DOKEZO Kuna Shule Wanafunzi wanashinikizwa wasiende likizo ili Walimu wakusanye michango, Mamlaka husika toeni mwongozo

DOKEZO Kuna Shule Wanafunzi wanashinikizwa wasiende likizo ili Walimu wakusanye michango, Mamlaka husika toeni mwongozo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Wakati Shule zikiwa zinafungwa kwa kumaliza mwaka wa masomo lakini kuna baadhi ya Shule za msingi zinaratibu utaratibu wa Wanafunzi kutokwenda likizo badala yake wanashinikiza kuendelea na masomo katika utaratibu rasmi.

Mfano katika Shule ya Msingi Ndumbwi, iliyoko Mbezi Juu Jijini Dar es Salaam na Shule ya Msingi Africana iliyopo Salasala Watoto wa darasa la tatu ambao inaelezwa kwamba watahitimu masomo yao ya elimu ya msingi kwa kuishia darasa la sita wameambiwa ni lazima kuendelea kuhudhuria shuleni kama kawaida.

Hoja ambayo inaelezwa na Shule ni kwamba wanajitahidi kukimbizana na masomo ambayo wangetakiwa kuyasoma kufikia darasa la saba ili wawe wameyasoma yote wakija kuhitimu kwa kuishia darasa la sita.

Ilielezwa hivyohivyo kwenye likizo ya muhula uliopita Wanafunzi wakaendelea na masomo kama kawaida huku baadhi ambao hawakudhuria wakipewa adhabu.

Jambo la kushangaza Wanafunzi wanaelezwa ni lazima kwa kuwa mambo wanayofundishwa hayatarudiwa Shule zitakapofunguliwa, badala yake wanasema wataendeleza pale walipoishia kwa maana kwamba mambo yatakayofundishwa kipindi cha likizo yatahesabika kwenye utaratibu rasmi.

Licha hoja hizo lakini Wanafunzi wanatakiwa kuchangia Shilingi 500 kila siku kwa ajili ya kuwezesha masomo hayo. Jambo hilo linafanya wengi kujiuliza maswali bila majawabu rasmi na kuibua minongono.

Kama suala hilo linafanyika kwa msukumo wa hoja zilizopo hasa kukimbizana na utaratibu mpya wa kuhitimu elimu ya msingi, kwanini uathiri haki ya Wanafunzi kupata likizo kama taratibu zinavyoelekeza au utaratibu huo mpya umekuja na mabadiliko?

Kuwashinikiza Wanafunzi kwamba ni lazima kuendelea na masomo kwa kuwa hawatarudi nyuma kuwafundisha mambo ambayo watakuwa wamefundisha kipindi cha likizo ni kuwanyima haki yao muhimu.

Kama ni utaratibu rasmi wa kimasomo kama inavyodaiwa, kwanini Wanafunzi watozwe pesa za kila siku kuwezesha masomo hayo?

Sidhani kama Wazazi hawapendi Watoto wao wapate elimu, lakini sio sawa kuweka mazingira ya shinikizo ambayo ni kinyume na taratibu na yanayoweza kuathiri Wanafunzi, kuna wakati Wanafunzi wanahitaji kupata likizo ili kupata utulivu kwa kupumzika, kupata nishati mpya na hata kukaa na familia kushiriki stadi za maisha.

Wito wangu kwa mamlaka, ni vyema wakatoa maelekezo na msisitizo kwa Shule ambazo zinafanya hivyo au zinakusudia kufanya hivyo kuzingatia taratibu na miongozo bila kuathiri haki za Wanafunzi. Suala hili linafanyika katika Shule nyingi za Serikali hususani zilizopo Jijini Dar es Salaam.
 
Hata huko Mkuranga, Pwani, wanaendelea kusoma wanafunzi wa darasa la 3 na la 6,kwa wiki mbili.

Hii ni sera ya nchi au ni ma DEO wanajiamulia!!??
 
