Kuna Timu Moja nchini Tanzania Mashabiki wake pamoja na Wanachama wao wakiitwa 'Mafuriko Sports Club' wasiwe wanakataa tafadhali

Nilikuwa nampenda sana huyu Mwamba wa Lusaka, kilichonifanya nimtoe thamani ni mechi ya tarehe 08 Machi, 2020 yaani alicheza hovyo kabisa. Mara awakanyage kwa makusudi wachezaji wa timu pinzani, mara apoteze mpira kizembe. Yaani alinifanya nimchukie kuanzia siku hiyo.
 
Chama anaondoka Mikiani kwa sababu Morrisson effects mkamshutumu alicheza chini ya kiwango..Mbona Kashata alishindwa kucheza mkamtoa nje...Hakuna kiungo wa Mikia anayeweza kumweka nje kiungo yoyote wa Yanga...Bangladesh nyie
 
Hawa vyura si ndio walikuwa wanasema chama so chochote pia Simba inaua vipaji wakisahau Dilunga alianzia kwao wakamwacha Leo Yuko Simba wanamwona nzuri wanaweza kumchukua Ila tukiwafunga wasilalamike tunawahujumu sababu ya wachezaji waliotoka Simba
Mna wachezaji 3 waliokua Yanga msimu uliopita,halafu msimu huu Yanga kachukua points 4 kwenu 😂
 
Huu ni wakati wa mavuno kwa wachezaji na mameneja/mawakala wao. Mameneja na wachezaji wajanja sasa hivi wanacheza na saikolojia ya viongozi kupitia vyombo vya habari kwa kuzusha timu fulani inanihitaji na iwapo mkataba wake unakaribia kwisha ndio balaa kabisa atataja na dau au ataleta hata mkataba wa awali aliopewa na timu pinzani. Basi kuanzia hapo ndio hizi sarakasi tunazoziona huku magazetini na kwenye "media" kwa ujumla wake.

Kama kumbu kumbu zangu zipo vizuri mwaka jana Simba ilitutangazia kuwa Chama kaongeza mkataba. Iwapo kweli Simba walimuongezea Chama mkataba na haikuwa kuuhadaa umma wa watanzania na dunia kwa ujumla basi sioni sabbabu ya Simba kupaniki. Ifike wakati sasa hivi vilabu vikue viachane na mambo ya kizamani. Kama Chama ana mkataba na Simba ni vizuri sasa wakawa subiri hao Yanga waje mezani wawape dau lake halafu wawaruhusu Yanga wakazungumze maslahi na mchezaji kisha Yanga kama kweli wana hiyo ya kumsajili Chama pesa waweke mzigo mezani wamchukue Chama msimbazi wamwamishie Jangwani.

Ni wakati sasa wa hivi vilabu kujifunza kuwapa mikataba mirefu wachezaji wanaowaona kama hazina kwenye timu zao ili timu ikifika bei wamuuze kwa bei nzuri kiasi waweze kumnunua mchezaji/wachezaji wenye uwezo sawa au zaidi ya huyo waliomuuza. Na iwapo mchezaji atakataa kuongeza mkataba mrefu mpaka mkataba wa mwanzo ufike ukingoni ni dhahiri kuwa mchezaji huyo anajiandaa kuondoka mwishoni mwa msimu kwa hiyo vilabu vyetu viwe vinajiandaa kutafuta mbadala wake mapema ili ikifika mwishoni mwa msimu visichanganyikiwe pale mchezaji huyo anapoamua kuondoka rasmi.

Na tatizo kubwa la hivi vilabu vyetu huwa havifanyi "scouting" ya wachezaji. Naamini kabisa siku ambayo hizi timu kubwa mbili zitakapoamua kuwa na timu za "scouting" kwa ajili ya usajili na kuanza kusajili kutokana na mahitaji ya timu badala ya mihemuko basi kuanzia hapo sarakasi hizi za usajili kwenye "media" hazitakuwepo. Na hili la kuviziana mara Simba wanamtaka Tshishimbi na Morison nao Yanga wanataka kuwasajili Chama na Dilunga nalo litakuwa limekwisha.

