Kuna mtu kaniuliza hili swali jamani, anataka msaada wa Mawazo yenu. Maji yamemfika shingon

huyo jamaa inaonesha hata akiprintiwa atasema JF wasimuingilie katika maamuzi yake. huyu anaapply kwenye ile sredi yako ya ving'ang'anizi. Tuongezeni maombi jamaa astuke

Sasa hapo achanganye na zake!!!Akiamua kubaki nae siku nyingine asianze kulialia!!!
 
omeona mbu na aanze kutupa mawe halafu mbona wakali sana wakati nasikia nyie wengine wanajisahau wanaenda nao mpaka nyumbani walinzi wanawashtua kina mama wao husamehe mara ngapi? halafu na kale kamsemo kenu MWANAUME HAWEZI KUWA MWANAMKE MMOJA NATURE INAFANYA KAZI:ballchain::juggle::smash:


...kwenye red patamu hapo.
"...na aliye msafi awe wa mwanzo kutupa jiwe!"
LD jibu hilo!

...duuu, nimejichokea mie.
ama mstaafu hapa umepigilia msumari kwenye jeneza.
 
Sina mpango wa kumkosea wala sijawahi kumkosea hata siku moja UMELOGWA WEWE

Mnataka kwenda wapi aisee!!
Hebu tulieni bwana.
Tunataka njia ya kumwadhibu mwanamke asiye kuwa mtiifu/mwaminifu kwa mume wake,
sio kuwatafutia Desdii na TF BAN bwana wangu!!!
 

Nnayo maswali mengi nataka kumuuliza huyo jamaa yako.

  • Alimuoa huyo mwanamke baada ya kufahamiana na ye muda gani?

  • Huyo mwanamama na huyo mkaka wanapishana sana kiumri?
  • Huyo jamaa yako anamtosheleza mdada kwa namna zote ukiacha mahitaji ya chakula, nguo, etc.
  • Mdada aliwahi kumfumania jamaa hata mara moja?
 


Mhhh kwahiyo hapo ni swala la mazoea zaidi!!Maana kwenye hii kesi hamna heshima wala kushirikiana...unless wameamua ashirikiane na watu wengine kumridhisha mke wake....kufahamiana hapo hamna maana huyo mwanaume anaonyesha fika hajui mke wake ni mtu wa aina gani ndo maana sasa hivi anauliza chakufanya!!!Shauri lake.....MAZOEA YAKIMPELEKA KABURINI KWA PRESHA AU NGOMA NDO ATAJUA mazoea mengine sio ya kuendekeza!!
 
Ha ha ha ha imeandikwa SAMEHE mara saba sabini??!!!!! Sasa wanaume wasamehewe mara ngapi maana kuchapa nje ni mila na desturi. Kama mume anachapa nje ruksa mke naye achape nje. Revenge!!
 
Huo ndio mpango Lizzy.
Yani hapa nipo kikazi zaidi yani, more than serious.
Maujumbe yote haya atayapata vizuriiiiiii!!!!

Yeah mpe achanganye na zake mpendwa!!!Hopefully maamuzi atakayofanya yatakua faida kwake na sio hasara!!!
 
Dah, na hiki ndicho kinachouma zaidi Mbu,
Kwa maana ingine kama nyie wote mnacheat inabidi msameheana tu sio?

...naam, naam, ingawa inategemeana nakosa, kusameheana kwenye mazingira hayo inakubalika kwani hakuna mkamilifu hapo. Kuna wengine wana justify cheating kulipiza alivyomtendewa, Utamlaumu vipi?


...swadakta.
Mtu anapokuwa na uwezo wa kusamehe mara tatu, na bado akaendelea kutendwa,
ni bora kujikalia kimya. Aibu ya mke ni yake pia.
Lazima kuna jambo huyo mwanaume amechangia hiyo tabia ya bi mkubwa kujirudia rudia,
hata kama ni kwa nia nzuri tu.

Katika maisha ya ndoa, kuna ushuhuda wa Mke, ushuhuda wa Mume, na Ukweli.
Lazima kuzingatia mambo matatu haya kabla ya kuhukumu.
 
