Kuna aina ya Ukristo ambayo ni ushetani

Anasingizia Ukristo na ulokole je angekuwa mcheza Ngoma au mama shughuli kila kukicha kwakijumbe vipi hapo? Wanafiki tu hawa.
ni mpumbavu sana kuponda maisha ya wokovu ya mke wake. Ashukuru Mungu mke wake ameokoka na kuna siku yaja atakuja ku appieciate maisha ya mke wake ya wokovu kwa kujutia na kutubu kuwa alimsema vibaya na hatimaye kuungana naye katika hiyo imani anayoiponda kwa kuiita ushetani wakati yeye mwenyewe ni mtumishi wa shetani. Je angependa mke wake awe malaya fulani mwenye waume wengi na mchawi? Ashike adabu kwa mke wake
 
👆🏾👍🏽👏🏾
 
Una uhakika unachoongea au haujaexperience unaongea kwa hisia........?
 
Kale kawimbo kakufikie popote ulipo....." Huyooooooo ni chaguoooooo lakoooooooo ".....
 
NIKUOE POLE NI SEME KWAMBA ULOKOLE SIO UJINGA WALA USHAMBA PUNGUZA MIHEMKO, HAPO TATIZO HALIPO KWENYE WOKOVU TATIZO LIPO KWA MKEO NI MJINGA HAELEWI ANACHO KIFANYA ...MAANDIKO YANASEMA HIVI....
“Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

— 1 Timotheo 5:8
KAMA MKEO HAWAJALI WA NYUMBANI MWAKE HUYO NI MTU MBAYA KULIKO MPAGANI, SASA SHIDA SIO ULOKOLE HAPO TATIZO NI LA MKEO TUOMBE RADHI WALOKOLE MKEO HASOMI NENO ANAHITAJI MSAADA WA KARIBU
 
Hapa tatizo ni wewe bro sio yeye. Jitahd kuwa Mwanaume Mzee. Kuna muda lazima mtu achague ndoa yake au matakwa yake. Lazima ijulikane mipaka ya kila kitu. Kuwa na kauli ya mwisho basi na iwe basi.
 
Mimi nichangie tu hapo kwenye kipengele cha kuvujishiwa siri na mtu wako wa jikoni...(bila shaka hgirl..na mnaelewana sana...), hapo uwe makini sana na hizo taarifa.Tango pori on flick..
 
Umesema ukweli mtumpu,hii tabia ya kuwarubuni waumini imeharibu ndoa nyingi na mwisho wa siku waliuoumia ni watoto.Inafikia stage mke hakai nyumbani kila siku maombi hadi usiku hajui shida za nyumbani yeye na Mchungaji tu,inafikia hatua baadhi ya wake za watu kupewa zamu za kumpikia chakula mchungaji wakati kwake hajui wamekula nini.Kifupi inasikitisha na mwisho wa siku ndoa nyingi zinayumba kutokana na baadhi ya Wanawake kukosa busara ya kutenganisha muda wa mambo ya Kanisa na Familia.
 
Asa baada ya kuchukua actions analia lia tu inamaana yeye ndo mwenye shida
Ni order kwamba kuanzia sasa sitaki hiki na hiki basi,narudia tatizo sio ulokole

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Kwa maana hiyo kutokana na maelezo yake, solution ni kumtimua...,kuna wanawake wengine haswa hao walokole hata umwambie kwa kutumia nn hasikii.
 
Mimi binafsi makanisa ya kilokole nayadharau kupita maelezo yani mtu anaamka njaa imemkamata anaanzisha kakanisa uchwara mwisho wa siku wachungaji feki hawa wanaanza kuwarubuni wake zetu hapo kamanda chukua hatua kali sana mpige stop kwenda kwa uyo mchungaji la sivyo ndoa itakufa chap
 
Haswaa kuna mambo mengi hao mazuzu hawajui hua wanajiona
wanamjua sana Mungu kumbe zero,
mfano imani ni kuchukua hatua ya kile unachoamini,
ukifikiri vibaya utapata matokeo ya uharibifu na
ukifikiri vema utapata matokeo chanya
walokole wapo busy kupambana na Ibilisi na ajent zake
badala ya kua busy na Mungu awape pumziko na ndio maana
wamechapika kiroho kimwili na kiakili
hawajui kanuni za ulimwengu wa roho kwamba
hupewi unachotaka ila unapewa unachoamini mfano
unataka utajiri na moyoni unajiona maskini sahau kupokea maana
mwenye nacho huzidishiwa na asiye nacho hata kidogo alichonacho hutwaliwa
Mungu huangalia moyo wa mtu ulivyo na anakupa kwa kipimo ukitakacho na zaidi
ukiwaza vema anakuzidishia ili kutimiza mapenzi na ufalme wake
ila ukiwaza vibaya hiyo kazi ni shetani anaingia on duty kuhakikisha anakupa sawa sawa na hitaji lako!
Walokole mawazo yao ni hasi muda wote kitu kidogo
tu utasikia shetani kajiinua tufanye maombi ya vita ,wanampa shetani kiki za kishamba badala ya kumpa Mungu utukufu
fakeni!
Sandali Ali
 
binafsi naishi kwa namna hiyo pia, na nimebarikiwa sana kwasababu hiyo, na hakuna mtu ambaye huwa anasimama kupambana na mimi kwa chochote lazima ashindwe kwasababu mimi sipigani peke yangu, ninapiganiwa na Mungu. kama haujui, Mungu sio fukara, Mungu sio maskini, ila anahitaji ushirikiano nasi just kuonyesha kwamba tunampenda na kumtiii, that's all he needs. ndio maana ipo sheria ya kiroho kabisa (sio sheria kama za wasabato, ila ni spiritual law) ambayo kwa kitu chochote unachozalisha, kabla haujakula matunda yake, yale mavuno ya mwanzo unatakiwa kumpa Mungu, na sio lazima umpe yoooote, hapana ni vile moyo utakavyoamua ila cha muhimu usile kabla Mungu hajala, unampa Mungu ale kwanza ndio wewe ule. (INAITWA MALIMBUKO), kwa namna hiyo, nimeshuhudia kwa maisha yangu, kila project ninayofanya hivyo huwa inakuwa bora kuliko chochote.

