Kumtangaza Rais akiwa katika mavazi ya kijeshi katika utawala wa kiraia ni 'inferiority complex'

Kumtangaza Rais akiwa katika mavazi ya kijeshi katika utawala wa kiraia ni 'inferiority complex'

Hivi tulipata Uhuru kwa Mtutu wa Bunduki? Mbona CCM wanakosa ufahamu kabisa, au labda wanatishana wenyewe humo kwenye chama. Nani asiyefahamu kuwa Samia ni Rais na Amiri Jeshi Mkuu? Kama wanapesa za kuchezea bora wangeweka zile picha za kihistoria wakati Mwingereza anatukabidhi Nchi.
 
Ingependeza sana katika mabango hayo yanayoitangaza siku ya uhuru wetu viwekwe vivutio vya utalii badala ya Rais wa utawala wa kiraia alievalia mavazi ya kijeshi.
kwani si tulishakubaliana rais nae ni kivutio sasa mapovu ya nini tena .. sawa basi tutamweka mbowe na lisu..
 
Sawa, sasa dawa yenu ni katiba mpya tu.
Wananchi ndio mamlaka ya mwisho ya kuamua uendeshaji wa nchi.

Kama wananchi ambao ndiyo wenye nchi wanataka katiba mpya ni nani wa kuzuia?
 
Kumbe tuna KATIBA pendekezwa ipo kabisa ambayo stage iliyokuwa imebakia ilikuwa ni kwenda kwa kwa wananchi kuipigia kura tu na kisha iwe tayari.

CCM mnaogopa nini? hebu ileteni tuipigie kura tumalize mchezo.
 
Machinery ya Serikali bado ni ya marehemu Magufuli. Government machinery ya Serikali ya Magufuli ilijengwa na watu wengi ambao ni primitive.

Ni watu wanaoamini kuwa kila kitu kinahitaji nguvu. Huku wakishindwa kutambua kuwa kitu adimu ni akili, nguvu, hata nyati anazo, na hazijawahi kumfanya nyati wa leo awe bora zaidi ya nyati wa karne iliyopita.
 
Mkuu, bado uko kwenye mavazi ya kijeshi tu?

Au ndiyo ile wenzetu wanasema 'the one who laughs last thinks slowly' 😂😂
Ukweli mchungu, unajichekesha kicheko hakiji, inakuja hasira, unatokwa mapovu.
Vumilia au mjibu kwa hoja : miaka60 ya utawala wa MaCCM maji na umeme tu vimewashinda .
Uimara wa kutesa, kupiga risasi kufunga jela na kuua wapinzani tu..?!
 
Yeye ndiye alionyesha chuki kwa demokrasia yetu.Halafu neno Mama lina heshima yake,koma kulitumia kwa watu wa hovyo kama huyu anaeonyesha chuki katika demokrasia yetuView attachment 2035428
Magu ndiye aliyeharibu hii nchi. Hata kuingamiza mifumo yote ya nchi. Angalia kwa mfano ishu ya separation of powers alivyoi paralyse! Kipindi cha kampeni Samia alikuwa bendera fuata upepo tu.


JESUS IS LORD!
 
Ndani ya miaka 60 ya uhuru chama cha CCM kimeshindwa kutatua changamoto ndogo kabisa ya maji na umeme halafu wiki hii kuelekea siku ya uhuru 09/12/2021 Rais wa utawala wa kiraia kutoka chama hichohicho anatangazwa kwenye mabango barabarani na mitaani akiwa amevaa mavazi ya kijeshi kuhadhaa uma kuwa ni Rais imara kutoka chama imara.Naona aibu mimi.

Kutangaza picha za Rais kwenye mabango akiwa katika mavazi ya kijeshi,katika utawala wa kiraia ambao Rais aliyepo ameingia madarakani kwa mujibu wa katiba ya kiraia ni inferiority complex na haimfanyi kuwa Rais bora na kwa watu wenye akili zao ni mambo ya aibu haya.

Rais bora anapimwa kwa kutatua changamoto ngumungumu kwa muda mfupi na kwa usahihi wake na wala siyo kwa kujitangaza akiwa kwenye mavazi ya kijeshi.Ninyi CCM Mnahitaji PhD kujua mambo madogo kabisa kama haya?

Ingependeza sana katika mabango hayo yanayoitangaza siku ya uhuru wetu viwekwe vivutio vya utalii badala ya Rais wa utawala wa kiraia alievalia mavazi ya kijeshi.

Halafu ninyi CCM ambao mmeshindwa kutatua changamoto ndogo kabisa ya maji na umeme ndani ya miaka 60 ya uhuru nani aliwaeleza kuwa sherehe za uhuru ni ‘birthday’ ya kiongozi aliyepo madarakani?

Kuelekea 09/12/2021 barabara zimepambwa na picha za Rais, hatuadhimishi siku yake ya kuzaliwa, tambueni hilo.

Kama mlitaka mitaa ipendeze kwa picha, kuna waasisi wa taifa hili pamoja na wapigania uhuru wa Taifa hili,wekeni picha zao barabarani.

Hiyo picha kajilazimisha mana awamu ya 5 ni bongo movie tu,hawana jipya
 
Back
Top Bottom