Kuna nguvu ya ziada Babu Talenti anaitumia sio bure kwa kweli.

Kuna nguvu ya ziada Babu Talenti anaitumia sio bure kwa kweli.

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Wakuu nahisi huyu ndugu babu talent kuna nguvu ya ziada anaitumia si bure.

Nimejaribu kufatilia kwa karibu kabisa wasanii waliokuwepo chini yake na baadaye kwa namna moja au nyingine wakaachana naye hasa kuachana naye katika mazingira ambayo sio mazuri ,wengi wao kama sio wote wanapotea kabisa kwenye ramani ya mziki na hawasikiki tena ,ngoja nikutolee mfano wa wanamuziki waliokuwepo chini yake na baadaye wakaachana naye na kupotea mazima ;


1)MB Doggy

Screenshot_2017-05-18-23-45-43_1.jpg
huyu jamaa alikuwa na ngoma kali sana kama vile Latifa ,Si uliniambia ,Sagablasha nk lakini baada ya kuachana na mzee talent tu basi akapotea mazima kwenye mziki .


2)Z _Anto

Screenshot_2017-05-18-23-50-13_1.jpg
huyu jamaa alitamba sana na ngoma kali kama vile binti kiziwi ,Jini jini,nk lakini baada ya kukorofishana na tale basi huo ndio ukawa mwisho wake wa muziki ,alipoachana na tale Z _ANTO alihamia kwenye kuimba taarabu ambako alizidi kujichimbia kaburi lake kwenye ramani ya mziki na mwisho wa siku hata aliporudi kwenye kuimba bongo fleva bado hakufanikiwa kufanya lolote lile .

Mbali na Z anto wengine waliopotea kwenye mziki ni kama vile

3)Pingu na mwenzake Deso

4)Spark

5)PNC ingawaje mwanzoni alijitahidi lakini baada ya muda akapotea mazima.


Hivyo basi napenda kutoa angalizo kwa bwana mdogo Diamond Platinumz awe makini sana na huyu jamaa kwani wakiachana tu jamaa hatotaka faida alizokuwa anapata kipindi yupo na mondi mwengine azipate hivyo basi atafanya juu chini kumpoteza mondi


Huu ni mtazamo tu naweza kuwa nipo sahihi au lah


Hivyo kwa namna moja au nyingine ningependa nisikie/kuona mawazo kutoka kwenu wanajamvi wenzangu.
 
Soko letu la muziki kuwa na watu wachache ambao ndiyo wanaamua nini kitokee na kutolipa wasanii ipasavyo ndiyo kimepoteza hao wasanii.
Wizkid, Skales na Runtown mwaka juzi/ jana waligombana na wanaowamiliki lakini hakuna aliyeyumba kwakua kwao muziki unalipa haswa na hauja?shikwa na kikundi kidogo cha watu.
 
Huyu Jamaa inaonekana ana roho ya kwanini!
Kwasababu nilisikiliza mahojiano ya yule designer wa diamond licha ya kuwa hakumtaja direct ila inaonekana yeye ndio aliyemuwekea ngumu!
Yupo mwingine anaitwa Alma's mzambele naye wanalalamika kama tale ndio tatizo!
 
Wala sio uchawi ni akili tu nyingi anazo, ametengeneza system fulani ya menejimenti na kila anaekuja anataka aifate hiyo hiyo matokeo yake wanakuwa watumwa wa taleism . Hakuna meneja ataefanikiwa kumzidi Tale na Fella mpaka waje na system yao ya menejimenti.
 
[QUOTE="Hance Mtanashati, post: 21188922, member: 400241Hivyo kwa namna moja au nyingine ningependa nisikie/kuona mawazo kutoka kwenu wanajamvi wenzangu.[/QUOTE]

Sasa unataka usikie maoni kutoka kwetu na ilhali unaemshauri ni diamond[emoji15] [emoji15] [emoji15]
 
Wala sio uchawi ni akili tu nyingi anazo, ametengeneza system fulani ya menejimenti na kila anaekuja anataka aifate hiyo hiyo matokeo yake wanakuwa watumwa wa taleism . Hakuna meneja ataefanikiwa kumzidi Tale na Fella mpaka waje na system yao ya menejimenti.
Walianzisha iPhone ila sasa Android imeizd. Alichonacho Tale kisichoigika ni nini?
 
Wala sio uchawi ni akili tu nyingi anazo, ametengeneza system fulani ya menejimenti na kila anaekuja anataka aifate hiyo hiyo matokeo yake wanakuwa watumwa wa taleism . Hakuna meneja ataefanikiwa kumzidi Tale na Fella mpaka waje na system yao ya menejimenti.
hajui kiingereza zaidi ya abc ila nashangaa anawapelekesha
 
Kila mtu huwa ana kilele katika mafanikio yake. Na ukishafika katika kilele, either ukazane ubakie hapo kwa muda ama ushuke chini.

Ndivyo ilivyotokea kwa wasanii ambao unawazungumzia. Kuanzia kwa Z Anton mpaka kwa MB Doggy, huenda nyakati hizo ndizo kilele cha mafanikio yao kimuziki.

Hata kama Tale angeliendelea kuwa meneja wao, lazima tu wangeshuka.

Vivyo hivyo kwa Diamond, yupo katika kilele ama anaelekea kufika. Baada ya muda naye ataporomoka hata kama Tale na Salaam wataendelea kuwa meneja wake. Ndivyo ilivyo.
 
Kila mtu huwa ana kilele katika mafanikio yake. Na ukishafika katika kilele, either ukazane ubakie hapo kwa muda ama ushuke chini.

Ndivyo ilivyotokea kwa wasanii ambao unawazungumzia. Kuanzia kwa Z Anton mpaka kwa MB Doggy, huenda nyakati hizo ndizo kilele cha mafanikio yao kimuziki.

Hata kama Tale angeliendelea kuwa meneja wao, lazima tu wangeshuka.

Vivyo hivyo kwa Diamond, yupo katika kilele ama anaelekea kufika. Baada ya muda naye ataporomoka hata kama Tale na Salaam wataendelea kuwa meneja wake. Ndivyo ilivyo.
uliosema ni kweli mkuu maana diamond wa 2015 sio wa 2017 kila siku graph inashuka.ndo ubaya wa ustaa hawa iweje utashuka tu .so ni vizuri kutumia muda wako vizuri ukiwa kileleni
 
hao jamaa ukitoka kwao, utaletewa fitna kwenye media, show hutapata za maana, yaani ndo mwisho wako hao jamaa wanacontrol muzik na entertainment media
 
Back
Top Bottom