Akirudia tena ammwage tu, hii misamaha mwisho hutupeleka kubaya, binafsi nilisamehe mara 3 kilichotokea baada ya hapo , ukisamehe sana mwisho mtu anafanya tu akitegemea msamaha. Hata msamehej mwisho unachoka . Pole sana kwa mkaka.
 

Ni kweli Mbu, hebu tujaribia kumfikiria huyu jamaa labda ana miaka 40, halafu labda ameishi na huyu mama miaka 10.
Kwenye ndoa ya Kikristo, mi simshangai sana jamani, anapoumia, nakushindwa cha kufanya juu ya uamuzi wa kumuacha.
Ni maamuzi magumu na mazito kweli kweli.
 
Mnataka kwenda wapi aisee!!
Hebu tulieni bwana.
Tunataka njia ya kumwadhibu mwanamke asiye kuwa mtiifu/mwaminifu kwa mume wake,
sio kuwatafutia Desdii na TF BAN bwana wangu!!!
Hamna BAN hapa wala babu yake na ban, unamwadhibu mwanamke ili iweje kwamba ukimuadhibu ndio ataacha??? Lazima ujiulize kwanza sababu za huyo mwanaume kumsamehe huyo mwanamke mara tatu.
 
Ld hembu chunguza vizuri napata mashaka lazima kuna jambo na mara nyingi upande mmoja hauwezi kukupa majibu yatayoridhisha maana hiyo sentensi aliyosema ni nzito je kwa mama inapply au ni kwa mtazamo wa baba anafikiri anampa kila kila anachohitaji?.

 
Ataendelea kukusamehe maana yeye ni ktom*i zaidi yako ndio maana anakusamehe ili na ww ukmgumia umsamehe pia,kwahiyo we endelea na yy ataendelea kama kawa
 

Man ni kweli inauma sana kuachana na umpedae lakini sometime you do so by assuming that she is dead. Kama anamuonea huruma sasa next time atamkuta kitandani Live na mwanaume mwingine wakicheza vengereeeee. Je, hapo atamwambie njoo mke wangu kavae nguo zako uje huku sebuleni au ataamua pia kumuogesha kabisa kuonyesha kwamba amemsamehe pia? Man chunga sana maisha matamu, ukifa hurudi pia hujui uendako ukifa! Hujiulizi kwanini taifa linakimbilia Loliondo?
 

Asante Samawati.
Naomba muda kidogo, nitaleta majibu ya haya maswali.
 

..ah haaha!
mara ngapi ushasikia wanandoa wanalalamikiana; "siku hizi simuelewi elewi kabisa mwenzangu, amebadilika!"
mara ngapi ushasikia watu wanasema, "akishaingia kwenye ndoa ndio utaona moto wake!"

Haya ndio yanayotokea ndani ya ndoa. Chaka hilo, huwezi jua miba yake mpaka uupande mchongoma!
BTW, nilimuomba LD atuambie huyo Bi Mkubwa huombaje msamaha.

Kuna wale wanawake wanapoomba msamaha hupiga magoti wakilia mpaka huruma inakujia,
wapo wenye kujiapiza kamwe hawatarudia tena, na huapa bora wajiue kuliko kuishi bila waliyemkosea.
Huruma mama, huruma.
 
Kama huyo mwanamke keshabambwa mara tatu basi hiyo ni ishara tosha kuwa keshachiti mara kibao.

Na kwa maoni yangu hakuna mwanaume wa ukweli, mwenye ego ya kiume atakayesamehe hata kuchitiwa mara moja achilia mbali mara tatu au zaidi!

Uamuzi wa mwisho ni wa huyo mume mtu. Lakini unapomsamehe mwenza muasherati mara zote hizo basi hata yeye huyo mwenza anaweza kukudharau sana.
 
Reactions: LD

Baeleze basikie bana
 
Mnataka kwenda wapi aisee!!
Hebu tulieni bwana.
Tunataka njia ya kumwadhibu mwanamke asiye kuwa mtiifu/mwaminifu kwa mume wake,
sio kuwatafutia Desdii na TF BAN bwana wangu!!!

Aondoke kwa mumewe huyo mwanamke hafai.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…