Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Hapa kuna wadau wametoa hpja mbili na mimi nijikite humohumo

A. Mmoja kasema tatizo siyo busara wala nini tatizo ni madaktari. Hilo naafikiana nalo kuwa ni madaktari au wahusika wowote wa mambo hayo mfano viongozi wa dini, kijamii na kimila.

Kulitakiwa kujengwe hali/mazingira ya kukubaliana na kifo kwamba mtu akitokea kuonekana na dalili zote basi tufikie ukomo wa kumhangaikia na siyo kumhangaikia mpaka kujiumiza nyinyi wazima msioumwa

Ukitaka kujua sisi hatujajengwa vizuri kwenye maswala hayo angalia 'Wengine' wakifiwa; wanalia kistaarabu tu ile kupunguza machungu ila M'bongo akifiwa sasa; utasikia uuuuuuwii! Hotateeeee weeeee hoootraaataraatraaaaa homameeeee weee! Yaani atataja mizimu yote na kama haitoshi atararua nguo zake bado chini atajigaragaza na mapepo atapandisha hapo bado kamasi plus homa plus...

Au angalia mfano M'bongo akiwa anaumwa halafu cheki hao wanaokuja kumcheki/ kumjulia hali sasa; badala ya kumfariji na kumpa huduma fulanifulani mgonjwa wao ni kujisuwaniza na kujisunja tu yaani mpaka tena mgonjwa ndo anawaonea huruma wao eti! (Samahani nimechanganyia na kiluga)

Hiyo inasababisha watu wanapukutika kiuchumi sana katika kumnusuru mgonjwa na maradhi fulani na hata mtu akifa bado inaonekana ameonewa sana kufa (regardless miaka 70 aliyonayo) hivyo bado wataendelea kupoteza mali kwa 'wataalamu' kutafuta aliye nyuma ya kifo hicho (mchawi) ni nani

Hoja hapo ni watu (hasa madokta) waseme tu ukweli kama mgonjwa amegundulika kuwa na homa ambayo ni 50 kwa 50 uhai na si kuwa-uplift watu halafu baadae ionekane kufa ni uonevu

B. Jambo la pili kuna mdau amesapoti na kusema eti ni sahihi tu kuuza/ kupukutisha mali zote ilimradi kumtibu au kuhangaikia mgonjwa, tena hakuishia hapo akasema tusiige uzungu bali tujikite kwenye Uafrika wetu kwamba hawa wanaobaki basi kuna wajomba, maanti, mababu, na kadhalika eti watawahudumia!!! Shame!

Mjomba kama unaishi kwa kutegemea hivyo kwanza pole sana halafu pili jiandae kuja kutemewa mate na wategemezi wako hapohapo kwenye kaburi utakalozikwa

Ni kweli kuna mtu kum'beba ndugu yake au ndugu wa babu baba na hata ndugu wa mama yake lakini siyo kihivyo aisee! Utawaachia watu jAnga
 
Mleta mada nilikusihi kwamba unaumwa akili... lakini nataka niseme kwamba sikumaanisha nikuudhi... nilitaka niku engage ili tujadili zaidi kwa nini nimesema hivyo... hata hivyo, kuambiwa unaumwa akili sio tusi...Nimesha futa hiyo post yangu na utanisamehe hata kama hatujuani kwani kama ulisikia uchungu hata kidogo, ninaamini kwamba uwajibikaji baada ya kufa itanihusu...lakini ndio binadamu tulivyo, tunatenda makosa kila wakati... nisamehe bure..

Wazo lako kwenye hii mada ni haki yako na waliotofautiana na wewe nae wana haki yao... mara zingine, wote wanakuwa sawa tu, ila mmoja anakuwa sawa zaidi kutokana na hali halisi ya ile issue husika...

Have a blessed Sunday...



Sent using Jamii Forums mobile app
 
How can you compare life and money wakati Mali zenyewe tunaziacha.
Unaziacha wewe unayekufa!

Kumbuka kuna watoto wadogo wasio na pa kwenda! Unauza nyumba halafu??

Busara inapaswa kutumika hapa na kujua lipi ni bora zaidi!

Uchague kati ya mzee wa miaka 70 na mayatima wadogo wasiojua kesho watalala wapi!

