KWELI Kuna mimea inakula nyama

KWELI Kuna mimea inakula nyama

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Kuna watu nimewahi kuwasikia kuwa eti kuna miema inakula nyama, je kuna ukweli wowote katika hili?

1730803696800.jpeg

 
Tunachokijua
Mimea inayokula nyama ni mimea inayopata baadhi au sehemu kubwa ya virutubisho vyake kwa kunasa na kula wanyama au protozoa, mara nyingi wadudu na viumbe wengine wa arthropodi, na wakati mwingine mamalia wadogo na ndege. Mimea hii inapata nguvu zake zote kutoka kwa usanisinuru.

Je, ni kweli kuna mimea inayokula nyama?
JamiiCheck imefatilia na kubaini kuwa ni kweli kuna mimea inayokula nyama na Kuna zaidi ya spishi 583 za mimea inayokula nyama. Mimea hiyo inakula nyama ili kufyonza virutubisho vinavyopatikana kutoka kwa wadudu.

Mifano maarufu ya mimea ilayo nyama ni pamoja na mimea aina ya Venus flytrap (Dionaea muscipula), pitcher plants, na bladderworts (Utricularia spp)

CephalotusMouths.jpg

Venus Flytrap (Dionaea muscipula) majani yake yanayofungika haraka ili kunasa wadudu, wanapoingia na kugusa majani hukunjuka na kufunika mdudu, na kisha hufyonza virutubisho baada ya kumeng'enywa.

Pitcher Plants (Nepenthes, Sarracenia, na wengineo) Majani yake yanayofanana na mtungi uliojaa maji yenye enzaimu za kumeng'enya kinachonaswa, Wadudu huvutwa na harufu na wakiingia, wanateleza na kuanguka ndani ambapo hufyonzwa taratibu

Bladderworts (Utricularia spp.) Hii yenyewe hupatikana majini au kwenye maeneo yenye unyevunyevu. Ina mifuko midogo ya hewa inayofanya kazi kama mitego ya kunyonya viumbe vidogo wanapoikaribia.

Nlowii_Rice_nepenlowii001.jpg
-Mimea hii huwa inavutia ili kuwanasa wadudu, Majani ya mimea ilayo nyama huwa kama mitego kwa wadudu kupitia harufu na rangi

-Mimea ilayo nyama hutoa kemikali za kumeng’enya (enzaimu) ambazo huvunja au kusaga wadudu kuwa virutubisho vinavyoweza kufyonzwa.

-Mimea ya carnivorous hufyonza virutubisho kutoka kwa wadudu ili kusaidia ukuaji wake katika mazingira yenye uhaba wa virutubisho vya asili.
Kuna watu nimewahi kuwasikia kuwa eti kuna miema inakula nyama, je kuna ukweli wowote katika hili?

Hao kitaalamu wanaitwa insectivorous plants.
Zipo specie kadha wa kadha, upo mmea flan wenyewe huwa una structures flan kwenye majani hizo structures huwa zinatoa sticky fluid (kimiminika kinachonata kama gundi) mdudu akijichanganya akatua ananaswa hafu anaanza kumeng'enywa na kuabzobiwa taratibu mpaka anaisha
 
Kuna mimea inapiga supu ya utumbo na chapati kila asubuhi! Inapiga na mswaki! na kuondoa mabaki ya nyama kwenye meno na stick! Hatari sana!
 
Nikimfundisha mwanangu akajibu hivi kwenye hii mitihani ya mkenda atapata tiki?
 
Pia kuna mimea inapiga story na mimbea hiyo. Jamiicheck fuatilieni hilo wakuu.
 
Kuna watu nimewahi kuwasikia kuwa eti kuna miema inakula nyama, je kuna ukweli wowote katika hili?

Ndio, kuna mimea inayokula nyama, na huitwa mimea inayokula wadudu au mimea ya minyama (carnivorous plants). Mimea hii imebadilika na kuweza kunasa wadudu na viumbe wadogo kwa ajili ya kupata virutubisho vinavyohitajika, hasa katika mazingira ambayo yana upungufu wa virutubisho kwenye udongo.

Mimea maarufu inayokula nyama ni pamoja na:

1. Venus Flytrap (Dionaea muscipula) - Ina majani yenye umbo la mtego ambayo hufunga ghafla inaposikia mguso wa wadudu.

2. Pitcher Plant (Nepenthes na Sarracenia) - Ina majani yenye umbo la kikombe kilichojaa kimiminika ambacho huteleza na kunasa wadudu wanaoingia ndani.

3. Sundew (Drosera) - Ina majani yenye nywele ndogo zenye ute, ambao hunasa na kumeng’enya wadudu.

4. Bladderwort (Utricularia) - Mimea hii huishi majini na ina mtego wa “vifuko” vidogo vinavyosababisha mkondo wa maji unaonasa wadudu wadogo.

Mimea hii husaidia kuongeza virutubisho kama vile nitrojeni, ambayo ni ngumu kupatikana katika udongo wa maeneo yenye virutubisho duni.
 
Mimi huwa naiona kwenye cartoon tu, ila pia nimewahi kusikia kuna mimea kama maua inafyonza wadudu. Sasa sijui ni inawala au inawanyonya tu maji na mafuta.
 
Back
Top Bottom