaluation na wameona hata wakifanya kwa matusi hawana cha kupoteza, kwani mtu makini haweza kumpa mtu kutukana hadharani wakati anajua anashindana kutafuta kura na nataka kuamini huyo bwana alitumwa iliaje atukane.Na pengine wamegundua watanzania wakiambia matusi ndo wanatoa kura.
 
Kama anajibu mapigo inamaana mtu akimuuwa ndugu yake nae atamuuwa badala ya kulipeleka hilo suala kwenye vyombo vya sheria.

kwanini vicent hakupeleka swala la mkapa ktk ukoo wao ili litatuliwe na yeye kumpigia moja kwa moja

ndio maana nimesema kuwa hizo ndizo kampeni zinazoendelea huko arumeru,tatizo tu ktk hili la Lusinde limepata wasemaje ila lile la wasila kutoka kwa mdee halijapata wasemaje,hapo ndipo utaona utofauti

 
Last edited by a moderator:
Poor Lusinde! Utafikiri alikuwa roboti.
 
By JacksonMichael
Ni kauli za kisiasa tu jamani, jadilini yalio na faida katika taifa lenu


Mkuu unashangaa nini wakati kila kukicha wapinzani wanaropoka mambo ya ajabu! sijaona cha kuwafanya mbowe a wenzake wapanic kwa kuwa ndio siasa za TZ kuattack personal kuliko sera.

Kilichonifurahisha hapa ni the way ulivyojibu.. Najua hata wewe muumini mzuri wa CCM yamekustua kiaci ambacho umejibu kwa unyonge sana.. Ndugu yangu kama viongozi wako wamekosea sio dhambi hata kidogo kuwakemea.. Alichokifanya Lucinde sio siasa.. Siasa haina matuci.. Kama wapinzani wanaropoka matuci haiwa-justify chama tawala nao watukane..!
 
Reactions: FJM
Ni kauli za kisiasa tu jamani, jadilini yalio na faida katika taifa lenu.

Mbona mmefungulia kesi kisa alisema Dr. Burian asipigiwe kura kwa sababu ni mwanamke tena hata hakufanya mabaya kama haya. JM unajua wazi Lusinde kawaharibia sana.
 

nashukuru sana mkuu kwa kunielewa

hayo ndiyo makosa ya kampeni za matusi kwa vyama vyote sio CDM wala sio CCM
 
Hapo hakuna kulea mashtaka ni lazima afunguliwe. Hili liko wazi na hata wakili mwanafunzi kesi hii anashinda. Kulea tabia hii ni hatari kwa taifa. Watoto utawakataza nini kama mjumbe wa halmashauri kuu hiyo ndo lugha yake. Hata CCM wenyewe kama wapo wachache wenye busara wanapaswa kuchukulia hatua za kinidhamu Lucinde.
Hii kanda itageuka mtaji mkubwa wa kuwachafua CCM kwa juhudi zao wenyewe.
 
Nimeona mulivyo biased nyinyi wachangiaji wote na ndiyo maana watu wanadai JF ni CDM. Wakati Mkapa anachafuliwa na mwendawazimu Vincent Nyerere muliona raha sasa CCM wameleta mwehu anayemzidi Vincent muna panic! Kweli mkuki kwa nguruwe....
 
Mimi naona hizi ni siasa tu za kawaida wala haina haja ya kumfungulia mashitaka!Kumbukeni kuwa hata mdee alimwita Wassira Sokwe hadharani hukohuko kwenye kampeni za Arumeru!!
 
Niitaka kusema kitu, lakini ngoja niache maana huyu Kilaza kajidhalilisha mwenyewe, team nzima ya campaign, chama chake, wapiga kura wake, serikari na wengine pia amefanya udhalilisha wa kijinsia. Sipati picha akina mama na akina dada waliokuwepo pale walivyo jisikia kwa matamshi yale. Huyu inabidi ashitakiwe na jamhuri.
 
Mkuu unashangaa nini wakati kila kukicha wapinzani wanaropoka mambo ya ajabu! sijaona cha kuwafanya mbowe a wenzake wapanic kwa kuwa ndio siasa za TZ kuattack personal kuliko sera.

Kuropoka mambo ya ajabu ni kuanika ufisadi ambao muda mwingi ulikuwa covered, sasa tuone maneno unayoona ya kawaida by Lusinde.
1. Mh Lema kaacha bwana, aliolewa mahabusu. (unajua mtu aliyeolewa hufanywa nini? Lusinde anaweza kuthibisha hilo?)
2. Mh Nyerere analiwa. (kwa lugha za vitarafa, neno kuliwa kwa alivotumia Lusinde ina maana a.na.la.wi.tiwa-aibu)
3. Mh Slaa anatembea kama kajinyea. Na ujinga mwingine mwingi alioongea utafikiri msukule au ndondocha.

Baya zaidi amuiga Idd Amin pale alipomwambia Mwl Nyerere (RIP) kuwa wapande ulingoni wapigane-aibu ccm.
 

Hivi huyu jamaha ana elimu ya kiwango gani?c.c.m wanajichafulia sana,hii inatakiwa iwe ni criminal case na si civil,nimesoma gazeti la mwananchi la leo,baadhi ya wazee wa Arumeru wanasikitishwa sana na baadhi ya wanasiasa kupanda majukwaani na kutoa matusi badala ya sera!huyu Lusinde anawakilisha aina ya wabunge wengi wa c.c.m walivyo,hv huyu ni kiongozi wa wananchi kweli?hao wananchi waliomchagua wanajisiaje juu ya kuwakilishwa na mtu mbumbu kama huyu?cha kusikitisha eti kuna mwana jf nae ana support these rubbish kwa minajiri ya eti ni maneno ya kisiasa!wapi huo u great thinker wa wana Jf?huyo mtu ana tofauti gani na huyo Lusinde ktk uwezo wa kufikiri?maneno ya kisiasa kumchafulia mtu thamani ya utu wake kwa jamihi yote??what a shame!
 
Nadhani Lusinde atakuwa na matatizo ya akili akapimwe. Kwa kitendo alichofanya anatakiwa kushughulikiwa. Kama hizo ndo sera za ccm hatufiki. naona wameamua kuweka hadharani tabia zao sasa
 
Ni kauli za kisiasa tu jamani, jadilini yalio na faida katika taifa lenu.

Mkuu, umenisikitisha sana. Kweli wewe ni m-Tz halisi. Maana silka ya wa-Tz ni muache tu bwana, si kauchafua mdomo wake!!!!
Kweli? Mtu anatoa matusi machafu kiasi kile, tena mbele ya watoto, tena wengine ndiyo kwanza wametoka shule hata majumbani kwao hawajafika (wako na magegi ya shule) wakiwa na hamu ya kusikia sera za wakubwa na wanasiasa wanakutana na ahh......

Inatia kichefuchefu, ashughulikiwe kisheria ili liwe fundisho kwa wengine.
 

Achan naye huyo utapoteza muda wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…