kitu kingine, fungu la kumi limekuwa likipingwa na wengi sana hasa siku hizi za manabii wa uongo, mimi pia nilishawahi kuwa convinced sana nao hasa wale wanaopiga, lakini cha ajabu nikamsikiliza mtu wa Mungu mmoja hivi aliyesema na yeye alishawahi kuhubiriwa sana moyoni kwamba fungu la kumi sio la nyakati hizi, ni la nyakati za kale, LAKINI AKASEMA, AKAAMUA AJARIBU MAISHA YA FUNGU LA KUMI NA YASIYO YA FUNGU LA KUMI YANAFANANAJE? Akaja kugundua kwamba, miezi ile ametoa fungu la kumi anapokea faida na baraka kuliko miezi ile ameiba fungu la kumbi ambayo matatizo mengi hutafuta mtaji na pesa zake, conclusion yake ikawa ni kwamba fungu la kumi ni lazima kwa kumtii Mungu na bado ni spiritual law. hata Yesu alisema, mafarisayo wamekazania kutoa fungu la kumi na kusahau mambo ya msingi (utakatifu) akawaambia mnatakiwa kuushika utakatifu, "na hayo pia (akimaanisha fungu la kumi) msiache". hivyo Yesu mwenyewe alisema hata pamoja na kufuata mambo mengine ya kimungu hatutakiwi kuacha kutoa fungu la kumi.

Mimi pia nilifanya utafiti kwa experiencwe yangu kabisa, na ninashuhudia kwa moyo wangu wote wala sisemi uongo, nimethibitisha kuwa fungu la kumi ni la lazima kama unataka kubarikiwa na Mungu. Roho Mtakatifu pia ananishuhudia kila siku kwamba fungu la kumi ni lazima na usipotoa ni dhambi kwasababu unakaidi sheria ya rohoni ya Mungu aliyoitoa kitabu cha Malaki. kuna project moja nilihangaika nayo sana miaka 5, ikasimama, sikutoa limbuko, wala fungu la kumi, ile project niliishia tu kupata mtaji nilioanzishia, faida yote ililiwa na magonjwa, ndugu, wezi na mambo kibao.

mwaka 2019 nikaanzisha project tena kama ile ile ya awali, maana ile ya awali ilikufa nikasahau kabisa shughuli hizo. nikauza, mauzo yangu ya awali, tena yalikuwa laki moja tu, nikaipeleka church kama sadaka ya malimbuko kabla sijaanza kula matunda ya ile project. kilichofuata, products zangu au niseme shughuli zangu zilianza kubarikiwa na hakuna ambaye huwa anasimama dhidi yangu, ni kama kuna kaupako/kibali fulani, wengi wanaanzisha project kama yangu na hata wakiweka karibu yangu wanaondoka wenyewe, na situmii uchawi wala dawa.

Mungu ameahidi tukitoa fungu la kumi yeye atamkemea alaye na kuharibu mazao/shughuli zetu. na pia kwa habari ya malimbuko, ukimpa Mungu ale kwanza faida ya kile ulichoanzisha nakuhakikishia along that business Mungu ataenda pamoja na wewe, atapambana na wale wanaokuhujumu na wewe binafsi hautapambana bali Mungu atakupambania. unakuwa umemheshimu Mungu, umemuweka yeye kwanza na wewe ufuate, hivyo Mungu atakutangulia kwenye shughuli zako zote na kila unachokifanya, nimethibitisha hili na ninawashauri wote msisikilize maneno ya manabii wa uongo na wapotoshaji wanaotumiwa na shetani. pia jueni kumtii Mungu ni uamzi wa binafsi, chagueni kufuata au kutofuata, kwasababu kwa kila uamuzi utakaoutumia utafuatana na matokeo ya kule ulikochagua.

nilikuwa nashangaa zamani kwanini Mungu ameandika kuwa, "onjeni muone kwamba Bwana yu mwema, heri mtu yule atakayemtumaini", kumbe Mungu anajua wanadamu ni wabishi na wanapenda kufuata upotoshaji wa mashetani, ndio maana anasema jaribuni kufanya hata haya kwa mfano, jaribuni kwa maisha yenu kutoa fungu la kumi na kutoa limbuko, halafu muone kama Bwana hatakuwa mwema kwenu. nina uhakika Mungu ni wa kuaminiwa, na atajidhihirisha hata wewe uliyeandika hapa utakuja kuwa balozi wa wenzako. jaribu tu, ukiona kweli haujaona matokeo chanya, basi labda atakuwa sio huyu Mungu ninayemwamini mimi na ambaye nimemwona maishani mwangu.

NB: fungu la kumi sio la kutoa kila sehemu, unaweza kutoa kwa manabii wa uongo wanaotumiwa na shetani, ikawa haijaenda kwa Mungu imeenda kwa mashetani, toa sehemu ambako kuna Mungu wa kweli, sehemu wanayoamini wokovu wa Yesu Kristo, sio sehemu wanayoabudu masanamu na maria, na sio sehemu wanayotumia mafuta na chumvi badala ya kutumia Jina la Yesu. toa sehemu ambayo wameokoka na wewe uokoke ndio matokeo yote hayo utayaona. all in all, utii ni wa muhimu kuliko dhabihu, na kwenda kwako kanisani, tii Neno la Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…