Kuna haja ya kufanya maridhiano ya kijinsia kwenye jamii yetu

Kuna haja ya kufanya maridhiano ya kijinsia kwenye jamii yetu

Natafuta Ajira

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2020
Posts
9,016
Reaction score
24,650
Kuna sumu kali sana baina ya mwanamke na mwanamme kwenye jamii ambayo inahitajika kuondolewa kwa faida ya vizazi vijavyo.

Angalia matukio ya kikatili yanayofanyika. Kule Mwanza jamaa kampiga risasi mke wake wanaume wanatetea uenda mwanamke hakuwa mwaminifu kwenye ndoa kule Dar dada kachoma moto nyumba mumewe akiwa ndani wanawake wanatetea kwamba kufika maamuzi hayo uenda kuna mabaya mengi alikua anafanyiwa na mumewe ndio uvumilivu umemshinda, yaani watu hawatoi mawazo kwa kuangalia uhalisia wa kitendo kilichofanyika wanatoa mawazo kwa kutetea jinsia zao.

Mwanamke anaona mabaya yanayomkuta mwanaume ni sawa tu, mwanaume anaona mabaya yanayomkuta mwanamke ni sawa tu. Kila jinsia inaishi na kinyongo kwa mwenzake. Je tumefikaje hapa? Machache ya kuzingatia ambayo binafsi naamini yanaweza kumaliza tatizo.

Kwanza, mafundisho ya jando na unyago yarudishwe. Mamlaka husika ziwe zinachungulia tu yanayoendelea uko kusiwe na vitendo vibaya mfano ukeketaji wa wanawake.

Jamii ya leo wanawake na wanaume tunakutana ukubwani tukiwa hatujapitia haya mafundisho kwaiyo kila mmoja hajui saikolojia na hulka ya jinsia nyingine wala hana muongozo wowote uenda hapo ndo tatizo linapoanzia.

Pili, movements na speechs zote zinazowahusu wanawake mfano gender equality, women empowerment n.k zipitiwe upya kama sio kupigwa marufuku kabisa, wanawake wanaoendesha hizi movements kwa kujua hama kwa kutokujua wanachokifanya sio kutetea haki sawa bali ni kupandikiza wanawake wenzao kiburi, jeuri, ubaguzi na chuki kwa mwanaume.

Tatu, maudhui ya vipindi vinavyooneshwa kwenye tv yapitiwe upya, maudhui mengi hayana afya kwa makuzi na maadili ya familia. Na watoto wa kike wamekua wahanga wakubwa maana ndio wanaoshinda na tv siku nzima.

Directors na hosts wa hizi tamthiliya na vipindi mfano wanawake live ya joyce kiria kwa kujua hama kutokujua wanatekeleza ajenda za mabeberu zenye lengo la kualibu kizazi kijacho cha taifa kuanzia kwenye ngazi ya familia ambayo ndio msingi wa taifa zima.

Nne, tatizo la ajira kwa vijana litafutiwe ufumbuzi wa haraka, ikiwezekana iundwe kamati ya vichwa smart ifanye research ije na mpango wa nini cha kufanya. Vijana wa kiume hawawezi kuoa kwa sababu hawana ajira wamebaki kuchezea tu mabinti wa watu.

Watoto wa kike ambao wanatoka kwenye familia zisizo na uwezo wanaamua kujihusisha na ukahaba na udangaji.

Mwanamke ukijisahau unajazwa mimba unakimbiwa mwanaume ukijisahau unapigwa pesa unakimbiwa matokeo yake victims wanabaki na chuki kwa jinsia nyingine kwaiyo wakipata nafasi na wao wanalipiza kisasi kwa mwingine na cycle iyo inaendelea. Hit and run ndo maisha ya vijana kwa sasa.

Hayo ni mawazo yangu kwa uchache tu wabobezi wa masuala ya ustawi wa jamii watakua na mengi zaidi ya kuyaangalia. Ubaguzi na chuki ya kijinsia ni tatizo ambalo linakua kwa kasi mamlaka husika zinapaswa kuliangalia kwa jicho la tatu.
 