Walimu nao waneona wale kwa urefu wa kamba yao. Huu ujinga ulianza shule za biashara, watu wa serikali wakanogewa, na una back up ya watu wa wilayani kwa kuwa kuna 'mgao wao'.

Wale watetezi wa haki za watoto hutowasikia hapa - kwao kupumzika na kujifunza stadi za maisha si haki - kwao haki ni kutochapwa tu.

Watoto wanashindishwa shule kuliko wasomi wanavyoshinda maabara, na wakihitimu ili hali hawana stadi za mtaani wanaambiwa kwa kebehi 'jiajiri', ili hali muda wote alikuwa anakokotoa X.

Hizo shule wanasoma maskini kama wa Namtumbo - watoto wanaolelewa na wazee, watoto wa wauza maandazi, n.k ili hali wapo mitaa yenye ahueni kiuchumi.
 
Wakati Shule zikiwa zinafungwa kwa kumaliza mwaka wa masomo lakini kuna baadhi ya Shule za msingi zinaratibu utaratibu wa Wanafunzi kutokwenda likizo badala yake wanashinikiza kuendelea na masomo katika utaratibu rasmi.

Mfano katika Shule ya Msingi Ndumbwi, iliyoko Mbezi Juu Jijini Dar es Salaam na Shule ya Msingi Africana iliyopo Salasala watoto wa darasa la tatu ambao inaelezwa kwamba watahitimu masomo yao ya elimu ya msingi kwa kuishia darasa la sita wameambiwa ni lazima kuendelea kudhuria shuleni kama kawaida.

Hoja ambayo inaelezwa na Shule ni kwamba wanajitahidi kukimbizana na masomo ambayo wangetakiwa kuyasoma kufikia darasa la saba ili wawe wameyasoma yote wakija kuhitimu kwa kuishia darasa la sita.

Ilielezwa hivyo hivyo kwenye likizo ya muhula uliopita Wanafunzi wakaendelea na masomo kama kawaida huku baadhi ambao hakudhuria wakipewa adhabu.

Jambo la kushangaza Wanafunzi wanaelezwa kuwa ni lazima kwa kuwa mambo wanayofundishwa hayatarudiwa Shule zitakapofunguliwa, badala yake wanasema wataendeleza pale walipoishia kwa maana kwamba mambo yatakayofundishwa kipindi cha likizo yatahesabika kwenye utaratibu rasmi.

Licha hoja hizo lakini Wanafunzi wanatakiwa kuchangia Shilingi 500 kila siku kwa ajili ya kuwezesha masomo hayo. Jambo hilo linafanya wengi kujiuliza maswali bila majawabu rasmi na kuibua minongono.

Kama suala hilo linafanyika kwa msukumo wa hoja zilizopo hasa kukimbizana na utaratibu mpya wa kuhitimu elimu ya msingi, kwanini uathiri haki ya Wanafunzi kupata likizo kama taratibu zinavyoelekeza au utaratibu huo mpya umekuja na mabadiliko?

Kuwashinikiza Wanafunzi kwamba ni lazima kuendelea na masomo kwa kuwa hawatarudi nyuma kuwafundisha mambo ambayo watakuwa wamefundisha kipindi cha likizo ni kuwanyima haki yao muhimu.

Na kama ni utaratibu rasmi wa kimasomo kama inavyodaiwa, kwanini Wanafunzi watozwe pesa za kila siku kuwezesha masomo hayo?

Sidhani kama Wazazi hawapendi Watoto wao wapate elimu, lakini sio sawa kuweka mazingira ya shinikizo ambayo ni kinyume na taratibu na yanayoweza kuathiri Wanafunzi, kuna wakati Wanafunzi wanahitaji kupata likizo ili kupata utulivu kwa kupumzika, kupata nishati mpya na hata kukaa na familia kushiriki stadi za maisha.

