Kuna fursa gani za kibiashara ambazo zipo Dodoma?

Kuna fursa gani za kibiashara ambazo zipo Dodoma?

Mbo-Mbo

New Member
Joined
Mar 3, 2019
Posts
2
Reaction score
0
Habarini za asubuhi wanajamvi . mimi ni kijana mwenye miaka 26 nimepata kazi ya uwalimu katika shule moja hapo mjini Dodoma ila msharaha wangu ni mduchu sana. Sasa nilikua nataka kujiongeza kufanya shughuri za biashara katika jiji hili na nimepata ugumu kujua biashara gani zinatoka na zinaweza kunikwamua ombi langu kwenu ni kunipa mawazo yenye kujenga ili niweze kupambana na hali ya maisha ya awam ya tano
 
Fursa zipo nyingi,ila wewe unapenda kujishughulisha na biashara gan zaidi
Nilikua na wazo la kufungua duka au kibanda cha nafaka challenge ikaja maeneo niliyopo ivyo viduka vipo vingi
 
Biashara zipo nyingi ni wewe tu
kuanza andaa budget uuze vifaa vya ujenzi sema usikae mjini kati
 
Fungua duka la kuuza gundi na dawa za kuua panya/mende/kunguni (insecticides/pesticides)
 
pia biashara ya glycerine inalipa sana huko
 
Back
Top Bottom