Katoto Kadogo
Member
- Jul 3, 2015
- 28
- 72
Tanzania inatimiza miaka 32 tangu kurejeshwa rasmi kwa siasa za vyama vya vingi nchini.
Julai, 1992 Tanzania iliweka wazi kurejesha mfumo wa siasa za vyama vingi, ambapo mwaka 1995 ulifanyika Uchaguzi Mkuu wa kwanza ulioshirikisha vyama vingi vya siasa.
Mfumo wa vyama vingi, umesaidia kuwaleta Wananchi pamoja na kuhamasisha ufuatiliaji wa mwenendo, kauli, matamko ya viongozi, sera na sheria mbalimbali nchini. Kubwa zaidi ni suala la uwajibikaji ambapo Wabunge kutoka vyama mbalimbali walitumia Bunge kuibua mijadala ya kitaifa kupitia vikao rasmi vya Bunge na kuikosoa Serikali bila kupepesa macho.
Tangu kuasisiwa kwa siasa za vyama vingi, kama wengi wanavyopenda kuita ‘siasa za mageuzi’ kulikuwa na mwelekeo wa ukuaji mzuri wa uendeshaji wa siasa na vyama vya siasa. Ushiriki wa Wananchi kwenye siasa na uongozi, ulikuwa unapiga hatua mbele mwaka hadi mwaka, changamoto zilizokuwepo wakati siasa za vyama vingi ziliporejeshwa tena, zilikuwa zinatatuliwa kutokana na maoni ya wadau mbalimbali.
Hata hiyvo, tangu 2020 tumerudi nyuma kabisa na tunashuhudia Bungeni kukiwa na idadi kubwa ya Wabunge kutoka Chama Tawala (CCM) ambapo wengi wao wamepitishwa bila kupingwa katika Majimbo mengi nchini.
Hali hii imepingwa vibaya na wananchi wengi ambapo wamedai ya kuwa kushindwa kwa wapinzani kwenye majimbo hasa mwaka 2020 kulitokana na figisu zilizofanywa na Chama Tawala huku Tume ya Uchaguzi na hata Ofisi ya Msajili wa Vyama wakifumbia macho.
Haki ya kuanzisha chama cha siasa ni haki ya Msingi na chama kinaweza kuundwa kwa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Vyama vya Siasa kwa ajili ya kuendeleza malengo na madhumuni ambayo hayako kinyume na Katiba ya JMTZ, Katiba ya Zanzibar au sheria nyingine yoyote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kifungu cha 6(1) cha Sheria ya Vyama vya Siasa.
Julai, 1992 Tanzania iliweka wazi kurejesha mfumo wa siasa za vyama vingi, ambapo mwaka 1995 ulifanyika Uchaguzi Mkuu wa kwanza ulioshirikisha vyama vingi vya siasa.
Mfumo wa vyama vingi, umesaidia kuwaleta Wananchi pamoja na kuhamasisha ufuatiliaji wa mwenendo, kauli, matamko ya viongozi, sera na sheria mbalimbali nchini. Kubwa zaidi ni suala la uwajibikaji ambapo Wabunge kutoka vyama mbalimbali walitumia Bunge kuibua mijadala ya kitaifa kupitia vikao rasmi vya Bunge na kuikosoa Serikali bila kupepesa macho.
Tangu kuasisiwa kwa siasa za vyama vingi, kama wengi wanavyopenda kuita ‘siasa za mageuzi’ kulikuwa na mwelekeo wa ukuaji mzuri wa uendeshaji wa siasa na vyama vya siasa. Ushiriki wa Wananchi kwenye siasa na uongozi, ulikuwa unapiga hatua mbele mwaka hadi mwaka, changamoto zilizokuwepo wakati siasa za vyama vingi ziliporejeshwa tena, zilikuwa zinatatuliwa kutokana na maoni ya wadau mbalimbali.
Hata hiyvo, tangu 2020 tumerudi nyuma kabisa na tunashuhudia Bungeni kukiwa na idadi kubwa ya Wabunge kutoka Chama Tawala (CCM) ambapo wengi wao wamepitishwa bila kupingwa katika Majimbo mengi nchini.
Hali hii imepingwa vibaya na wananchi wengi ambapo wamedai ya kuwa kushindwa kwa wapinzani kwenye majimbo hasa mwaka 2020 kulitokana na figisu zilizofanywa na Chama Tawala huku Tume ya Uchaguzi na hata Ofisi ya Msajili wa Vyama wakifumbia macho.
Haki ya kuanzisha chama cha siasa ni haki ya Msingi na chama kinaweza kuundwa kwa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Vyama vya Siasa kwa ajili ya kuendeleza malengo na madhumuni ambayo hayako kinyume na Katiba ya JMTZ, Katiba ya Zanzibar au sheria nyingine yoyote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kifungu cha 6(1) cha Sheria ya Vyama vya Siasa.
Hakuna chama kipya tangu miaka 10 iliyopita
Hata hivyo, imepita takriban miaka 10 tangu chama cha mwisho cha siasa kusajiliwa.