Mambo ya kucheza biko hapana!
 
Mleta mada nilikusihi kwamba unaumwa akili... lakini nataka niseme kwamba sikumaanisha nikuudhi... nilitaka niku engage ili tujadili zaidi kwa nini nimesema hivyo... hata hivyo, kuambiwa unaumwa akili sio tusi...Nimesha futa hiyo post yangu na utanisamehe hata kama hatujuani kwani kama ulisikia uchungu hata kidogo, ninaamini kwamba uwajibikaji baada ya kufa itanihusu...lakini ndio binadamu tulivyo, tunatenda makosa kila wakati... nisamehe bure..

Wazo lako kwenye hii mada ni haki yako na waliotofautiana na wewe nae wana haki yao... mara zingine, wote wanakuwa sawa tu, ila mmoja anakuwa sawa zaidi kutokana na hali halisi ya ile issue husika...

Have a blessed Sunday...



Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa mkuu. Yameisha. Uwe na siku njema pia. One love.
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu JamiiForums.

Ndugu zangu Watanzania;

Kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa. Familia masikini/fukara kuuza nyumba yao ya pekee ni pigo kubwa sana kwa watoto wadogo.

Ninaandika haya nikijua fika ya kwamba hakuna idadi ya mali au pesa kinachoweza kulingana na uhai wa mwanadamu. Unakumbuka ajali ya MV Bukoba wewe? Unakumbuka ajali ya MV Spice kule Zanzibar?

Ni Watanzania wangapi walikufa katika ajali zile? Hivi wakati wa majanga yale uliwahi kusikia hata siku moja Watanzania wanalalamika kuhusiana na thamani ya zile meli?

Unajua gharama ya vyombo vile ni mamilioni ya pesa ngapi za Kitanzania? Licha ya kuwa ni pesa nyingi sana zilitumika katika kununua/kuunda vyombo vile Watanzania bado wakawa wanalilia roho za binadamu wenzao kwa maana kwamba hakuna cha kufananisha na uhai wa mwanadamu.

Hiyo ndio asili ya huruma ambayo Mungu ametupa sisi wanandamu. Familia zetu hizi masikini, mali tunazipata kwa tabu sana, ujenzi wa kuungaunga nyumba moja unajenga kwa kudunduliza miaka zaidi ya 9.

Baada ya ujenzi kukamilika, mnaishi miaka yenu 3, alafu ghafla mnasikia baba yenu mzazi anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya ini au figo zote zimefeli anapaswa kupelekwa India kwa matibabu zaidi.

Ndugu wanajitahidi kuchangisha kwa jamaa na rafiki zao hapa na pale kiasi hakifikii pesa sahihi inajohitajika kuweza kukidhi gharama za matibabu hivyo wanaamua kuuza mali zao za thamani walizonazo kumpeleka baba yao nje ya nchi (India) kwa matibabu zaidi.

Matokeo yake baba anakufa, mzee wa miaka 69, na mali zote mmeuza. Unaikuta familia iliyotoka kupanga chumba na sembule kisha wakajikwamua kujenga wanarudi tena katika nyumba za kupanga na maisha ya kuomba omba.

Nimemua kuleta mada hii hapa baada ya kukutana na kijana mmoja jina lake ni ****** ambaye nilikuwa ninakaa nao Keko Juu mwaka 2011 ambaye baba yao alifariki mwaka 2014 kwa ugonjwa wa saratani ya kibofu cha mkojo.

Inasemekana kwamba mzee yule wa miaka 66 hakuwa na matumaini ya kupona, kulingana na taarifa ambazo mmoja wa ndugu yao wa karibu (baba mdogo) alipewa na daktari katika hospitali moja maarufu tu hapa Dar.

Kwa kuwa familia bado ilikuwa inampenda na kumthamini mzee wao wakaona ni bora wauze hata nyumba waliokuwa wanajenga huko Toa Ngoma njia ya Kongowe ili wampeleke baba yao huko India. Matokeo yake ndio kama haya. Wamepoteza vyote, baba pamoja na nyumba.

Mama ndio hivyo tena biashara za kuungaunga za akina mama lishe, dada zake wawili walizaa tu hapo nyumbani yaaani nilipoonana na huyu kijana (ni agemate na mimi) machozi yalitaka kunitoka.

