Kuna uhusiano gani kati ya sura/muonekano wa mtu na matendo yake?

Kuna uhusiano gani kati ya sura/muonekano wa mtu na matendo yake?

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Natumai wengi mtakubaliana nami kuwa Duniani tupo Watu wa aina tofauti..hii imepelekea wengi wetu kuhusisha baadhi ya matendo na aina fulani ya Watu. Kwa mfano kuna aina fulani ya Watu ukimkuta anafanya shughuli fulani lazima moyo wako utashtuka kwanza na utatamani kujiridhisha ni kwa nini Dada/ Kaka au Mama/ Baba huyo yupo kwenye shughuli ile.

Iwe ni Mwanamke au Mwanaume zipo sura au muonekano ambao utaona Mtu mwingine anatumia nguvu kubwa kukuaminisha kuwa Mtu huyo ni tofauti kabisa na anavyoonekana. Mathalani utamsikia Mtu akikuaminisha jinsi fulani alivyo na roho nzuri au upendo, na kinyume chake Wapo ambao inalazimika Mtu kumuelezea namna alivyo na ukosefu wa dabu na heshima ili tu usihadaike na muonekano wake.

Kuna Mtu ukiambiwa ni Mwizi au Jambazi anayevunja nyumba za Watu usiku basi utabaki na mshangao, na Wapo ambao ukiambiwa hivyo wala hutoshtukakwa jinsi Mtu huyo anavyoonekana.
 
Sura ya mtu inaakisi sana kilichomo ndani ya mtu huyo na mara nyingi inakuwa hivyo. Nilipokuwa mtoto mdogo kama miaka 5 hivi nilimwona mtu mmoja na kudhani ni mchawi. Nilipokuwa mkubwa nilishuhudia akishutumiwa kwa uchawi na hata yeye baadaye kukiri hivyo.
 
Hakuna uthibitisho wa kisayansi japo kuna wanasaikolojia wanaodai kuwa wanaweza kuona mema na mabaya; na hata uchungu na trauma katika sura ya mtu.

Hata akina Mshana watakwambia sijui kuna jicho la tatu kupitia kwenye macho/sura ila kimsingi hii ni taaluma ya kubahatisha tu sawa na watabiri akina Sheikh Yahaya na wengineo.

Baadhi ya ma-serial killers kama Teddy Bundy walikuwa na sura zenye bashasha na kuvutia sana kumbe.....
 
Kuna watu hawana miili, wembamba ila makatili,unakuta mtu bonge ila mwoga.

Sasa ukutane na wazee mwonekane wao wana heshima ila tabia za hovyo hata mbele za watu anaweza akasema matusi
 
Sura ya utulivu unyenyekevu
Matendo yakishetani
Hapa haswa ndio upo msingi wa hoja yangu.

Kwa nini sura au muonekano wa Mtu unakidhi kushawishi wengine kuwa Mtu huyu ni Mnyeyekevu au Mkorofi..ili hali tabia ni mambo ya ndani ya Mtu?
 
Hakuna uthibitisho wa kisayansi japo kuna wanasaikolojia wanaodai kuwa wanaweza kuona mema na mabaya; na hata uchungu na trauma katika sura ya mtu.

Hata akina Mshana watakwambia sijui kuna jicho la tatu kupitia kwenye macho/sura ila kimsingi hii ni taaluma ya kubahatisha tu sawa na watabiri akina Sheikh Yahaya na wengineo.

Baadhi ya ma-serial killers kama Teddy Bundy walikuwa na sura zenye bashasha na kuvutia sana kumbe.....
Kabisa, nakumbuka utotoni (enzi za video cassete) niliangalia muvi moja kwa rafiki yangu...tuliazima muvi library...siikumbuki jina ila ilikuwa muvi nzuri sana ya kipelelezi...kuna Dada alibakwa alfajiri akiwa anafanya mazoezi ya kukimbia(jogging)...basi katika kumtafuta Mbakaji walikamatwa/walihisiwa Watu mbalimbali mpaka mwishoni kabisa walipompata muhusika ambaye aliwaacha Watu wote wa mji ule vinywa wazi kwa kuwa tu muonekano wake haukuwahi kumfanya yeyote kumuhisi...jamaa alikuwa mtanashati, sura nzuri ya upole, Mtu anayeonekana kujali na kufuata taratibu na sheria n.k.
 
Kuna watu hawana miili, wembamba ila makatili,unakuta mtu bonge ila mwoga.

