Kuna faida gani kusafiri daraja la kwanza au VIP kwenye ndege?

Kuna faida gani kusafiri daraja la kwanza au VIP kwenye ndege?

Wakuu salama?

Naombeni mnitoe "matongotongo"

Abiria wa daraja la kwanza au VIP kwenye ndege anatofautianaje na wa madaraja ya kawaida?

Nawasilisha🙏
Kupanda daladala kwenda kariakoo na mimi nikitumia Landcruiser V8 New Model wote tunafika kariakoo! Ndege hiyo hiyo ila uwezi kaa compartment moja na watu wakubwa wenye ukwasi mkubwa na viongozi wakubwa au marais
 
1. Viti vya daraja la kwanza vina nafasi ya kutosha, pia unaweza kuvilaza unavyotaka pindi unapotaka kulala au kupumzika.
2. Huduma za ndani ya ndege ni ya kiwango cha juu tofauti na daraja la kawaida. Mfano, abiria wanaosafiri daraja la kwanza wanapewa mvinjo tofauti na ujazo tofauti, vyakula pia wana uhuru wa kuchagua zaidi ya daraja la kawaida.
3. Hakuna msongamano kama kwenye madaraja mengine.

4. Bei ya kusafiri daraja la kwanza ni kubwa kuliko.

Pamoja na tofauti hapo juu, saikolojia ya daraja la kwanza na mengine ni uthibitisho wa ubinadamu wetu. Watu wengi wakiwa na vijisenti kidogo tofauti na wengine au madaraka yatokanayo na vyeo, tunapenapenda kuonyesha hela au vyeo kupitia tofauti hizi.

Binafsi sijaona umuhimu wa kusafiri daraja la kwanza toka nimeanza kusafiria ndege 2008. Sababu kubwa ni uwiano wa bei na pia mimi siyo mtu wa kupenda sifa au ulimbukeni.
 
Wakuu salama?

Naombeni mnitoe "matongotongo"

Abiria wa daraja la kwanza au VIP kwenye ndege anatofautianaje na wa madaraja ya kawaida?

Nawasilisha🙏
1. Confortable sitting. Mfano, mtu anayekaa kwenye benchi na yule wa kwenye sofa, yupi anakuwa confortable if other factors are kept constant

2. Extra services ndogondogo
 
Back
Top Bottom