Chanzo cha yote haya ni yale ya 50 kwa 50 yanayopigiwa kelele,hapa namaanisha ukishasema hivyo hapo tayari hapo hakuna kiongozi wote mpo sawa, sasa likitokea tukio la mauaji kila upande utaangalia namna ya kuitetea 50 yake ndio maana uhasama unazidi.

Umeandika vizuri kwamba hao wanahamasisha usawa wa kijinsia ni lazima waangaliwe kwa umakini,lengo ni zuri ila namna yao ya kuliendea ni mbaya,hapa inaweza kuwa makusudi au hawajui.

Kitu ambacho wanawake hawajui ni kwamba wanaume ikifika mahali wakaona hizi harakati zinawakandamiza kurudi chini, wao wakimua kurudi kwenye 'status yao ni rahisi sana.

Wanaume tukisema leo tunataka tuwarudishe chini wanawake itahitaji kikao kimoja tu na matokeo utaanza kuyaona haraka tofauti na wao ambao utekelezaji wao bado mgumu sana.

Nitakupa mfano,angalia namna kipimo cha tezi dume cha vidole kilivyokataliwa na wanaume mpaka ikabidi ianzishwe kampeni ya kuwaelimisha kwamba sio vidole tena ila wanapima kwa damu tu,yaani walikuwa wako tayari kufa na ugonjwa ila sio kudhalilika, au angalia jinsi neti za mbu zilivyogomewa kisa walisema zinaua nguvu zetu za kiume, au juzi hapa chanjo ya Corona ilivyogomewa kwa kuhisiwa inaudogosha uume,kwahio wanaume wakiamua kitu leo matokea yake ni makubwa sana tofauti na wanawake ambao kwanza wao kwa wao vita imetawala.

Wote tunakubaliana kwamba wanawake wanahaki sawa na kwamba hawapaswi kunyanyaswa na namna yoyote ile,ila ni lazima tuseme hio 50 kwa 50 ni wapi na ni kwa vitu gani,lakini sio kila mahali.

Mtoto wa kike kusomeshwa,kuajiriwa,kujiajiri,kurithi mali, kuolewa nk ni halali kabisa,kupinga ukeketaji,unyanyasaji kingono,udhalilishaji ni sawa kabisa ila sio kusema haki sawa kila mahali hio haipo.

Nenda hata huko Ulaya na marekani kaulize wanawake wangapi jeshini wanapelekwa frontline?au Special operation?uone kama utaikuta hio 50-50.

Ukiangalia ugomvi na mauaji mengi yanatokea zaidi kwenye level ya familia ambapo kuna ndoa na mahusiano,ukileta usawa huu wa 50/50 huku tegemea majanga kwa sababu mmoja ni kichwa/kiongozi mwingine ni msaidizi,hivi kweli useme mwanamme akirudi usiku na mwanamke anahaki ya kurudi usiku patakalika hapo,au useme mwanaume apangiwe ratiba ya kufua na kupika sawasawa na mwanamke itawezekana vipi?

Tatizo la Afrika tunapenda kuchukua mambo kutoka magharibi na kujifanya tumeshayamudu matokea yake yanatuumiza zaidi kuliko hata huko yalikotokea,mfano angalia tu hata utandawazi unavyotuua,mtu anaangalia waigizaji wa Porn anaenda kujaribu kama ilivyo,wakati wale ni waigizaji,matokeo yake magonjwa yameshamiri,kansa ya koo,ulawiti,ukimwi nk,vyombo vya moto ndio usiseme tunavamia kama kwamba tunavijua sana matokea yake vinatuacha na ulemevu na kudumu.

Kwahio sera ya 50/50 ipitiwe upya ili watu waelimishwe ni wapi pa kuitekeleza na sio kila mahali.Hawa wanaojiita wanaharakati wapatiwe elimu kabisa na vyeti maana wanafundisha Umma,sio kuwaacha waongee wanayotaka wanaharibu jamii badala ya kujenga,ni lazima wasimamiwe.
 
