Kumpa maziwa kwa chupa
Kama unamlisha mwanao kwa chupa, hakikisha umechanganya maziwa hayo sawasawa ili mtoto apate malisho yanayofaa. Pia zungumza na daktari wako wakati utaanza kumlisha mwanao mchanganyiko (familia) ulio na iro.
Vipi, lini na nini unalisha mtoto wako ni muhimu. Kila kitu kutoka aina yamchanganyika, joto la mchanganyiko na aina ya chupa unazotumia hujalisha. Unaweza ujumbe huu kutoka kwa daktari wako au kliniki.
Hakikisha umemuliza daktari wako kuhusu utakapoanzia kumpa mtoto wako chakula kikavu. Hata kama mtoto wako ataanza kujaribu kukifikia/kushika kijiko, ni vizuri umuulize daktari kwanza.
Kumuosha mwanao
Ni vizuri kumweka mwanao safi na mkavu km. kumgeuzia nappy mara kwa mara. Hakikisha kuosha napi vizuri baada ya kuchafuliwa. Uso, sehemu za siri na mikono ya mtoto wako zinafaa kuoshwa kwa sifongo (sponge) kila siku. Unafaa kumwosha mwili wote baada ya siki mbili au tatu. Watoto wachaga bado wana ugue wa kitovu. Unapaswa kumwosha kwa sifongo hadi wakati ugue huu utakatika kabisa. Uoshe ugue huu kwa uangalifu mwingi na utumie mvinyo (spirit) wa upasuaji uliotiwa kwa kitakia cha katani. Usivute ugue wa kitovu unapaswa kujiangusha mwenyewe.
Usije ukamwacha mwanao ndani ya karai la kuogea. Watoto wanaweza kufa maji yaliyofika inchi mbili tu. Unapomwosha, hakikisha una vifaa vyaa kumwoshea, sabuni na kadhalika ili usimwache mwanao kwa karai la kuogea bila wakumwangalia unapoenda kuvichukua.
Maji yaliyo moto sana huenda yakamchoma mwanao. Kama unakifaa cha kupasha maji moto weak kwa joto la 49oC . Pima joto la maji kwa kiko cha mkono wako. Kabla hujamweka mwanao ndani na uhakikishe maji ni vuguvugu
Kumvisha nguo
Mvishe mwanao na kunjo moja zaidi wakati yu mchanga na jiepushe na kumwacha mwanao kuliko na baridi kwa muda mrefu.
Watoto hupoteza joto haraka sana, hivyo hakikisha umewafunika kichwa na miguu
Wakati kuna joto jingi, mweke mwanao mbali na jua. Linda mwanao kna nguo za mikono-mirefu(long-sleeve), nyepesi na umweke kivulini
Nguo zote mpya zinafaa kufuliwa kabla ya kutumia
Kuota meno
Mtoto wako atakapofikisha miezi sita, ataanza kuota meno. Watoto wengine huanza kkuudhika kwani huumia kabla meno hayajatokea kwa ufizi. Watoto wengi humwaga mate sana na hutaka kutafunatafuna vitu. Wakati mwingine watoto hutapika au kuhara wakiota meno.
Kwa kawaida kuota meno hakufanyi mtoto kupandwa na joto. Kama mtoto wako atapata joto. Kama mtoto wako atapata joto, yaweza kuwa jambo lingine. Hakikisha umemwona daktari wa watoto.
Mawaidha wakati mtoto anaota meno
Wakati wa kulala, weka kitambaa safi chini ya kichwa cha mwanao ambapo ule utamwagika. Unaweza kibadilisha kitambaa hichi kitakapo loweka ute.
Mpatie mtoto kitu cha kutafuna ambacho hakitamdhuru. Usimpatie kitu kidogo sana kwani anaweza kukimeza. Unaweza kumpatia vidunde vya mpira visivyokuwa na majimaji ndani kwani vyaweza kupasuka. Unaweza kumpa kijiko cha mpira au kitambaa safi.
Usifungilie kidunde cha kutafuna kwa shingo ya mwanao. Kinaweza kushikwa na kummyonga.
Kuna dawa nyingi dukani za kupiunguza maumivu wakati mwanao anaota meno. Hata hivyo, mwone daktari wa watoto kabla jujampa mwanao dawa yoyote
Baada ya mwanao kuota meno hakikisha unayatunza