Kuna abiria kaleta zogo hapa anasema bila wao kuzima nyimbo za kidunia atashuka na wala nauli hataki kurudishiwa na wataiona hasira ya Mungu

Nyimbo zenyewe za kishenzi , takataka hizi ,hao mafala wanaimba matusi na lugha chafu ,na mpo kama maombi mnasikiliza na watoto wenu bila aibu , halafu mnalalamika mmomonyoko wa maadili ,
Huyo jamaa na muunga mkono , Watz wapumbavu sana
 
Kuna mambo mengine unaona kabisa watu mnajitafutia misongo ya mawazo; yaani huyo Mungu anayetaka muda wote umuwaze yeye tu yaani hajatoa maagizo ya kufanya vingine ?
 
Hahaha Kwani mungu anapenda kwaya bongofleva na anaelewa kiswahele hadi awe na hasira na mwenye mziki wake na kachagua midundo apendayo mwenyewe?
 
Mwamba ameshuka kabisa hataki ujinga😂, ame-fume sana, na wala hajaomba refund

Abiria wengine wamemzomea ashuke tu kwa maana anajiona yeye mtakatifu kuzidi wote.

Vp kwa upande wako uaonaje hii ishu na pia ungei solve vp?
Utakatifu au ni upumbavu? "usijihesabie haki..." walokole tunakwama wapi Wakuu?

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Yupo sahihi. Kuna mama mtu mzima hivi aliniambia ndani ya bus kuwa sisi vijana tuna nafasi ya kufanya mabadiliko kwa bus za route ndefu kwenda mikoani kuonyesha video za maigizo zenye maudhui ya mambo ya watu wakubwa wakati ndani ya bus kuna abiria wanasafiri na watoto, wazazi au wakwe wao, na pengine wamekaa siti moja au zinazokaribiana
 
Ukiachana na mambo ya dini ila kiukweli kusafiri na mabasi ya mikoani inakera sana na hizo miziki na video zao

Nimewahi kupanda Tahmeed la kwenda Mombasa njia nzima tumewekewa kaswida na mawaidha
Ukipanda mabasi njia ya Arusha njia nzima ni nyimbo za injili
Ukipanda mabasi ya kwenda njia ya Mwanza njia nzima ni filamu za majuta na mkojani
Ukipanda mabasi njia ya Mbeya njia nzima ni zile movies zimetafsiriwa kiswahili

Hii ni KERO kwakweli sio kila mtu anataka kusikiliza au kuangalia haya mavitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…