Kuna jamaa yangu alikua USAID akawa ananifungia vioo, leo kanitumia ujumbe kama nina mchongo wowote nimpasishie

Kuna jamaa yangu alikua USAID akawa ananifungia vioo, leo kanitumia ujumbe kama nina mchongo wowote nimpasishie

Mtoa post nawe limbukeni na maskini tu ndio nini kumuanika mwanaume mwenzio huku kwenye forum.
 
Kuna watu sijui ni ulimbukeni au ushamba.

Huyu jamaa yangu yeye alibahatika kupata kazi tu after graduation kwenye hizi NGO zilizokua chini ya USAID, kwa kipindi kile kijana mdogo kulipwa 3m per month ilikua ni pesa nyingi mno.

Jamaa akaanza maringo na akawa anatuona akina sisi ambao by that time tulikua majobless sio wa standard zake. Imepita miaka kadhaa hatimae Trump kafanya yake huko.

Jamaa leo kanitumia ujumbe eti nikisikia au kama nina mchongo wowote nimpasishie. Nimemjibu me niko nalima kijijini kwetu kama unaweza njoo tupige jembe, huo ndio mchongo nilionao kwa sasa.

Jamaa hajajibu kitu.
Huna jamaa yoyote wa huko sema ni wivu tu ulikua unakusumbua sasa umeona fursa ya kuwasimanga.
 
Mssamehe tu mkuu, watu wengi wako hivyo. Mimi classmate wangu mmoja aliwahi kupata kazi benki moja hivi, akapata vijisenti wakati wengine bado tunajitafta, akawa na maringo mengi sana hata kwenye group la darasa letu wa mwaka wetu akajitoa. Miaka michache iliyopita nadhani pale kazini paliota nyasi, akaanza kututafta ambao hatukua na chochote( kwa sasa tuna zaidi ya chochote)

Akaanza kuomba akopeshwe elfu 20, mara 30 eti atalipwa siku flani, siku flani. Akaanza kuomba akopeshwe kiwango cha pesa ambacho mimi siwezi kumkopesha mtu, below 100k sikukopeshi, nakupa tu, sasa ajabu mtu ananiomba nimkopeshe elfu 20 au 30 nikajiuliza sasa hii inamsaidia nini huyu boss?

Mpuuze tu mkuu.
mmmh binadamu kazi sana.
 
Sijaona tatizo la jamaa wako wa USAID.
Alijuaje kama jamaa anadharau?,alijuaje kama jamaa kamfungia vioo? .sio mtu anapiga simu muda wa kazi isipopokelewa unasema kakufungia vioo.

Mimi nilipomaliza chuo miaka mingi iliopita ,nilikuwa naona wenzangu kama wananifungia vioo sababu wamepata kazi nzuri na wengi cycle yangu walikuwa washapita hatua kubwa sana.
lakini nilipoanza kupata kiasi ambacho nimejaaliwa na Mungu nikaanza kuona ilikuwa ni bias tu , wengi walikuwa busy sana na majukumu mengi. familia za kiafrika akitoka mmoja tu basi ndugu jamaa marafiki ,ukoo wanadondokea huko.

Tujifunze kitu pia ,ukipata usidharau au kumfungia viooo aliepo nyuma yako

Ally Mohamed, Nairobi 18:00 EAT
 
Back
Top Bottom