SI KWELI Kuna namba inayowapigia watu na wakipokea wanafariki

SI KWELI Kuna namba inayowapigia watu na wakipokea wanafariki

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
kuna ujumbe unasambazwa kwenye makundi ya whatsapp ukidai kuwa kuna namba ikikupigia ama kutuma ujumbe na ukijibu unapoteza maisha kwani mtumiji wa namba hiyo anatafuta damu za watu ni kweli?
Jmc.jpg
 
Tunachokijua
Kumekuwepo na ujumbe mfupi wa maandishi unaosambazwa kwenye makundi ya Whatsapp ukiwatahadharisha watu kuhushu uwepo wa namba ya simu inayotuma ujumbe ama kupigia simu watu, na wale watakaoujibu ujumbe huo ama kupokea simu kutoka kwenye namba hiyo wanapoteza maisha, na watu 12 wameshapoteza maisha kutokana na kujibu ama kupokea simu kutoka kwenye namba hiyo.

Ujumbe huo pia unaeleza kuwa anayetumia namba hiyo ni mwanamke ambaye lengo lake ni kuwanyonya watu damu.

Ukweli upoje?
JamiiCheck imeuchunguza ujumbe huo na kubaini si wa kweli kwani taarifa hiyo imeeleza kuwa vifo 12 vilivyotokana na suala hilo imetangazwa “Leo saa mbili” kwenye shirika la habari TBC, ujumbe unasema kuwa taarifa imetangazwa “Leo’’ lakini haujaweka tarehe husika ya suala hilo lilipotangazwa hivyo kuleta changamoto ya kubaini “Leo” inayozungumziwa ni ipi? Lakini pia ujumbe haujaeleza hivyo vifo vimetokea wapi na lini, na waliofariki ni akina nani.

Ujumbe huo umeweka namba ya simu inayotumika na anayedaiwa kuwa mnyonya damu lakini namba hiyo ni pungufu kwa ina namba tisa badala ya kumi kama ilivyo kwa namba nyingine.

JamiiCheck imeipigia namba hiyo na majibu yalikuwa kwamba "Namba hiyo haipo tafadhali hakikisha namba na ujaribu tena."

JamiiCheck imewasiliana pia na Shirika la utangazaji Tanzania (TBC) kupitia kwa Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano cha shirika hilo Catherine Nchimbi kupata uhalisia kama wameshawahi kutoa taarifa hiyo ambapo amesema kuwa tarrifa hiyo uzushi na imekuwepo kwa muda mrefu.
JamiiCheck hii inawezekana ila sio kwa scenario aliyoleta mtoa mada, Jana tumetoka kuona tukio la Pagers (Inafanya kazi kama simu) za wapiganaji wa Hezbollah zimelipuka nakuua wapiganaji tisa, huku watu si chini ya mia moja wakiwa majeruhi, Kinachoonekana ni kuwa hizi simu zilikua zimekwa small quantity (20g) ya milipuko ya kijeshi ambazo zilifichwa ndani ya simu kusubiri command ya mlipuko, na command hii inaweza kuwa activated kwa namba maalumu au sms maalumu. hapo hapo mlipuko unatokea na unaweza kufariki. Hii ni moja ya kazi za Mossad Israel.

source: Israel's spy agency Mossad planted explosives in Hezbollah pagers, reports say
 
Back
Top Bottom