Hizi timu ziumize vichwa kwenye usajili. Sio lazima umuone Morison Yanga au Chama Simba ndio uanze kumrubuni umsajili wakati ni jambo la uhakika kabisa ukizuunguka tu hapa East and Central Africa utawapata wachezaji wengi tu wanaowakaribia viwango vyao au hata sawa na wao. Na hizi timu zetu zijifunze kuwa wakifanya usajili mapema wakati ligi inaendelea watafanya usajili kwa gharama ndogo lakini wakisubiri mwisho mwa msimu wataendelea kulipa pesa nyingi tu.
 
Kuna msomi alisikika akisema ukitaka kuwa mwehu Tanzania shabikia hizi timu mbili, utajikuta uko kijiweni unabishana na watu siku nzima huku hauna hili wala lile kuhusu kutafuta kazi. Mwisho wa siku unaanza kulia na kuilalamikia serikali kuwa hakuna kazi wakati ajira za kujiajiri mwenyewe zipo kibao.
 
Mna wachezaji 3 waliokua Yanga msimu uliopita,halafu msimu huu Yanga kachukua points 4 kwenu 😂

Hivi Simba ina point ngapi na Yanga ana ngapi vileee? Sir Alex Ferguson aliwahi kusema, yeye hajali kufungwa na Liverpool anachojali yeye ni kuwa bingwa tu na Liver aliendelea kuwa teja wa Man U.
 
Mechi moja na ukaamua kumtoa "thamani"
Huwa unafuatilia mpira?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi Simba ina point ngapi na Yanga ana ngapi vileee? Sir Alex Ferguson aliwahi kusema, yeye hajali kufungwa na Liverpool anachojali yeye ni kuwa bingwa tu na Liver aliendelea kuwa teja wa Man U.
Morrison effect bado iko kichwani,Yanga ainunuliki mtanunua kwa hizo timu zingine kupata point,kukuakishieni kama mnanunu tumechukua point 4 kwenu sababu Yanga imeziba mianya ya rushwa,timu lenu bovu bila tigo pesa lingekua kwenye janga la kushuka daraja,hapa tulipo Yanga africans tunajiuliza mpaka leo ile droo ya jan mliipataje kama si yule mama mwamuzi kuwapa penalti
 


Mko na point ngapi nyuma ya Simba, hujajibu swali. Katika msimamo wa ligi, nyie ni wa ngapi pia?
 
Mko na point ngapi nyuma ya Simba, hujajibu swali. Katika msimamo wa ligi, nyie ni wa ngapi pia?
Mbona amekujibu, ungetulia vizuri ungemuelewa! Yaani ukitoa pointi mlizopata kwa kuhonga marefa na wachezaji wa timu pinzani ongeza na mbeleko ya Karia, sasa hivi mngekuwa nyuma ya Yanga kwa pointi zaidi ya 10!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gsm katenga bilioni moja na nusu ya usajili na kulipwa madeni nikiangalia madeni ya yanga Kuna papaa zahera, chirwa, Dante, juma Abdul na wengineo walishalipwa Sana Sana yanga wanaweza kubaki na milioni 150 za usajili Kama tshishimbi anataka milioni 180 asajili sijui watasajili nani
 
Una matatizo wewe Mikia FC toka 8 March tulivyokupiga kimoko.
 
Mashabiki Wa Simba Mliokaa Jukwaa La Walalahoi Leo Taifa Mmesababisha NIWAFUNGISHENI. - JamiiForums

Kwanza Kabisa Napenda Kuchukua FURSA Hii Adhimu Kuwapongeza Wana Yanga Kwa Kutufunga Leo Simba Magoli Mawili Kwa Nunge Japo Kwa MAUDHI YALE NILIYOFANYIWA Na MASHABIKI Wa SIMBA MAPOPOMA Waliokaa Jukwaa La WALALAHOI La Buku 7 Huku WAKIPEWA KIBURI Na Mwenyekiti Wetu Wa Usajili Kapteni Wa Zamani Wa Jeshi La JWTZ Ya Kuleta USHABIKI Wa Siasa Na KUPENDA UKAWA Na MABADILIKO Yake Taifa Nasema NIMEFURAHI MNO KUFUNGWA Na Watani Zetu Yanga Football Club.