Basi tu kwa kuwa na mimi mwenyewe ni Taxi Driver mlala hoi sina cha kumpa zaidi ya kusimuliana story za zamani tulipokuwa tunacheza mpira (cha ndimu) wote na kwenda kuogelea baharini kule Kurasini tulikuwa tunapaita ZAMCARGO au SAVA.

Ndugu zangu, kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike tusizidishe umasikini katika familia.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Kuna kipindi ni muhimu kukubali kwamba kifo kwa ujuzi wetu wa sasa hakiepukiki, na kuna watu wataendelea kuishi baada ya mtu kufariki, hivyo, inaweza kuwa busara kuweka mbele interests za watakaobaki.

Hususan kama mgonjwa anaumwa ugonjwa chronic na kashakuwa mtu mzima.

Mimi siwezi kubariki wazo la kuuza nyumba zangu nilizohangaikia maisha yangu yote, zije kuwa nguzo ya kusaidia uchumi wa kizazi changu na ndugu zangu wa karibu, ili tu niongeze miaka michache katika maisha yangu.

Kitu cha muhimu kabisa ni kujiweka katika mazingira ambayo hatuhitaji kuchagua kimoja kati ya mawili haya, na tunaweza kufanya yote. Kujihudumia matibabu bila kufikia hatua ya kufanya kitu kama kuuza nyumba.
 
Kuna kipindi ni muhimu kukubali kwamba kifo kwa ujuzi wetu wa sasa hakiepukiki, na kuna watu wataendelea kuishi baada ya mtu kufariki, hivyo, inaweza kuwa busara kuweka mbele interests za watakaobaki.

Hususan kama mgonjwa qnaumwa ugonjwa chronic na kashakuwa mtu mzima.

Mimi siwezi kubariki wazo la kuuza nyumba zangu nilizohangaikia maisha yangu yote, zije kuwa nguzo ya kusaidia uchumi wa kizazi changu na ndugu zangu wa karibu, ili tu niongeze miaka michache katika maisha yangu.
Umenena vema sana mkuu...
 
Kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike
Hii Mada yako iko sawa; Labda ila nadhani inategemeana na Potential ya Mtu; Mfano mtu alikuwa ni mpambanaji (potential) hili lazima liangaliwe kwanza kupambana kuhakikisha anatoboa,
Sasa unakuta watu wanapambana na Mtu wa 90, of which kama Busara alishawaachia wenye umri mdogo, lakini hela inatumika nyingi sana tena kwa kuchangishana binafsi sionagi umuhimu wake.

Kama Hela ya Matibabu ya muda mrefu ipo na si tatizo miongoni mwa wanafamilia, then atibiwe tu mpaka umauti utakapomfiika.
 
Hii Mada yako iko sawa; Labda ila nadhani inategemeana na Potential ya Mtu; Mfano mtu alikuwa ni mpambanaji (potential) hili lazima liangaliwe kwanza kupambana kuhakikisha anatoboa,
Sasa unakuta watu wanapambana na Mtu wa 90, of which kama Busara alishawaachia wenye umri mdogo, lakini hela inatumika nyingi sana tena kwa kuchangishana binafsi sionagi umuhimu wake.
Hakunaga umuhimu kabisa kwa watu wanaotoka katika familia ya kipato duni/cha chini...
 
Unaziacha wewe unayekufa!

Kumbuka kuna watoto wadogo wasio na pa kwenda! Unauza nyumba halafu??

Busara inapaswa kutumika hapa na kujua lipi ni bora zaidi!

Uchague kati ya mzee wa miaka 70 na mayatima wadogo wasiojua kesho watalala wapi!

Mambo ya kucheza biko hapana!
Ninaomba kutilia mkazo tu kwamba, watoto wadogo ni lazima wapewe kipaumbele kwanza.
 
Hustling tunazofanya kila siku huwa sio kwa ajili yetu, zaidi ni watoto tunaowaleta Duniani...wewe maliza kila kitu sasa uwaachie makaburi tu halafu hizo mali watatafuta wenyewe.
1610996476659.png
 
Back
Top Bottom