Chanzo cha yote haya ni yale ya 50 kwa 50 yanayopigiwa kelele,hapa namaanisha ukishasema hivyo hapo tayari hapo hakuna kiongozi wote mpo sawa, sasa likitokea tukio la mauaji kila upande utaangalia namna ya kuitetea 50 yake ndio maana uhasama unazidi.

Umeandika vizuri kwamba hao wanahamasisha usawa wa kijinsia ni lazima waangaliwe kwa umakini,lengo ni zuri ila namna yao ya kuliendea ni mbaya,hapa inaweza kuwa makusudi au hawajui.

Kitu ambacho wanawake hawajui ni kwamba wanaume ikifika mahali wakaona hizi harakati zinawakandamiza kurudi chini, wao wakimua kurudi kwenye 'status yao ni rahisi sana.

Wanaume tukisema leo tunataka tuwarudishe chini wanawake itahitaji kikao kimoja tu na matokeo utaanza kuyaona haraka tofauti na wao ambao utekelezaji wao bado mgumu sana.

Nitakupa mfano,angalia namna kipimo cha tezi dume cha vidole kilivyokataliwa na wanaume mpaka ikabidi ianzishwe kampeni ya kuwaelimisha kwamba sio vidole tena ila wanapima kwa damu tu,yaani walikuwa wako tayari kufa na ugonjwa ila sio kudhalilika, au angalia jinsi neti za mbu zilivyogomewa kisa walisema zinaua nguvu zetu za kiume, au juzi hapa chanjo ya Corona ilivyogomewa kwa kuhisiwa inaudogosha uume,kwahio wanaume wakiamua kitu leo matokea yake ni makubwa sana tofauti na wanawake ambao kwanza wao kwa wao vita imetawala.

Wote tunakubaliana kwamba wanawake wanahaki sawa na kwamba hawapaswi kunyanyaswa na namna yoyote ile,ila ni lazima tuseme hio 50 kwa 50 ni wapi na ni kwa vitu gani,lakini sio kila mahali.

Mtoto wa kike kusomeshwa,kuajiriwa,kujiajiri,kurithi mali, kuolewa nk ni halali kabisa,kupinga ukeketaji,unyanyasaji kingono,udhalilishaji ni sawa kabisa ila sio kusema haki sawa kila mahali hio haipo.

Nenda hata huko Ulaya na marekani kaulize wanawake wangapi jeshini wanapelekwa frontline?au Special operation?uone kama utaikuta hio 50-50.

Ukiangalia ugomvi na mauaji mengi yanatokea zaidi kwenye level ya familia ambapo kuna ndoa na mahusiano,ukileta usawa huu wa 50/50 huku tegemea majanga kwa sababu mmoja ni kichwa/kiongozi mwingine ni msaidizi,hivi kweli useme mwanamme akirudi usiku na mwanamke anahaki ya kurudi usiku patakalika hapo,au useme mwanaume apangiwe ratiba ya kufua na kupika sawasawa na mwanamke itawezekana vipi?

Tatizo la Afrika tunapenda kuchukua mambo kutoka magharibi na kujifanya tumeshayamudu matokea yake yanatuumiza zaidi kuliko hata huko yalikotokea,mfano angalia tu hata utandawazi unavyotuua,mtu anaangalia waigizaji wa Porn anaenda kujaribu kama ilivyo,wakati wale ni waigizaji,matokeo yake magonjwa yameshamiri,kansa ya koo,ulawiti,ukimwi nk,vyombo vya moto ndio usiseme tunavamia kama kwamba tunavijua sana matokea yake vinatuacha na ulemevu na kudumu.

Kwahio sera ya 50/50 ipitiwe upya ili watu waelimishwe ni wapi pa kuitekeleza na sio kila mahali.Hawa wanaojiita wanaharakati wapatiwe elimu kabisa na vyeti maana wanafundisha Umma,sio kuwaacha waongee wanayotaka wanaharibu jamii badala ya kujenga,ni lazima wasimamiwe.
Umeongea ukweli mtupu mkuu
 
Back
Top Bottom