Kuna shida gani Tanzania ikitangaza rasmi kuisaidia Congo kupambana na M23? Tuna Viongozi wa namna gani?

Kuna shida gani Tanzania ikitangaza rasmi kuisaidia Congo kupambana na M23? Tuna Viongozi wa namna gani?

Jeshi letu ingawa wanasiasa wanajaribu kuliingilia ila bado halijawa dhaifu.

Nakumbuka enzi zile tunatoa kichapo kwa M23 tulikuwa na vyuma kama Gen. Mwamunyange, Brig G. Mwakibolwa na mwanajeshi wangu bora kwa wakati wote Lt. General Paul Ignace Mella.
Sasahivi wakithubutu watachapika kweli kweli, Kagame amejipanga haswa kwenye hii vita.
 
Kujiingiza kwenye vita bila kuwa na manufaa ya moja kwa moja ni gharama kwa nchi na wananchi wako. Vita vya Uganda vilitugharimu miaka mingi baada ya vita.
 
Vita ya kagera tulifaidika na nini..
Tumlaumi Nyerere kwa siasa zake za ujamaa, ilibidi tuingie mkataba na Uganda, makampuni yetu yapige kazi miaka 100 kule, tungetegemeza utegemezi fulani hivi, tungehamishia viwanda vyao hapo Kagera n.k
 
Tumlaumi Nyerere kwa siasa zake za ujamaa, ilibidi tuingie mkataba na Uganda, makampuni yetu yapige kazi miaka 100 kule, tungetegemeza utegemezi fulani hivi, tungehamishia viwanda vyao hapo Kagera n.k
Kama tuna think tank kwenye hii nchi wakipitia uzi wangu na comment zangu. Kisha wakisoma comment yako na za wenye akili kubwa wachache waliochangia humu, wataelewa tunamaanisha nini!
 
Hii Mada ni bora kabisa, yaani M23 rebels ni Rwanda inataka kuongeza mipaka, ikimaliza Goma na kujizatiti lazima watakuja kuchukua Kigoma wakiwa na nguvu zaidi, hapa TZ haina namna inapaswa kuondoa wahuni hao kabla hawajajijenga zaidi Goma maana hata malori yetu yamekwama huko madereva roho mkononi bizness haziendi uchumi wetu unashuka, tunapaswa kuwafurusha kwa mgongo wa majeshi ya UN
 
Hao mabeberu ndo shida,eti kulinda amani na Hali m23 wanaua watu.
Kama ingekuwa siyo mabeberu Goma na maeneo yake yote yange kuwa shwari siku nyingi
Mabeberu yanafaidika na vita vya Congo Kwa asilimia 💯 % na ndio maaana huoni Cha maaana kule wakifanya
 
Back
Top Bottom