Sasa ukutane na wazee mwonekane wao wana heshima ila tabia za hovyo hata mbele za watu anaweza akasema matusi
Wapo Watu wanaochukulia (advantage) ya mionekano yao 'kuwapiga' wengine.

Na utamsikia au kuwasikia Watu wanasema "Yule Kaka hawezi kufanya hivyo" au "Yule Baba hawezi kukutapeli" n.k....kumbe anayejijua ni Mtu mwenyewe na nafsi yake.
 
Kuna wataalam wa zamani kidogo wa mambo ya sheria waliamini kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya umbo la mtu na matendo yake. Wasomi hawa wakiongozwa na Caessor Lombroso na Enrico Feri waliamini kuwa, watu walio na vinyweleo vingi, mikono mirefu na yenge nguvu, taya na vichwa vikubwa etc kwa asili yao ni watu waovu. Yaani watu hawa wanazaliwa na uovu ndani yao (reo nato).
Lakini baadae ilionekana wazi hii nadharia ilikuwa ya uongo. Kuna walioamini pia kuwa uovu wa watu huzidi kadiri mtu anavyosogelea mstari wa equator.
Hitimisho ni kuwa " science is yet to establish how to read human mind basing on physical appearances
 
umenikumbusha movie moja ya kikorea ili ujue tabia ya mtu kulikuwa na wataalamu wa kusoma sura yako wanajua tabia yako ikoje
 
Ila wazinzi hujulikana kabisa[emoji125][emoji125][emoji125]
 
Ila wazinzi hujulikana kabisa[emoji125][emoji125][emoji125]
Hapa ndio nakataa...ingawa labda yaweza kufanya kazi kwa wale wa jinsia ya KE.

Mimi kuna Msichana/Mwanamke nikimuangalia naweza ku imagine kabisa kwamba huyu si wa kutulia...hata kwenye porn kuna sura nyingine mpaka unatamani kuhakikisha kama kweli "anafanya" ili hali kuna sura nyingine unaona kabisa hapa ni kipele kimekutana na mwenye kucha.

Huwa roho inaniuma nikimuona Demu mwenye sura "innocent" anashiriki porn...tena unakuta yupo three sum ya ma men wawili...naumwa roho na wivu wakati huo huo.
 
Huu mtazamo una ukweli...mfano tu mrahisi ...handsome men wengi ni wastarabu na wapole na wapenda amani,hivyo hivyo kwa wanawake wanawake wanzuri na sio uzuri wakutafutwa kwenye makopo...wengi wao waaroho nzuri na wastarabu na wapole..

Pia jaribu kuangalia viongozi my handsome..mfano Idd-Amin na Obote..n.k
 
Hapa ndio nakataa...ingawa labda yaweza kufanya kazi kwa wale wa jinsia ya KE.

Mimi kuna Msichana/Mwanamke nikimuangalia naweza ku imagine kabisa kwamba huyu si wa kutulia...hata kwenye porn kuna sura nyingine mpaka unatamani kuhakikisha kama kweli "anafanya" ili hali kuna sura nyingine unaona kabisa hapa ni kipele kimekutana na mwenye kucha.

Huwa roho inaniuma nikimuona Demu mwenye sura "innocent" anashiriki porn...tena unakuta yupo three sum ya ma men wawili...naumwa roho na wivu wakati huo huo.
Ila walio wengi wapo hivyo, wana matamanio yanayo onekana kabisa
 
Hakuna uhusiano isipokuwa ni Jamii ndio inasababisha haya. Yaani ukiwa na sura mbaya utadharaulika utatengwa ,sofa zako mbaya ndo zitakuzwa. Ukifanya wema unapuuzwa ila ukikosea ukafanya ubaya ndo utakuzwa ill muradi tu uonekane adui. Sasa mwisho wa siku mtu anakua adui kweli kwa kua anaona Jamii yote haimkubali.

Na wale wenye sura nzuri zenye mvuto ni kinyume chake hata wakiwa waovu Jamie haiwatengi wala kuwasimanga matokeo yake wanazidi kufanya uovu.
 
Mtu anayekunja kunja mdomo au ana mdomo anaouvuta vuta huyo ni mkorofi au mpenda fitina na ugomvi.
 
Mtu anayekunja kunja mdomo au ana mdomo anaouvuta vuta huyo ni mkorofi au mpenda fitina na ugomvi.
Ila kiukweli kuna Watu wana muonekano wa kiburi kwa kumuona tu mara ya kwanza.
 
Back
Top Bottom