Uchaguzi 2020 Kuna tatizo kidogo na namna CHADEMA wanavyonadi sera zao. Ubunifu ni kidogo sana na wanashindwa kwenda sawa na matarajio ya Umma

Uchaguzi 2020 Kuna tatizo kidogo na namna CHADEMA wanavyonadi sera zao. Ubunifu ni kidogo sana na wanashindwa kwenda sawa na matarajio ya Umma

William Mshumbusi

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
1,761
Reaction score
2,391
Ingawa mgombea wao Ameanza kunadi Sera zao, lakini hayapo uzito Mambo yanayowagusa wengi. NI Kama anasema tu juu juu na kukazia maswala binafsi yanayomuhusu yeye na watu wa chama chake.

Ajira, kilimo na biashara kila moja kinaweza kumuathiri kila mtu Ila mgombea anashindwa kuonesha kila ajenda NI ya kitaifa na hivyo kutoa ahadi za makundi makundi.

-Mfano mfumo mzuri wa haki na malipo kwa watumishi wa imma na binafsi utasaidia Sana kuweka fedha nyingi mtaani zitakazo wasaidia wakulima na mafundi kupata Bei Bora ya huduma na bidhaa zao.

- sekta ya kilimo Cha biashara na chakula ikilindwa. Wakulima wakipata malipo ya haki na wakati itainua uzalishaji wa mazao husika hivyo kupata fedha za kigeni za kutosha kuagiza bidhaa nje na kujenga uchumi.

-mfumo mbovu wa Kodi haumuumizi tu mfanyabiashara. humuuniza mlaji wa mwisho na ndio maana nchi jirani bidhaa Bei chini Kama Uganda , Burundi na Ata Kenya.

Lazima mgombea atoe hotuba za mifano mfano ulinganisho wa Bei za sukari au simenti tz na Uganda, Tanzania na Malawi.

Lazma abinu mbinu kuwafikia wapiga kura kwa njia mbalimbali. Matangazo mafupi ya dk 1 yenye Sera na ahadi za mgombea

Kuchapisha matangazo mafupi ya vipeperushi vyenye Sera na ahadi na kuviuza kila Kona.

Kuepuka lugha za hasira na kebehi kwa Viongozi wengine.

Kurekodi audio na video fupi zenye kero, Sera na ahadi na kuzisambaza kwa njia ya mitandao ya kijamii.

Kila kinachoandaliwa kizingatie lugha yenye staha, iepuke Takwimu zisizo sahihi.

Msisite kuwasemea wasanii wote adha wanazopitia.
 
Sema hawaendi sawa na matarajio yako sio umaa
 
Ingawa mgombea wao Ameanza kunadi Sera zao, lakini hayapo uzito Mambo yanayowagusa wengi. NI Kama anasema tu juu juu na kukazia maswala binafsi yanayomuhusu yeye na watu wa chama chake...

Hoja nzuri.

Mgombea lazima a fine tune ujumbe wake kadiri muda unavyokwenda.

Na sisi mashabiki na wapenzi wa vyama mbadala tuchukue jukumu la kuwa wasambazaji wa ilani za vyama vyetu.
 
Ingawa mgombea wao Ameanza kunadi Sera zao, lakini hayapo uzito Mambo yanayowagusa wengi. NI Kama anasema tu juu juu na kukazia maswala binafsi yanayomuhusu yeye na watu wa chama chake.

Ajira, kilimo na biashara kila moja kinaweza kumuathiri kila mtu Ila mgombea anashindwa kuonesha kila ajenda NI ya kitaifa na hivyo kutoa ahadi za makundi makundi..
CC Yeriko Nyerere
 
Back
Top Bottom