Nipo Ktk KAMATI Yenu Ya UFUNDI Na Muda Mwingi Huwa Nakuwa Na Wajumbe Akina Kajuna Na Tully Na Nadhani Kwa UTAMBULISHO Wangu Huu Viongozi MTAKUWA Mmeshanijua Mimi Ni Nani. Kumbukeni Ni Mtu Gani Leo MLIMKABIDHI Jukumu La Kuwamaliza Yanga Kuanzia Pale Getini Hadi Vyumbani Kwa Mambo Yetu Yale Ya KIUTAMADUNI. Nimezicheza Mno Mechi Za Yanga Zile 3 Zilizopita Na Tulizowafunga TENA HADI NIKIJITOA MUHANGA Hata KUHATARISHA MAISHA Yangu Kwa Kuipenda Simba Sports Club ILA Kwanza Kitendo Cha Majuzi Kumuona Hanspoppe ANAJIPENDEKEZA KUTOA MSAADA KWA Team Lowassa NILIKWAZIKA Mno Na Nakumbuka Hata Viongozi Wa Simba Walisikitika Na Kitendo Kile Huku Tukijua Kuwa Mheshimiwa Dr. Magufuli Ni Mwana Simba Sports Club Mwenzetu. Anyway Ile Ilikuwa Tisa Na Kumi Ni Kitendo KILICHONIPANDISHA Hasira Pale Taifa Ni Cha Wanasimba Kuanzia Baa Za Kule Nje MIANZINI Na Kwa MAMA CHICHI Muda Wote Badala Ya Kuzungumzia MPIRA Wao Wanazungumzia Tu Siasa Na Hasa Lowassa Na UKAWA Yake Na Hata WALIPOINGIA Ndani Ya Uwanja Muda Wote Walikuwa Wakisimama Na Kuonyesha ALAMA YA MABADILIKO Huku Mzee Hansppope AKIKENUA Tu MIMENO Yake Ya KIPOPOMA.

Nilipoona Hivyo KUDADADEKI Wala SIKUPATA SHIDA Na HASA UKIZINGATIA MZIGO Wote Wa MAANDAMIZI NILIKUWA Nao Wa KUFANYIA KAZI MAALUM Na Nilichokifanya Tena Kwa HASIRA Ni KUCHUKUA ILE MIZIGO Yote a.k.a MAKOMBORA Na Kwenda KUYATUPILIA MBALI CHOONI Kisha Nikapandisha Juu Kabisa MKABALA Na Walipokuwa Wamekaa Watangazi Akina SWEDI MWINYE Na JESSE JOHN Na Nikajilalia Zangu Na Kuna Watangazaji Wanaonijua Kuwa Mimi Ni Simba LIA LIA Walikuwa Wanashangaa Huku Wengine WAKICHEKA Na Nilichowajibu Kule Juu Ni Kwamba Simba Waende Kwa Lowassa Wao ATAWAPA USHINDI.

Na MSIPOBADILIKA Kujifanya MNAIPENDA SANA UKAWA Na Lowassa Wenu Na Kuleta USHABIKI Wenu Mpirani NAWAHAKIKISHIENI Kuwa NITAZICHEZA MECHI ZOTE ZA SIMBA Mpaka Mtatia ADABU Na Bahati Nzuri Sehemu Zote Za KIUFUNDI Huwa NAWAELEKEZENI Mimi Hivyo Hamna UJANJA Kwangu. Niombeni MSAMAHA UPESI Huku MKINIHAIDI Kuwa HAMTAGANYA TENA UPOPOMA WENU WA KULETA USHABIKI Wenu Wa UKAWA Na Lowassa Wenu Ndani Ya UWANJA. Simba Naipenda ILA CCM Na Magufuli Wake NAWAPENDA Zaidi.

Naomba Radhi Kwa Wana Simba Wote ILA Imenibidi Nifanye Niliyowafanyieni Na Kesho au Keshokutwa TFF Wanakaa KIKAO Cha KINIDHAMU Kutuzungumzia Kwa Kitendo Hicho Kwani WALICHATUONYA MAPEMA SANA Ila Sisi Leo Tumekaidi.

Jioni Njema Na Maumivu Mema Ya KICHAPO. Akhsante Sana Amissi Tambwe Na Malimi Busungu Na Shikamooni Wana Yanga Wote Mlio Ndani Na Nje Ya Tanzania Na Kwa Marafiki Zangu Vipenzi Mussa Mgosi Na Jonas Mkude MTANISAMEHE Sana Na Nawangojeeni Hapa Mango Garden Usiku Huu Kuanzia Saa 2 au Saa 3 Hii Tuje Kuserebuka Na Twanga Huku Tukizikatia Viuno Bao 2 Za Yanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gentamycine unakumbuka maneno yako haya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…