Kuna shida gani Tanzania ikitangaza rasmi kuisaidia Congo kupambana na M23? Tuna Viongozi wa namna gani?

Mkuu ulishawahi kuona bata amejivika mfuko wa plastic shingoni anavyokombia nakutapatapa..? basi ndo itakuwa hivyohivyo tukiingilia huo ugomvi!.
 
Unataka tufe njaa?? Tukamuliwe Kodi mpaka tubaki mbavu 2. Yanayoendelea Kongo sisi hatuna ubavu wa kuyatuliza. Unaweza kuhisi unapigana na M23 kumbe unapigana na mabepari wakubwa.
Sisi tunaweza kutoa mkopo in terms of man power.

Silaha tunanunua kwa fedha zao na kuwasaidia kukomboa eneo lao.
 
Sisi ni masikini wa kijitakia
Sasa kama watoto wanakaa chini bila madawati
Vyoo vya hospital ukiingia unaondoka na maradhi
Unategemea hizo hela za kuwalisha wanajeshi na vifaa vyao na silaha zitoke wapi?
Usilinganishe kamwe na US au Europeans ni mbingu na ardhi
 
Tatizo ni kwamba Kagame anaona jeshi lake ni kiboko sana hakuna nchi ya Africa inaweza kumpiga
Sidhani kama Kagame anaona jeshi lake ni kiboko sana, ila ni ukweli pia kwamba katika Africa mashariki Kagame ndiye unayeweza kusema kati ya watawala ni mwanamikakati bora zaidi wa kijeshi na geopolitics za ukanda huu kwa sasa.
 
Watu wanavyoona marekani anaenda kupigana Iraq na Afghanistan huko wanadhani anapenda vita kumbe kuna faida za kiuchumi?

Wanakula hela za marekani kuwanunulia ARV na kuwajengea vyoo wanafikiri zinapatikana na kodi tu za Wamarekani.

How comes tunashindwa kumsaidia Congo kwa kufikiria kufaidika kiuchumi?
 
Sidhani kama Kagame anaona jeshi lake ni kiboko sana, ila ni ukweli pia kwamba katika Africa mashariki Kagame ndiye unayeweza kusema kati ya watawala ni mwanamikakati bora zaidi wa kijeshi na geopolitics za ukanda huu kwa sasa.
Congo saivi wamefika mwisho kuhusu Kagame.

Endapo sisi leo tukiwasaidia hata nafasi yetu kwenye kutawala uchumi wa Congo itakuwa kubwa sana.

Wacongo wanahitaji sana mtu wa kuwasaidia. Hata kwa terms mbaya za mkopo wako sawa tu. Why hatutumii hii nafasi alafu JW wetu wanavunja matofali tu kwenye shughuli za uhuru?
 
Vita ya m23 na serikali ya congo ni ya kimkakati. Unaweza ambiwa leo kuwa, waasi wa m23 wamesalimisha silaha na makumi ya waasi wamejisalimisha,lakini kesho ukaambiwa tena goma na kivu yote zipo mikono mwa waasi wa m23.
 
Mkuu ulishawahi kuona bata amejivika mfuko wa plastic shingoni anavyokombia nakutapatapa..? basi ndo itakuwa hivyohivyo tukiingilia huo ugomvi!.
Hapana. Haitakuwa hivyo.

Nina uhakika tukitoa tamko hata leo. Kesho Congo wako tayari ku negotiate huo mkataba kwa any terms tutakazoweka.

Na kesho tu Rwanda ataufyatq.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…