ACT Wazalendo kilipewa usajili wa kudumu mnamo tarehe 5 Mei 2014 hakuna chama kingine chochote cha Siasa kilichopewa usajili ama wa muda au wa kudumu. Hii ni kwa mujibu wa tovuti ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Je, ni kweli kwamba tangu Mei 2014, watanzania waliotaka kuanzisha vyama? Kwanini tovuti ya Msajili wa Vyama haina taarifa za walioomba na kama walikataliwa na sababu za kukataliwa kwao ili wengine wasifanye makosa?
Inatafakarisha sana!
ACT Wazalendo kilipewa usajili wa kudumu mnamo tarehe 5 Mei 2014 hakuna chama kingine chochote cha Siasa kilichopewa usajili ama wa muda au wa kudumu. Hii ni kwa mujibu wa tovuti ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Je, ni kweli kwamba tangu Mei 2014, watanzania waliotaka kuanzisha vyama? Kwanini tovuti ya Msajili wa Vyama haina taarifa za walioomba na kama walikataliwa na sababu za kukataliwa kwao ili wengine wasifanye makosa?
Inatafakarisha sana!
Alichosema Jaji Mutungi mwaka 2023
Itakumbukwa tarehe 17 Julai 2023, Msajili wa Vyama, Jaji Francis Mutungi wakati akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kufungua kikao kazi kati ya ofisi yake na viongozi wa vyama, alisema ofisi yake imepokea maombi 18 ya vyama vipya vya siasa na kwamba wanaendelea na mchakato wa usajili. Aidha, alisema wamesitisha kwa muda usajili wa vyama vipya ili kupisha uhakiki wa vyama vilivyopo.
Lakini, utaratibu wa Usajili wa Vyama unamtaka Msajili kuweka tangazo la usajili. Kwa mujibu wa Kanuni za Usajili na Ufuatiliaji wa Vyama vya Siasa, Kifungu cha 4 (a) “Msajili atachapisha tangazo katika angalau magazeti mawili yanayosambazwa kote nchini, moja likiwa la Kiswahili na lingine la Kiingereza, akialika pingamizi kutoka kwa mtu yeyote au chama chochote cha kisiasa kuhusu jina, alama au rangi ya chama kinachotafuta usajili wa muda au jambo lolote lingine linalohusiana na usajili wa chama cha kisiasa husika;”
Tangu Jaji Mutungi aseme kuna vyama 18 vimeomba usajili, hakuwahi kuweka tangazo kwenye gazeti lolote kuhusu vyama hivyo. Jambo linaloleta ukakasi sana kwetu Wananchi.
Je, kuna hujuma katika ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuzuia usajili wa vyama vipya?
Sisi tunataka majibu yanayoeleweka kutoka kwa Ofisi hiyo. Tunataka kufahamu haya;
1. Kwanini tangu chama cha ACT Wazalendo kisajiliwe hakuna chama kingine kimesajiliwa licha ya kuwepo kwa vyama vilivyoomba usajili
2. Kwanini Msajili hajawahi kutangaza kuhusu vyama vinavyotaka kujisajili kama Kanuni ya Usajili inavyomtaka kufanya?
3. Kwanini hakuna uwazi katika kutangaza vyama vilivyoomba usajili, na kusema sababu zilizofanya kukosa usajili?
Lakini, utaratibu wa Usajili wa Vyama unamtaka Msajili kuweka tangazo la usajili. Kwa mujibu wa Kanuni za Usajili na Ufuatiliaji wa Vyama vya Siasa, Kifungu cha 4 (a) “Msajili atachapisha tangazo katika angalau magazeti mawili yanayosambazwa kote nchini, moja likiwa la Kiswahili na lingine la Kiingereza, akialika pingamizi kutoka kwa mtu yeyote au chama chochote cha kisiasa kuhusu jina, alama au rangi ya chama kinachotafuta usajili wa muda au jambo lolote lingine linalohusiana na usajili wa chama cha kisiasa husika;”
Tangu Jaji Mutungi aseme kuna vyama 18 vimeomba usajili, hakuwahi kuweka tangazo kwenye gazeti lolote kuhusu vyama hivyo. Jambo linaloleta ukakasi sana kwetu Wananchi.
Je, kuna hujuma katika ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuzuia usajili wa vyama vipya?
Sisi tunataka majibu yanayoeleweka kutoka kwa Ofisi hiyo. Tunataka kufahamu haya;
1. Kwanini tangu chama cha ACT Wazalendo kisajiliwe hakuna chama kingine kimesajiliwa licha ya kuwepo kwa vyama vilivyoomba usajili
2. Kwanini Msajili hajawahi kutangaza kuhusu vyama vinavyotaka kujisajili kama Kanuni ya Usajili inavyomtaka kufanya?
3. Kwanini hakuna uwazi katika kutangaza vyama vilivyoomba usajili, na kusema sababu zilizofanya kukosa usajili?