Kuna mtu kaniuliza hili swali jamani, anataka msaada wa Mawazo yenu. Maji yamemfika shingon


Dah, umesema kweli, nahisi ingekuwa mimi ningeondoka kabla sijaambiwa ondoka......
Lakini sasa upendo una nguvu ujue, yawezekana kabisa huyu kaka anampenda mke wake,
na uamuzi wa kumfukuza ni mgumu na mzito kwake. Hajui hata aanzie wapi yani.
Au ndo limbwata lol!!
 
Yani huyu bibie kashafumwa kaka angu.

Kwa kuwa anajua kwamba hata akisamehewa atarudia tena...basi asimsumbue jamaa yake na machozi ya uongo!
 
Aende Makongo, Jangwani, Zanaki au Tambaza High School ajichagulie mrembo aanze kumlea kwa ajili ya maisha mapya..... Na wewe akuwashie taa za emergence tayari kwa kuanza safari nyingine ya kuwa na hao unaocheza nao
 
Kama wewe hapo swala kama hili ungefanya je AK-47?
Ok huwezi kumsamehe, sasa ungefanya je? Unampa Talaka, Unamfukuza kama Mbwa, unamrudisha kwao au unafanya je?

Kwa hilo hata maandiko yatanisamehe dawa ni kuachana nae tu LD.
 

Aliyeomba ushauri ni kaka Bobby, na anaumia kweli kweli, kwa jinsi anavyomjali mke wake lakini haridhiki.
Hapo kwenye Red usiogope sana bwana, wakati mwingine hizi tabia ni za mtu mmoja tu. Wengine kwenye ukoo wanaweza kuwa salama.
 

1,2,3 ye yumo tuu ..sasa ya 4 pia asamehe basi ..
inaonyesha ana moyo wa chuma AU nae anafanya sema hajafumaniwa,
so it doesn't pain him..after all they say 'tit for tat is a fair game'.
 
Kwa hilo hata maandiko yatanisamehe dawa ni kuachana nae tu LD.

Sawa AK-47. Hebu niambie unachana je naye??
Yani unafanya nini, ili kumalizana naye kabisa, halafu useme nimeshakuacha sasa.
 
Mwambie huyo mwanamke aondoke maana mara ya nne nadhani atachinjwa...japo kuwa nachelea kusema kwamba huyo mwanaume ni sawa na raisi mmoja anayeoatikana katika East Afrika ambaye hawezi kufanya maamuzi magumu,
 
Aende Makongo, Jangwani, Zanaki au Tambaza High School ajichagulie mrembo aanze kumlea kwa ajili ya maisha mapya..... Na wewe akuwashie taa za emergence tayari kwa kuanza safari nyingine ya kuwa na hao unaocheza nao

Dah kaka huna huruma, upendo wa kweli, unasamehe saba mara sabini jamani.
Mbona sisi tunawasamehe wanaume?
 

...Madhali amevunja kiapo cha utiifu na miiko ya ndoa, ni aheri kuachana nae ambayo yanajumuisha yote hayo mawili, kumpa talaka na "kumrudisha" /kumkabidhisha kwao.

mara tatu nadhani huyo mwanaume ana mapungufu katika kufanya maamuzi mazito

...Simlaumu kwa hilo, hili linategemea na Mapenzi aliyokuwa nayo kwa mkewe.
 
Aliyeomba ushauri ni kaka Bobby, na anaumia kweli kweli, kwa jinsi anavyomjali mke wake lakini haridhiki.
Hapo kwenye Red usiogope sana bwana, wakati mwingine hizi tabia ni za mtu mmoja tu. Wengine kwenye ukoo wanaweza kuwa salama.

I thought ni dada ndo aliomba ushauri....
Unajua kufumwa ni dalili za kurudia kosa mara nyingi...anazini mara nyingi huyo mke....
Binafsi sipendekezi msamaha...
Huyo jamaa ajitenge kwanza na huyo mke (angalau kwa miezi 6), aweze kutathmini maisha yake....angaalie uwezekano wa maisha bila ya huyo mke....
Kama bado ataona anamhitaji, basi amwite waongee upya....ila kumwacha for good ndo ushauri wangu wa kwanza!
Kama ataona
 
Babu DC, mwenzio anampenda mke wake, lakini ndo hivyo huyo bibie anashindwa kuacha hiyo tabia.
Kwani babu unadhani usingeweza kusamehe mara zote hizo?

Mara tatu hapana mpenzi LD.

Yaani nikifikie hata hiyo mara moja nakaribia kuzimia. Sasa ikifika mara tatu si sawa na kujiandikia RIP?
 
Mwambie huyo mwanamke aondoke maana mara ya nne nadhani atachinjwa...japo kuwa nachelea kusema kwamba huyo mwanaume ni sawa na raisi mmoja anayeoatikana katika East Afrika ambaye hawezi kufanya maamuzi magumu,

Inawezekana anaweza kufanya maamuzi magumu kabisa EM, lakini aanzie wapi, mtu anampenda jamani. Amfukuze? afanyeje sasa? hebu mpe njia ya kufanya basi. Unajua kuna yale maisha unaishi kwa kumjali mkeo na kujenga heshima kiasi kwamba hata ukisema unamuacha kwa ukahaba wake, unaumia mwenyewe kwanza. Yani huu moyo wa huyu kaka ndio unaongea haya maneno. Na amechoka kweli tabia ya mke wake. Lakini kila anapofikiria huo uamuzi alionao sasa hivi wa kumuacha awe huru, anaumia sana. Anaona ni kwa nini mwanamke amekuwa na roho ngumu kiasi hiki kwenye swala la uaminifu kwenye mahusiano?
 
Hapa mi nafikiri kuwa huyu mwanaume naye anayo matatizo fulani ndiyo maana anamsamehe kila wakati, Mapungufu ni ya Mwanaume, Kama mwanaume hana mapungufu hawezi kuwa anasamehe samehe ujinga kila mara.
Nashauri huyu jamaa ajichunguze yeye mwenyewe kwanza ni mambo gani mke anakosa toka kwake?
 

Haya Mtakatifu nimekuelewa na kukupata.
Kwa hiyo ampe likizo sio. Asimfukuze kama Mbwa eeh!!
Wala asimpe Talaka kwanza?
 


Hapo hakuna libwata wala chochote hivi na huyo mwanamke amekaa tu anaona jamaa falaaa eti anamsamehe mara tatu na anasubiri ya nne mpe tahadhali ya hali ya juu sana huyo mwanaume sio mjinga hata kidogo ataletewa mwanamke aambiwe alale chini ndo ataisoma namba
 
Mara tatu hapana mpenzi LD.

Yaani nikifikie hata hiyo mara moja nakaribia kuzimia. Sasa ikifika mara tatu si sawa na kujiandikia RIP?

Haya babu yangu, nimekupata kabisa.
Sasa babu, mwanaume akifumaniwa hata mara mia mbili unaweza shauriwa umsamehe tu.
Vipi hapo Babu yangu hakuna kauonevu kweli.
 
Dah AD, hapa mdada naona hana chake.
Enough is Enough!!!

Hakuna mwanaume mjinga kiasi hicho asikwambie mtu wanakuwaga na uvumilivu na wanaweza kuvumilia sana
Ila kwa hilo sidhani kama anamaanisha huyo jamaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…