Kumuota mtu ambaye ameshafariki inakuwa na maana gani?

Kumuota mtu ambaye ameshafariki inakuwa na maana gani?

Nashukuru mkuu lakini mimi siamini kwenye kuombea wafu
Kwa mimi huwa nikiwaota wapendwa waliotangulia basi huwa nawatolea sadaka
Ila ipo kwenye Imani zaidi
Huenda na hili utalikataa lakini ni vizuri kuwakumbuka kwa namna hii pindi wanapotuijia kwenye ndoto
I miss my Dad
 
Wakati nadhani namuota mtu kwasababu nipo nyumbani kwake, nikaamia dodoma, naona bado ndoto zinarudi,
Kwa mimi huwa nikiwaota wapendwa waliotangulia basi huwa nawatolea sadaka
Ila ipo kwenye Imani zaidi
Huenda na hili utalikataa lakini ni vizuri kuwakumbuka kwa namna hii pindi wanapotuijia kwenye ndoto
I miss my Dad
 
Kama nimeota tukiwa kwenye mambo ya kawaida tu mimi uwa nachukulia kuwa ni wakati mwingine mzuri nilioupata wa kukaa pamoja na wapendwa wangu. Mradi isiwe ndoto yenye matukio ya kusikitisha.
 
Hii hali imenisumbua sana,ila surely ni mizimu ya familia ,+(utakuwa mchaga bila shaka) au kwenye asili ya mama yako ni watambikaji.hyo siyo hali nzuri kwa kuwa hizo Roho Huwa zinauwezo wa kuzuia baadhi ya mafanikio mpaka ufanye baadhi ya ritual ya kuridhisha mizimu husika na utakuwa umeifungulia milango rasmi kwenye uzao wako.suluhisho ni maombi ya kutosha,nilikuwa nalega nalega kwenye maombi ila nilipokaza sioti Tena ndoto za wafu.
 
Mara Ninaporudi nyumbani nilipozaliwa huwa namuota sana marehemu mama yangu 🤔

Kwa namna anavyokuja ndotoni ni mtu mpole sana, mkimya,huniangalia na kutabasamu, mara nyingi huwa namuota yupo jikoni au chumbani kwake amepumzika, maana hawezi kufanya tena kazi ngumu, labda kupika tu pekee.
Mara nyingi huja kututembelea tukiwa family nzima au wanaukoo baadhi baadhi

Muda mwingine, ni kama hunionya vitu ambayo Ata sikumbuki,

👉Nawaza huenda ni kwasababu nikirudi nyumbani masaa Machache kabla sijalala kila siku huwa nachukua dk tano hadi Lisaa kumfikiria, alikuwa kama Nyerere na aina Ile ya watu ambao Ata wakifa Yan matendo yao unajikuta unayaishi Kila siku, au lazima utamtolea mfano unakumbuka fulani alifanya ABC wakati wa uhai wake.

Lakini pia, huwa nasoma vitabu vyake viwili alivyoacha ili kujichotea hekima na madini ,haswa nyakati za usku nikiwa nimetulia

👉Karibuni, wakuu kwa michango na mitazamo, Aidha ni physics ndo inafanya kazi au ni 😅ndio wafu hutembelea watu ndotoni
Hii isikupe shida,, wewe ni miongoni mwa mamilioni ya watu wanaowaota wapendwa wao waliotangulia....ila umenishangaza uliposema huwa huombei wafu...kwa maana hiyo wewe sio muislam/mkristo?
 
Wakati nadhani namuota mtu kwasababu nipo nyumbani kwake, nikaamia dodoma, naona bado ndoto zinarudi,
Nafsi zinaonana na zinaongea
Kuna mengi binaadamu hatuyajui ila yapo sana
Muombee na pia peleka chochote kwa yatima au hata kwa wagonjwa
Sadaka ni muhimu sana
 
Hii isikupe shida,, wewe ni miongoni mwa mamilioni ya watu wanaowaota wapendwa wao waliotangulia....ila umenishangaza uliposema huwa huombei wafu...kwa maana hiyo wewe sio muislam/mkristo?
Kutokana na huo mstari kutoka katika maandiko Sasa kuna haja gani ya kuombea mfu
 

Attachments

  • Screenshot_20250116_185109.jpg
    Screenshot_20250116_185109.jpg
    55.8 KB · Views: 3
Nafsi zinaonana na zinaongea
Kuna mengi binaadamu hatuyajui ila yapo sana
Muombee na pia peleka chochote kwa yatima au hata kwa wagonjwa
Sadaka ni muhimu sana
Samahani, mkuu naomba kuhoji
Mimi japo Sina utaratibu huo wa kupeleka vitu kwa watoto yatima au wagonjwa but I don't the reason behind matajiri wengi hupeleka msaada kwa hizo grupu mbili ulizotaja

Je ni CSR (giving back to community) wanafanya, ama ni kusaka fame? Na je, kuna mwanangu yeye anasemaga ukitaka pesa zako ziongezeke peleka kwa wagonjwa ama yatima?
Inamaana Sasa msingi wa kupata kusaidia wa hitaji kumbe ni kutaka kuongeza utajiri nasivinginevyo
 
Samahani, mkuu naomba kuhoji
Mimi japo Sina utaratibu huo wa kupeleka vitu kwa watoto yatima au wagonjwa but I don't the reason behind matajiri wengi hupeleka msaada kwa hizo grupu mbili ulizotaja

Je ni CSR (giving back to community) wanafanya, ama ni kusaka fame? Na je, kuna mwanangu yeye anasemaga ukitaka pesa zako ziongezeke peleka kwa wagonjwa ama yatima?
Inamaana Sasa msingi wa kupata kusaidia wa hitaji kumbe ni kutaka kuongeza utajiri nasivinginevyo
Sio kweli mkuu, kupeleka au kutoa msaada kwa wanaohitaji sio kutafuta Kiki wala kujionyesha kwani wanaojionyesha wakati wa kutoa sio sahihi kwa kujipiga mapicha
Na sio kila anaetoa anategemea utajiri uongezeke hapana
Kutoa sio utajiri
Huwa nashangaa watu wanaona wa kutoa ni matajiri tu

Na sadaka (charity) sio lazima mali mkuu hata tabasamu lako ni sadaka pia kwa waislam ila dini zingine au wengine sijui

Mama yangu miaka mingi sana alikuwa na tabia ya kwenda hospitali mapema asubuhi akiwa amebeba hata mikate na kwenda kuwasalimu na kuwafariji wagonjwa kwa kuwapa pole
Hana utajiri wa hela bali wa moyo
 
Kuota mtu aliyekufa mara kwa mara, ni roho ya mauti inakufatilia hapo kifo kpo karibu, Sali sana Mungu akuepushe
 
Back
Top Bottom