Wanajamvi,, Jana kuna orodha ya watu takribani 65 Mubasharah iliwekwa hadharani kuonyesha jamii kuwa watu hawo wanajihusisha kwa namna moja au nyingine
,, MIHADARATI ,,
Nisicho muelewa Manji ni kuhusisha tuhuma dhidi yke na Club ya Yanga,, kwamba yeye ni mwenyekiti wa klub kubwa hivyo hapaswi eti kuitwa kuhojiwa,,
Tuhuma zinapomkabiri mtu hazizingatii umaarufu au wadhifa wa mtu,, kwa haraka haraka nilikigundua kwa Manji ni kutaka aonewe huruma na kupandisha jazba kwa mashabiki wa klabu yke ili waone kama mwenyekiti wao kaonewa ikiwezekana wahamasishe fujo ili kupinga kutajwa kwake.
Wala Manji hapaswi kujipangia muda na sk ya kwenda pale Central,, anapaswa kutii mamlaka kaambiwa aende siku ya Ijumaa sio Alhamisi.Maana tumeambiwa tuzitii hizi mamlaka,,
Yeye kama ni Mwenyekiti wa Yanga,, bado anapaswa kukumbuka pia kuwa hii Yanga ipo ktk mkoa wa Dar,, na aliyetoa agizo hilo ndiye mkuu wa lpmkoa huu.
Leo nimeshangaa Nakala nyingi za gazeti la Jambo leo zikigawiwa bure ktk ofs nyingi za Umma,, makala nyingi zinaelezea huduma na mambo mbali mbali ya Manji,,
Kwanin haya magazeti yagawiwe bure leo na siyo kesho au juzi? HAPANA MANJI AFUATE TARATIBU AACHE HIZI FUJO ZA KWENDA KULIPOTI SK AMBAYO HAKUPANGIWA.