Kumtangaza Rais akiwa katika mavazi ya kijeshi katika utawala wa kiraia ni 'inferiority complex'

Kumtangaza Rais akiwa katika mavazi ya kijeshi katika utawala wa kiraia ni 'inferiority complex'

Behaviourist

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2016
Posts
39,926
Reaction score
95,626
Ndani ya miaka 60 ya uhuru chama cha CCM kimeshindwa kutatua changamoto ndogo kabisa ya maji na umeme halafu wiki hii kuelekea siku ya uhuru 09/12/2021 Rais wa utawala wa kiraia kutoka chama hichohicho anatangazwa kwenye mabango barabarani na mitaani akiwa amevaa mavazi ya kijeshi kuhadhaa uma kuwa ni Rais imara kutoka chama imara.Naona aibu mimi.

Kutangaza picha za Rais kwenye mabango akiwa katika mavazi ya kijeshi,katika utawala wa kiraia ambao Rais aliyepo ameingia madarakani kwa mujibu wa katiba ya kiraia ni inferiority complex na haimfanyi kuwa Rais bora na kwa watu wenye akili zao ni mambo ya aibu haya.

Rais bora anapimwa kwa kutatua changamoto ngumungumu kwa muda mfupi na kwa usahihi wake na wala siyo kwa kujitangaza akiwa kwenye mavazi ya kijeshi.Ninyi CCM Mnahitaji PhD kujua mambo madogo kabisa kama haya?

Ingependeza sana katika mabango hayo yanayoitangaza siku ya uhuru wetu viwekwe vivutio vya utalii badala ya Rais wa utawala wa kiraia alievalia mavazi ya kijeshi.

Halafu ninyi CCM ambao mmeshindwa kutatua changamoto ndogo kabisa ya maji na umeme ndani ya miaka 60 ya uhuru nani aliwaeleza kuwa sherehe za uhuru ni ‘birthday’ ya kiongozi aliyepo madarakani?

Kuelekea 09/12/2021 barabara zimepambwa na picha za Rais, hatuadhimishi siku yake ya kuzaliwa, tambueni hilo.

Kama mlitaka mitaa ipendeze kwa picha, kuna waasisi wa taifa hili pamoja na wapigania uhuru wa Taifa hili,wekeni picha zao barabarani.

Cssv.jpg
 
Mkuu, bado uko kwenye mavazi ya kijeshi tu?
Au ndiyo ile wenzetu wanasema 'the one who laughs last thinks slowly' 😂😂
Imagine unafanya maandalizi makubwa ya kusherekea miaka 60 ya uhuru ambapo ndani ya uhuru huo siyo tu kwamba umeshindwa kuwa huru bali umeshindwa kutatua changamoto ndogo kabisa ya maji,umeme na matundu ya vyoo halafu unavaa mavazi ya kijeshi katika utawala wa kiraia ili kutishia na kuhadhaa uma kuwa wewe ni Rais bora na imara kutoka chama bora🤡🤡🤡
 
Umeongea ya maana (maji na umeme). Ila umeonesha chuki kwa mama.

YESU NI BWANA NA MWOKOZI
 
Imagine unafanya maandalizi makubwa ya kusherekea miaka 60 ya uhuru ambapo ndani ya uhuru huo siyo tu kwamba umeshindwa kuwa huru bali umeshindwa kutatua changamoto ndogo kabisa ya maji, umeme na matundu ya vyoo halafu unavaa mavazi ya kijeshi katika utawala wa kiraia ili kutishia na kuhadhaa uma kuwa wewe ni Rais bora na imara kutoka chama bora🤡🤡🤡
Mkuu, tuongelee tu miaka 60 ya uhuru, masuala ya maji, umeme, hospitali, barabara, nk, lakini hayana uhusiano wowote na mavazi ya kijeshi.

Kuvaa kiraia hakumaanishi maendeleo in any way!
 
Mkuu, tuongelee tu miaka 60 ya uhuru, masuala ya maji, umeme, hospitali, barabara, nk, lakini hayana uhusiano wowote na mavazi ya kijeshi.
Kuvaa kiraia hakumaanishi maendeleo in any way!
Haujaelewa nilichoandika.Hakuna mahali niliposema kuwa Rais anapaswa kuvaa kiraia ili nchi ipate maji na umeme.
 
Mkuu, tuongelee tu miaka 60 ya uhuru, masuala ya maji, umeme, hospitali, barabara, nk, lakini hayana uhusiano wowote na mavazi ya kijeshi.
Kuvaa kiraia hakumaanishi maendeleo in any way!
Tujibie hoja sio mtoa hoja,ndio maana tunatakiwa tusome to understand not to ask questions,mtoa hoja kaelezea maudhui ya hoja yake sasa mimi na wewe tujitahidi kusoma ili kuielewa nini lengo la hoja!
 
Ushamba huu uliasisiwa na stoni. Mi nadhani mavazi yale ni ya askari aliyefuzu mafunzo ya kijeshi. Rais wa Tzani ni amirijeshi mkuu, lakini sio askari hivyo hapaswi kuvaa ile sare.

Lakini sehemu kubwa ya waTz wameshapandikizwa ujinga, no wonder unaambiwa mradi huu tunajenga kwa 'pesa zetu za ndani' kumbe ni mkopo. Eti ukishakopa pesa inakuwa ni yako ya ndani. Sijui ya nje ni ipi!
 
Wakati wanajeshi walioshika madaraka ya urais kama Al Sisi wa misri wakikomaa kuvaa suti ili waonekane kwa udi na uvumba kama viongozi wa kiraia, hangaya anang'ang'ana kuvaa kombati ili aonekane kama kiongozi wa kijeshi, ngachoka mimi.
 
Kikwete hakujinasibisha uanajeshi wake kwa mavazi "yale"!Yametukutani Leo hii?Ajabu!Tupambane na maadui watatu.Ujinga,umaskini na nini sijui!
 
''Ninyi CCM Mnahitaji PhD kujua mambo madogo kabisa kama haya?''

Wanazihitaji zile za akina MUSUKUMA
 
Back
Top Bottom