Kumzoesha Mtoto hela ni dhambi?

Kumzoesha Mtoto hela ni dhambi?

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,611
Hii mada niliikuta sehemu imezua mjadala mkali sana baina ya mtoto (mwanafunzi) na mama yake wakati wakifanya manunuzi ya stationery za kwenda shule Januari hii.

Mama anashikilia kwamba hela ni hatari kwa mtoto (hasa wa bweni) kwamba yeye mama enzi zake kama mwanafunzi hakupewa hela ambazo mtoto wake anadai apewe leo.

Mtoto anashikilia kwamba bila kupewa hela za kumtosha basi asitegemee atasoma masomo ya mchepuo wanaotaka wazazi wake wa ECA ili awe Mhasibu.

Mtoto anaamini kupewa hela za kukidhi matakwa yake siyo dhambi bali dhambi ni kupewa hela kidogo maana akipewa za kumtosha basi hata ukubwani atazitafuta kwa bidii maana atakuwa ameishafundishwa utamu wake.

Akipewa kidogo au kunyimwanyimwa basi ukubwani hatofanya bidii kutafuta hela maana atakuwa hajazizoea (ataziogopa kwamba ni hatari) na kwamba wazazi wake wasipokuja kupata hela toka kwake wasije kumlaumu.

Kumzoesha mtoto hela ni dhambi?

Nini ushauri wako kwa hii familia.

Taswira kwa hisani ya google.

1641897793250.png
 
Hela mzee zina kichwa na kichwa
Kuna vichwa sio vya kukaa na fedha kabisa
Kuna mtu akipata fedha anachanganyikiwa kabisa ila kuna vichwa vinakaa na fedha ya maana na wala huwezi hata kuvijua
In fact mwangalie kwa umakini mwanao utamwelewa tu katika haya ninayokwambia na utakuja kunishukuru
 
Hii mada niliikuta sehemu imezua mjadala mkali sana baina ya mtoto (mwanafunzi) na mama yake wakati wakifanya manunuzi ya stationery za kwenda shule Januari hii.

Mama anashikilia kwamba hela ni hatari kwa mtoto (hasa wa bweni) kwamba yeye mama enzi zake kama mwanafunzi hakupewa hela ambazo mtoto wake anadai apewe leo.

Mtoto anashikilia kwamba bila kupewa hela za kumtosha basi asitegemee atasoma masomo ya mchepuo wanaotaka wazazi wake wa ECA ili awe Mhasibu.

Mtoto anaamini kupewa hela za kukidhi matakwa yake siyo dhambi bali dhambi ni kupewa hela kidogo maana akipewa za kumtosha basi hata ukubwani atazitafuta kwa bidii maana atakuwa ameishafundishwa utamu wake.

Akipewa kidogo au kunyimwanyimwa basi ukubwani hatofanya bidii kutafuta hela maana atakuwa hajazizoea (ataziogopa kwamba ni hatari) na kwamba wazazi wake wasipokuja kupata hela toka kwake wasije kumlaumu.

Kumzoesha mtoto hela ni dhambi?

Nini ushauri wako kwa hii familia.

Taswira kwa hisani ya google.

View attachment 2076967
Acha ubahili mpe mtoto pesa amuhonge baby wake
 
Hela mzee zina kichwa na kichwa
Kuna vichwa sio vya kukaa na fedha kabisa
Kuna mtu akipata fedha anachanganyikiwa kabisa ila kuna vichwa vinakaa na fedha ya maana na wala huwezi hata kuvijua
In fact mwangalie kwa umakini mwanao utamwelewa tu katika haya ninayokwambia na utakuja kunishukuru
Sisi wakati tunakuwa tuliambiwa "weweee... usipende ela ni hatari"

Nilipokuja mjini nikakuta Mchaga, Msomali na Mhindi wanawaachia watoto wao duka kutwa nzima na siku wanarudi shule wanalipwa posho kwa kazi ya kuuza maduka ya wazazi wao.

Ndipo nikajiuliza je, mbona sisi hatukuruhusiwa kuuza biashara za wazazi wetu? na kwamba tulichokuwa tukiambiwa ni "ogopa ela ni hatari" kwahiyo tumekuwa tukijuwa kumbe ela ni hatari!!!
 
Back
Top Bottom