Wito wangu kwa mamlaka, ni vyema wakatoa maelekezo na msisitizo kwa Shule ambazo zinafanya hivyo au zinakusudia kufanya hivyo kuzingatia taratibu na miongozo bila kuathiri haki za Wanafunzi. Suala hili linafanyika katika Shule nyingi za Serikali hususani zilizopo Jijini Dar es Salaam.
Walimu waache uhunu,kipindi cha likizo ndio wakati ambao watoto wanatakiwa wakawajue babu zao,shangazi zao,hami zao,na wafundishwe kazi za nyumbani na mengineyo, walioweka utaratibu wa likizo hawakuwa wajinga,


Halafu ukiwasikiliza kama vile kweli wana malengo mazuri na watoto,kumbe ni kutaka kupiga pesa, mfano kuna shule darasa la nne wapo karibia mia tatu,ukipiga hesabu iyo mia Tano kwa idadi iyo ni Laki na Nusu,
 
Elimu ni gharama weka pesa upate pesa weka muda upate mafanikio

Mwanao unaweza mchukua tu uondoke naye Kama yupo vizuri

Ila mtu Kama Mimi ambaye sipendi usumbufu akae uko atakuja kula xmass na mwaka mpya !!
Basi likizo zifutwe ili walimu wapige pesa na watoto wasome zaidi, mi sioni umuhimu wa likizo kwa wanafunzi!!
 
Huu upuuzi nilishaukataa kitambo sana. Mkuu wa shule hawezi kunibakisha shuleni hata siku moja wakati ni likizo ya wanafunzi waende wakapumzike wajiandae na muhula mpya wa masomo. Kufundisha sana kutaka sifa ni ujinga unachosha wanafunzi
 
Nilidhani ni kwa mwezi wa sita tu!!! Mpk December kumbe!
walimu tuache njaa, utajiri hauji kwa michango ya buku buku 😁😁😁

Au kuna walimu wakuu wanautafuta uafisa elimu nini?!
 
Eti unakuta darasa la tatu na la sita hawafungi, haohao wakiingia la nne na la saba mwakani hawatafunga likizo zote ni kufululiza kufundisha tu mpaka kunako mitihani ya taifa. Huu mtindo ni wa kipuuzi na haupo katika kanuni za ufundishaji
 
Elimu ni gharama weka pesa upate pesa weka muda upate mafanikio

Mwanao unaweza mchukua tu uondoke naye Kama yupo vizuri

Ila mtu Kama Mimi ambaye sipendi usumbufu akae uko atakuja kula xmass na mwaka mpya !!
Kwahiyo watoto wasipewe likizo?
 
Eti unakuta darasa la tatu na la sita hawafungi, haohao wakiingia la nne na la saba mwakani hawatafunga likizo zote ni kufululiza kufundisha tu mpaka kunako mitihani ya taifa. Huu mtindo ni wa kipuuzi na haupo katika kanuni za ufundishaji
Hapo niupigaji tu wa hela.
 
Huu upuuzi nilishaukataa kitambo sana. Mkuu wa shule hawezi kunibakisha shuleni hata siku moja wakati ni likizo ya wanafunzi waende wakapumzike wajiandae na muhula mpya wa masomo. Kufundisha sana kutaka sifa ni ujinga unachosha wanafunzi
Hawataki sifa wanataka hela
 
Sijui ni kitu gani au ni mipango ya maofisa elimu, kila ofisa elimu ana mipango yake? Kuna halmashauri wanafunzi wa darasa la nne walipomaliza mitihani yao ya taifa hawakurudi shuleni mpaka matokeo yao yatoke ndio watarudi hapo mwakani kuendelea na darasa la tano. Ila kuna halmashauri watoto wa darasa hilo waliendelea kwenda shuleni kama kawaida sambamba na wenzao mpaka walipohitimisha muhula wa pili na kufunga shule wiki iliyopita hadi shule zitakapofunguliwa tena kwa muhula mpya wa masomo. Inakuwaje wanafunzi wafunge na wengine waendelee kwenda shule wakati ratiba ya mihula ni moja nchi nzima?
 
Huu ni ushenzi.
Ina maana wizara na serikali ilipopanga hawa watoto waishie std 6 hawakulioni hilo kuwa masomo ni mengi kuliko muda ?
Huu ushenzi wa watoto kusoma bila kupumzika ni wa dunia 4 ambako wameshindwa kuvumbua hata dodoki la kuoshea vyombo.
 
Wakati Shule zikiwa zinafungwa kwa kumaliza mwaka wa masomo lakini kuna baadhi ya Shule za msingi zinaratibu utaratibu wa Wanafunzi kutokwenda likizo badala yake wanashinikiza kuendelea na masomo katika utaratibu rasmi.

Mfano katika Shule ya Msingi Ndumbwi, iliyoko Mbezi Juu Jijini Dar es Salaam na Shule ya Msingi Africana iliyopo Salasala Watoto wa darasa la tatu ambao inaelezwa kwamba watahitimu masomo yao ya elimu ya msingi kwa kuishia darasa la sita wameambiwa ni lazima kuendelea kuhudhuria shuleni kama kawaida.

Hoja ambayo inaelezwa na Shule ni kwamba wanajitahidi kukimbizana na masomo ambayo wangetakiwa kuyasoma kufikia darasa la saba ili wawe wameyasoma yote wakija kuhitimu kwa kuishia darasa la sita.

Ilielezwa hivyohivyo kwenye likizo ya muhula uliopita Wanafunzi wakaendelea na masomo kama kawaida huku baadhi ambao hawakudhuria wakipewa adhabu.

Jambo la kushangaza Wanafunzi wanaelezwa ni lazima kwa kuwa mambo wanayofundishwa hayatarudiwa Shule zitakapofunguliwa, badala yake wanasema wataendeleza pale walipoishia kwa maana kwamba mambo yatakayofundishwa kipindi cha likizo yatahesabika kwenye utaratibu rasmi.

Licha hoja hizo lakini Wanafunzi wanatakiwa kuchangia Shilingi 500 kila siku kwa ajili ya kuwezesha masomo hayo. Jambo hilo linafanya wengi kujiuliza maswali bila majawabu rasmi na kuibua minongono.

Kama suala hilo linafanyika kwa msukumo wa hoja zilizopo hasa kukimbizana na utaratibu mpya wa kuhitimu elimu ya msingi, kwanini uathiri haki ya Wanafunzi kupata likizo kama taratibu zinavyoelekeza au utaratibu huo mpya umekuja na mabadiliko?

Kuwashinikiza Wanafunzi kwamba ni lazima kuendelea na masomo kwa kuwa hawatarudi nyuma kuwafundisha mambo ambayo watakuwa wamefundisha kipindi cha likizo ni kuwanyima haki yao muhimu.

Kama ni utaratibu rasmi wa kimasomo kama inavyodaiwa, kwanini Wanafunzi watozwe pesa za kila siku kuwezesha masomo hayo?

Sidhani kama Wazazi hawapendi Watoto wao wapate elimu, lakini sio sawa kuweka mazingira ya shinikizo ambayo ni kinyume na taratibu na yanayoweza kuathiri Wanafunzi, kuna wakati Wanafunzi wanahitaji kupata likizo ili kupata utulivu kwa kupumzika, kupata nishati mpya na hata kukaa na familia kushiriki stadi za maisha.

Wito wangu kwa mamlaka, ni vyema wakatoa maelekezo na msisitizo kwa Shule ambazo zinafanya hivyo au zinakusudia kufanya hivyo kuzingatia taratibu na miongozo bila kuathiri haki za Wanafunzi. Suala hili linafanyika katika Shule nyingi za Serikali hususani zilizopo Jijini Dar es Salaam.
We mpe tu mwanao hizo jero jero bwana mambo yasiwe mengi. Mzazi punguza gubu jamani.
 
Back
Top Bottom